Watu wauawa, Ofisi zachomwa Mtwara | Bunge la jioni lasitishwa - Hali ni tete...

Binafsi ningenda hiyo gesi isichimbwe kabisa mpaka ccm Wang'oke madarakani.

Maana ccm kazi yao na kusaini tu bila kujua wanasaini nini kwa maslai ya nani.!!
 
Mkuu Mnyinda,unachokisema ni sahihi saana,mfano mzuri angalia kinachotokea Mtwara sasa.Kuna post moja nimetoka kuisoma sasa hv kwenye uzi mmoja anasema" mtu mjinga akigundua kua unamuibia halafu akacharuka,hua ni hatari kuliko mkorofi"

nikweli@BBJ@siyo mtwara peke yake angalia na loliondo,monduli,mbeya,arusha,iringa,nakwineko kla kona watu wanataka hakizao,
 
[FONT=courier
new]Kwani Dr. Slaa amesemaje mpaka sasa....mwenye kujua
atujuze. Namshauri pia awatulize wananchi wake wa
Mtwara
[/FONT]

Kama wameshindwa kuwaamini wenye mamlaka watamuaminije huyu ambaye hata wazo kwamba Mtwara kuna gesi ni ndoto kwake?. A cha unazi wa kisiasa kuchekelea wakati watu wako ktk wakati mgumu.
 
Kwa ninachokiona hapa ni kwamba kwa kiburi cha serikali na maisha magumu tuliyonayo wananchi tunajenga mianya ya wabaya wetu ( kwa maana ya mataifa ya nje na watu wachache wasiopenda amani yetu) kujipenyeza na kufanya matukio ya kigaidi. Tunajenga mazingira ya mataifa ya magharibi kujipatia ajira kwetu kwa kigezo cha waangalizi wa mwenendo na amani ya nchi. Sifurahii kufikia hatua ya kuuana sisi kwa sisi, maana hata polisi ni kaka, dada zetu na wazazi wetu. Lakini hii ni ishara tosha ya kwamba wananchi hawana imani na serikali yao. Na kama viongozi ni waadilifu na wawazi kama wanavyojinadi, ni muda muafaka wa kuonesha hilo kwa kuwajibika. Kwa mtizamo wangu, kuna shida gani wakijenga mtambo wa kusindika hiyo gesi (samahani kama nimetumia neno lisilo sahihi) kisha ikasafirishwa kwenda kwenye masoko mengine ya ndani na nje? Itatoa fursa ya ajira kwa wana mtwara na watanzania wengine. Itatoa fursa ya biashara kwa bandari ya mtwara na pia kufanya fair industrial distribution. Kitendo cha kukazania gesi kuja dar pia kinaleta maswali mengi. Gharama ambazo zingetumika kujenga bomba zingefanya miradi mingine ya kimaendeleo. Maana naamini pia lazima kujengwe mitambo mingine dar ambayo ingejengwa mtwara. Wananchi wa haki ya kudai mali yao wanapoona kuna dhuluma. Nawakilisha.
 
Duuh, wamakonde ni nouma aisee? Kumbe muungwana akigundua una muonea kwa sababu ya uungwana wake ni hatari kuliko mkorofi!

Wamakonde siku zote ni noumer, hata enzi zile za nduli idi amini walichapa sana wale waganda. Hapa ukijifanya Ghandi utakufa kifo kibaya sana, heri wachuchukue mishale yao and baruti za samaki piga ua. Hivi kama kilieleweka misri kwanini kisieleweke huku?
 
Serikali itumie busara ktk hili hakuna popote nguvu za dola zimewahi kudumu maisha, hili la gesi litufumbue macho
 
kuna gari ya wanajeshi kutoka nachingwea kuja mtwara kusaidia imepata ajali mbaya njia yaani wameumia hata kabla haijafika

Mh kweli Gas haitoki hata kwa bomba la pen!! Mpaka kunakucha kesho tutasikia Mengi!! Viva mtwara mnaelewa kuwa hakuna Dhambi mbaya na kubwa kama dhambi ya woga..
 
Haya ya Mtwara yangetokea kaskazini wangesema ni UKANDA na chanzo ni vurugu za CDM. Ya Mtwara tuyaiteje? Na chanzo chake tukiite UDINI? U-CUF? au UKABILA?
 
Tamko la serikali lipo wazi kwamba Bomba la Gesi Ntwara hadi dar linajengwa kwa gharama yoyote: no changes; ila tu watapeleka askari wengi kudhibiti mgomo wa wana mtwara wakidhani hilo ndilo suruhisho..

Mkuu hapo kwenye bold nadhani Bi mkuu /madam Spika............ hajaliona au kusikia kwenye Bajeti ya Waziri husika.
Anaahirisha Bunge kuhitaji tamko gani tena?-Angetoa mwongozo wa Tamko na kwamba Bunge litapiga kura kuafikiana na hoja husika ! zaidi ya hivyo ni kupoteza kodi zetu Bure kwa kuongeza muda wa Bunge kuwa Dodoma.

Matarajio ya baadhi ya hoja!

1. Kwamba Serikali iendelee kupeleka askari wengi kudhibiti mgomo wa wana mtwara kwa matumaini ya kuwa hilo ndilo suruhisho..
2. Mradi usitishwa mpaka Serikali itakapo kubaliana na Wananchi wa Mtwara
3. Kuafikiana na matakwa ya Wana Mtwara kuwa gesi isitoke kwa Bomba.
 
Nimeeleza kwa ufasaha sana ni kwanini kuna uharaka wa kusafirisha gesi sasa. "Eti tusubiri miaka kumi hadi tutakapopata uwezo wa kujenga PowerPlant Mtwara, ilihali uwezo wa kusafirisha sasa hiyo gesi tunao. Kwanini tusiokoe uchumi unaodidimia kutokana na ukosefu wa umeme, kwa kuamua kusafirisha hiyo gesi ili iokoe hali ya mambo iliyopo nchini hivi sasa?

Kuhusu swali lako la pili, kama tatizo ni mikataba, basi iwekwe wazi kwamba kinachogomewa ni mkataba. Ni ukweli ulio dhahiri ambao pia umedhihirisha na Dr F. Ndugulile kwamba gharama za ujenzi wa hili bomba ni mara nne ya gharama halisi.

Tatizo tulilonalo ni la hawa wabunge wa CCM kama akina Ndugulile, wanajua matatizo yaliyopo, lakini mbunge wa upinzani akisimama kutoa hoja kama hiyo.

Sasa we una tofauti gani na CCM, Ukweli wote unaujua, halaf unapinga wanachofanya Wanamtwara.
 
Last edited by a moderator:
nchi hii ina mengi ya kutufunza,na huko tuendako ni kubaya zaidi,wewe jiulize kama serikali hii inavyo jiita kila siku ni serikali sikivu,kwanini wanafanya mambo yao kwa uficho,usiri mkubwa tatizo hapo ni nini?wamakonde bwana ogopa,ata vita vya MAJIMAJI VILIANZIA HUKOHUKO MTWARA,kazi wanayo magamba

Natamani isambae nchi nzima.
 
Inasikitisha! Kiburi na ubabe wa watawala ndo umeifikisha Mtwala hapa ilipo. Kamwe nchi ya kidemokrasia haiwezi kuongozwa kwa risasi na mabomu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom