Watu hawakumuelewa Rais Magufuli

Watanzania wengi hatuna kumbukumbu na huwa hakuna maandishi mengi kuhusu Tanzania ya miaka ya nyuma na yaliyopo kidogo watu hatusomi. Haya mambo ya kukamata wazururaji yalikuwepo sana. Watu walihamishiwa mpaka kwenye vijiji vya ujamaa kwa nguvu! Na utendaji wa aina ya Magufuli sio mpya. Mrema alikuwa maarufu na anasifiwa kuliko Magufuli. Kwa kifupi Magufuli anaongoza kwa staili ya miaka ya nyumba ambayo mafanikio hayakupatikana. Ngoja niwaache na kibao cha Urafiki Jazz Band cha Gezaulole. Kipindi hicho ndicho ''wazururaji'' wanakamatwa kweli kweli. Polisi wakipita wanakusanya makundi ya vijana wasio na vitambulisho halafu wanawatoa kitu kidogo na kuwaachia.


Sema wewe, tukisema wengine watasema huyo Kiranga tu.

Magufuli hajui hata economic theory moja. Anahangaika tu.

Kibaya zaidi, hana hata utashi wa kujua. Anabaki kutaja boiling point ya silver na kilomita za barabara tu.

Ndiyo maana anarudia ukomunisti ambao ushatupwa kwenye jalala la historia.
 
Futeni katiba na uchaguzi basi, rais achaguliwe na kitengo na kutawala kisultani.

Ya nini kupoteza hela nyingi kwenye uchaguzi na kuhadaa ulimwengu?
Kwa hiyo wabunge na madiwani wanachaguliwa na kitengo!, ina maana tunazo fedha nyingi sana za kupoteza!. Rudisha akili yako kwenye maisha halisi unayoyaishi kwa sasa, hizo dreams na fantasies ulizonazo zitakupatia maumivu ya moyo, maumivu ambayo hakuna daktari atakayeweza kuyatibu.
 
Kwa hiyo wabunge na madiwani wanachaguliwa na kitengo!, ina maana tunazo fedha nyingi sana za kupoteza!. Rudisha akili yako kwenye maisha halisi unayoyaishi kwa sasa, hizo dreams na fantasies ulizonazo zitakupatia maumivu ya moyo, maumivu ambayo hakuna daktari atakayeweza kuyatibu.
Maisha halisi ninayoishi kwa sasa yakoje na umeyajuaje kwamba yako hivyo?
 
Sema wewe, tukisema wengine watasema huyo Kiranga tu.

Magufuli hajui hata economic theory moja. Anahangaika tu.

Kibaya zaidi, hana hata utashi wa kujua. Anabaki kutaja boiling point ya silver na kilomita za barabara tu.

Ndiyo maana anarudia ukomunisti ambao ushatupwa kwenye jalala la historia.
Rais ni taasisi sio mtu mmoja, na hili ni jambo la kawaida kabisa ambalo unatakiwa ulifahamu. Kuna vitengo vingi vinavyokuwa chini yake. Utakuja kumuelewa vizuri kadri siku zinavyopita.
 
Maisha halisi ninayoishi kwa sasa yakoje na umeyajuaje kwamba yako hivyo?
Maandishi yako ni taswira ya roho yako. Wewe kumuona JPM hafai ni chaguo lako, lakini itabidi uvumilie kwa miaka mingi sana mpaka kile unachokitaka kiweze kufanikiwa.
 
Maandishi yako ni taswira ya roho yako. Wewe kumuona JPM hafai ni chaguo lako, lakini itabidi uvumilie kwa miaka mingi sana mpaka kile unachokitaka kiweze kufanikiwa.
Hujajibu uliloulizwa na ulilojibu kama ni jibu, si la swali nililouliza.

Roho ni nini? Unaweza kuthibitisha ipo? Au ni ndoto yako kama "Magufuli ni straightforward" ?

Mtu aliyeuza nyumba za serikali kwa hawara wake na mdogo wake kinyume cha taratibu za serikali hawezi kuitwa "straightforward" nje ya ndoto za cheerleaders na fanboys.
 
Hujajibu uliloulizwa na ulilojibu kama ni jibu, si la swali nililouliza.

Roho ni nini? Unaweza kuthibitisha ipo? Au ni ndoto yako kama "Magufuli ni straightforward" ?

Mtu aliyeuza nyumba za serikali kwa hawara wake na mdogo wake kinyume cha taratibu za serikali hawezi kuitwa "straightforward" nje ya ndoto za cheerleaders na fanboys.
Hapa ndipo panapo nifanya nimasome kwa ukaribu KIRANGA.
 
..Raisi anakosea kutoa kauli za VITISHO.

..pia kuwahimiza ma-rc na ma-dc kuwasweka mahabusu kwa masaa 48 watendaji wa serikali kunaweza kusababisha uonevu kwa wananchi wasio na hatia.

..zaidi utaratibu na pilikapilika za kukamata vijana wasio na kazi siyo jambo jipya hapa nchini. But one thing has remained constant, utaratibu huo haujawahi kutatua tatizo la uzururaji ambalo linasababishwa na ukosefu wa ajira.

..uchumi wetu, kutokana na sera mbovu za ccm, hauzalishi ajira za kutosha na zinazovutia kwa vijana wetu na hi yo kusababisha wazurure mitaani. Sijui kama unakumbuka tukio la vijana kujaa uwanja wa taifa wakati idara ya uhamiaji ilipotangaza nafasi za kazi.

..kwa hiyo Raisi na watendaji wake warudi kwenye drawing board na kuja na mikakati ya kupambana na tatizo la UKOSEFU WA AJIRA.

Viongozi, waje na mbinui ya kubuni miradi yenye kuibua nafasi za ajiri.
 
Hebu ipitie upya utaona ukweli wa nilichokisema
Kusema alisema.

Na mimi nasema na nitaendelea kusema Watanzania ni wavivu, wanapenda utajiri wa haraka haraka wasioutolea jasho. Hata hivyo sheria ya nchi inamruhusu mtanzania kuwa mahali popote ili mradi havunji sheria. Sasa tujue tu sheria zinasemaje.

Sasa tuone Watekelezaji wataichukulia literary au wataongeza na yao? Baa hazitakiwi kuuza alcohol kabla ya saa kumi au hawaruhusiwi kufungua kabla ya muda huo? Hizo kambi zilishaandaliwa? Nani atazisimamia? Watalala wapi na kula nini? Wananchi wanaojiajiri wamepangiwa mpango gani wa vitambulisho vya kazi?

Hiki kitu kinahitaji utekelezaji mzuri.
 
Kusema alisema.

Na mimi nasema na nitaendelea kusema Watanzania ni wavivu, wanapenda utajiri wa haraka haraka wasioutolea jasho. Hata hivyo sheria ya nchi inamruhusu mtanzania kuwa mahali popote ili mradi havunji sheria. Sasa tujue tu sheria zinasemaje.

Sasa tuone Watekelezaji wataichukulia literary au wataongeza na yao? Baa hazitakiwi kuuza alcohol kabla ya saa kumi au hawaruhusiwi kufungua kabla ya muda huo? Hizo kambi zilishaandaliwa? Nani atazisimamia? Watalala wapi na kula nini? Wananchi wanaojiajiri wamepangiwa mpango gani wa vitambulisho vya kazi?

Hiki kitu kinahitaji utekelezaji mzuri.
Sheria inaelekeza zifunguliwe saa 10 jioni zifungwe saa 5 usiku. Hilo la kupelekwa kambini ni wale watakaokaidi kufanya kazi.
 
Hujajibu uliloulizwa na ulilojibu kama ni jibu, si la swali nililouliza.

Roho ni nini? Unaweza kuthibitisha ipo? Au ni ndoto yako kama "Magufuli ni straightforward" ?

Mtu aliyeuza nyumba za serikali kwa hawara wake na mdogo wake kinyume cha taratibu za serikali hawezi kuitwa "straightforward" nje ya ndoto za cheerleaders na fanboys.
Huyo huyo aliyeuza nyumba za serikali watu milioni nane wamemchagua. Maswali mengi ya kitoto hayafai kujibiwa, ndio maana siyajibu. Umarekani unakusumbua kaka, unaongelea cheerleaders na fanboys kwenye issue ya siasa za bongo. Tuliza mzuka JPM ndio rais wako, wakikuuliza marafiki zako ambao sio watanzania waambie hivyo, huyo uliyenaye moyoni mwako wala hawamjui.
 
Huyo huyo aliyeuza nyumba za serikali watu milioni nane wamemchagua. Maswali mengi ya kitoto hayafai kujibiwa, ndio maana siyajibu. Umarekani unakusumbua kaka, unaongelea cheerleaders na fanboys kwenye issue ya siasa za bongo. Tuliza mzuka JPM ndio rais wako, wakikuuliza marafiki zako ambao sio watanzania waambie hivyo, huyo uliyenaye moyoni mwako wala hawamjui.
Tatizo unajadili watu, wakati mimi najadili dhana na taasisi.

Tupo level tofauti katika upevu wa fikra.
 
Tatizo unajadili watu, wakati mimi najadili dhana na taasisi.

Tupo level tofauti katika upevu wa fikra.
Hizo taasisi zinasimama vipi bila ya hao watu?, kaka jioni hii unapata kinywaji sehemu wakati tunaongea?. Naona kama vile unapoteza mwelekeo wa maongezi. Wewe hujadili taasisi unapenda ligi ya ubishi, umezoea ubishi wa mitaani, suala la taasisi nililiongelea muda uliopita kuhusiana na usaidizi anaopewa rais akiwa ikulu.
 
Hizo taasisi zinasimama vipi bila ya hao watu?, kaka jioni hii unapata kinywaji sehemu wakati tunaongea?. Naona kama vile unapoteza mwelekeo wa maongezi. Wewe hujadili taasisi unapenda ligi ya ubishi, umezoea ubishi wa mitaani, suala la taasisi nililiongelea muda uliopita kuhusiana na usaidizi anaopewa rais akiwa ikulu.
Watu watafanya kazi vipi kwa ufanisi bila taasisi?

Kama ungeelewa umuhimu wa taasisi wala usingetetea udikteta hapa.

Halafu umezidi ku assume na kuota, jioni ikiwa kwako unajua dunia nzima jioni?

Too many assumptions.
 
Watu watafanya kazi vipi kwa ufanisi bila taasisi?

Kama ungeelewa umuhimu wa taasisi wala usingetetea udikteta hapa.

Halafu umezidi ku assume na kuota, jioni ikiwa kwako unajua dunia nzima jioni?

Too many assumptions.
He he he kaka unapenda sana ligi ya mdomoni. JPM anafanya kazi yake ambayo watanzania wamemtuma kuifanya, hii issue ya taasisi unaleta sasa baada ya kushindwa kujenga hoja zenye mantiki kuhusiana na aina ya rais unayemtaka wewe ambaye hafanani na huyu wa sasa. Nchi ngapi za kiafrika zenye taasisi zenye kufanya kazi nzuri ambazo wewe unazifahamu, usije ukawa unaota yale mambo ya Marekani ndio yawe hapa bongo.
 
Sheria inaelekeza zifunguliwe saa 10 jioni zifungwe saa 5 usiku. Hilo la kupelekwa kambini ni wale watakaokaidi kufanya kazi.
Kazi gani?

Nashindwa kucomment vizuri kwa vile nina doubts na uwezo wa Viongozi wa kubuni njia bora za kutekeleza vyema maagizo hayo.

Ambacho ningependa kufahamu Magufuli amepewa deadline na nani? Imetuchukua miaka 30 kufika tulipofika, kweli inawezekana kubadilika ndani ya mwaka mmoja? I'm not talking about the economy tu, nahoji pia attitudes na hata maadili ambayo tumeyaadopt.

Kuhusu kilimo: mtu ambaye amewahi kulima atakwambia kilimo siyo rahisi kama inavyosemekana humu. Ukitoa changamoto ambazo ni controllable kama pembejeo, washauri nk na hizi bado zinaleta shida, kuna zile ambazo ziko nje ya uwezo Kama vile mvua, Jua kali, upeo, milipuko ya magonjwa ya mazao
 
Habari wana JF
Jana Rais Magufuli aliwahutubia kwa muda mfupi wakuu wa mikoa baada ya kuwaapisha. Rais aliongea mambo machache lakini yaliyobeba maana kubwa kuhusu uwajibikaji na watu kufanya kazi hasa akitia msisitizo kuwa tumeshachelewakwa kuwa haya yalitakiwa kuanza miaka kumi iliyopita.
Ni ukweli uliyodhahiri kuwa tumechelewa tena sana kutokana na nchi yetu iliyojaliwa kuwa na raslimali nyingi pamoja na ardhi kubwa yenye rutuba.
Jambo la kushangaza watu wameibuka na kauli mbalimbali wakiwemo wanasiasa, ambazo zimebadili maana halisi iliyokuwa kwenye baadhi ya maneno ya Mh. Rais.

Mh. Rais aliwaambia ma-RC "kuna watendaji wengine kazi yao ni kuwanyanyasa wananchi nendeni mkawashughulikie. Nyinyi mna mamlaka ya kumweka mtu ndani masaa 48, wawekeni ndani ili wawaheshimu wananchi". Lakini kauli hii imepindishwa na watu, hata wengine wakisema wakuu wa mikoa wameagizwa waende kuwakamata vijana wasiokuwa na kazi!
Hivi kweli hawa wakuu wa mikoa ni watu wasiojitambua ambao wanaweza kuitumia sheria inayowapa mamlaka hayo kuwaonea watu wasiokuwa na hatia?

Jambo jingine ambalo linapotoshwa ni kauli ya Rais kuzuia watu kucheza pool table asubuhi na kuwataka vijana kufanya kazi badala ya kuzurura pale alipokazia kuwa ikiwezekana walazimishwe kufanya kazi kwenye kambi maalum.
Watanzania wenzangu hivi ni kutokufuatilia sheria au ni upotoshaji wa makusudi? Niwaulize wanasheria akina Tundu Lissu, sheria inasemaje kuhusu muda wa kufungua bar na sehemu mbalimbali za starehe? Sheria inasemaje kuhusu uzembe na uzurulaji?
Mimi sioni kama mh. Rais ametunga sheria mpya ya kwake bali anasimamia sheria ambazo zilikosa usimamizi ambazo leo ni matokeo yaliyozalisha makundi ya vibaka mitaani.

Hapa Tanzania haiingii akilini kwa mtu anayejua hasa kutumia zile dutu nyeupe zilizo katika fuvu la kichwa ukimwambia hakuna kitu chochote cha kufanya kukuingizia kipato. Huko ni kukosa ubunifu na kuyaacha mambo yaende kwa kudra za Mwenyezi Mungu. Katika nchi iliyo na ardhi zaidi ya 70% haijakaliwa na watu wala haimilikiwi na mtu. Ardhi ni mtaji wa kwanza kwa sababu juu ya ardhi ndipo kila kitu kinafanyika.

Kila Mtanzania aliye na akili timamu kutoka moyoni mwake ukiacha anachokisema mdomoni ili kuwahadaa, anajua kuwa sasa hivi vijana wengi wamekuwa wavivu hawataki kazi ngumu, wamekuwa ni watu wanaotaka kuvuna wasipopanda. Kiasilia hilo jambo halipo wala haliwezekani, hata Simba porini anapambana kupata mawindo.

Rai yangu kwa Watanzania wenzangu, acheni kupotosha maana halisi ya maneno ya Mh. Rais ambaye ameonesha uthubutu wa kukemea maovu yaliyokuwa yameshamiri hapa nchini. Ili Tanzania isonge mbele hata tufikie katika huo uchumi wa kati, haina budi kila Mtanzania kutimiza wajibu wake kwa moyo wa uzalendo, na si kukosoa kila jambo ilimradi kila mtu aonekane anajua kuliko mwenzie.
Wanasiasa wa vyama vya upinzani acheni kuwa na roho zilizojawa na hamu na maombi ya kuiombea serikali ishindwe mpate mashiko katika uchaguzi ujao. Hivyo mtakuwa na malengo ya kushika dola tu na si kutaka Tanzania iendelee. Kwani Nchi inaweza endelezwa na yeyote na chama chochote.

Nahitimisha kwa kusema nchi ilipofikia haitaji tena siasa wala kubembelezana, sasa twende kwa mwendo wowote ikibidi hata kukimbia ilimradi tufike.
You might be right, but only chademalaria fans made the speech upside-down. Thank for backup. Merci becoup mwaaest....
 
Sheria gani inayopanga muda Wa kucheza pool?
Usikimbilie ya uzururaj, haihusu
KUMBUKA pool ni michezo ya club, watu tu wamefoji wakaleta hadi mitaani.
HIVI kwa akili ya kawaida pool can make you earn a living?
 
Wewe unawaza hili sasa. Lakini hujui yalishafanyika miaka iliyopita na matokeo yake yalikuwa 0. I wish nchi ingekuwa rahisi hivyo kuongoza kwani ungekuta tuna maendeleo kibao. Mimi sipendi uvivu na najua watanzania wengi ni wavivu lakini hii njia haifanyi kazi...

Njia ipi inafanya kazi?
 
Back
Top Bottom