Watoa huduma na wafanyabiashara badilikeni katika hili

aise

JF-Expert Member
May 16, 2018
4,124
11,992
Kuna hii kasumba sijui tuseme ulimbukeni limeenea sana kwa wafanya biashara na watoa huduma.

Mfano unaenda dukani kununua shati, muuzaji anakwambia bei ya shati ni 40,000.

Wakati shati kama hilo kwa kawaida huwa bei yake ni 15,000, Sasa unamuuliza mbona bei sana? Anajibu "ulikuwa na sh ngapi?"

Unamjibu, basi bwana, (huku unaondoka) umeanzia juu sana, mimi nilidhani labda itakuwa 12,000.

Unaondoka zako anakuita "boss rudi ongeza buku basi nikuachie"

Hivi kwanini usimwambie mteja wako bei inayoeleweka?

Kwangu mimi nikiona mtoa huduma ana hiyo kasumba huwa namdharau sana na hatawahi tena kuniona narudi kwake.

Badilikeni aise, wengine kukaa unalialia na muuzaji eti apunguze bei hatuwezi.

Taja bei ya kueleweka siyo unataja bei za kidalali.
 
DFB6E26B-A28F-4E8C-AD0A-66FDFE48D662.jpeg
yaani mimo huwago sichukui kabiso akinianzio bei juu hivu nikimpa mgongu sigeuki teno haiwezekano uniibiii hvhv nakuono
 
Ni kawaida sana kwa watafta riziki na hakuna bei elekezi yupo mtu akiuliza ukimtajia 40k anatoa anachukua kungekua na bei elekezi ya bidhaa watu wasingefanya hivyo.

Alafu kuna namna ya kwenda kufanya manunuzi
 
Ni kawaida sana kwa watafta riziki na hakuna bei elekezi yupo mtu akiuliza ukimtajia 40k anatoa anachukua kungekua na bei elekezi ya bidhaa watu wasingefanya hivyo.

Alafu kuna namna ya kwenda kufanya manunuzi

Nakubaliana na wewe mkuu,
Ila kwanini utoke kwenye 40k, 30k, 20k mpaka uje uuze kwa bei ya 12k?
Huoni hapo kati kuna watu (kama mimi) ambao hatuwezi kuombaomba upunguze bei umetupoteza?
Wewe bidhaa umenunua 5k, unataka uiuze 25k, mara uiuze 20k, mara 15k, 10k, 7k, yaani hueleweki.

Kwanini usiweke bei moja ya kueleweka kwenye bidhaa yako ili iuzike haraka na kwa wingi kuliko kuweka bei za kidalali?

Mwisho wa siku watu wanakuja wakisikia bei hawaongei mara mbili wanaondoka.
Kumbe ungeweka bei zilizonyooka ungeuza bidhaa nyingi na ungepata faida mara dufu kuliko kuweka bei za kidalali.

Wewe bidhaa umenunua 5k, ukipiga hesabu ukaona ukiiuza kwa 8k itakulipa, uza kwa bei hiyo, hakuna haja ya kumwambia mtu eti 30k
 
Bongo longo longo nyingi sana ujanja wa kishamba unawafanya biashara zinadoda.

Kuna hili kundi la watu wana-post bidhaa mtandaoni bila kuweka bei ya bidhaa ili uingie DM akupige.

Tufanye biashara kisomi zaidi, tupunguze tamaa weka price tag halisi ya bidhaa yako.
 
Ndio biashara ilivo unaanzia juu ili akibargain ukishusha usipate hasara au ili akija kizembe unampiga!
 
Back
Top Bottom