The Evil Genius
JF-Expert Member
- Mar 21, 2014
- 5,465
- 17,307
Watanzania sijui watashtuka lini. Lakini hii ni uthibitisho wa fikra za Darwin kwamba hapa Duniani ni eitha uchague kua chakula uliwe ama uchague kua mla chakula.
Siku zote wala chakula hutafta chakula kilichoiva wakile, wakikukuta umejikalia kama chakula kilichoiva lazima utaliwa tu.
Watanzania wakiwemo viongozi wa dini wametapeliwa na kampuni ya Upatu inayoitwa Best Capital Management ambayo ilikua na ofisi pale karibu na Ubalozi wa Marekani.
Kampuni hiyo ili kujiunga ulipaswa kua na mtaji usiopungua milioni 23 kama kianzio. Watu waliweka hadi Bilioni 1.
Mwanzoni mwa uwekezaji, watu walikua wanalipwa faida bila shida ila baadae malipo yakaanza kusua sua, ukienda ofisini hakuna mtu hapo ndio baadhi ya wawekezaji wakakimbia polisi, muwekezaji mkuu akakamatwa na baadhi ya mali kuuzwa na kulipwa wawekezaji lakini idadi kubwa ya wawekezaji wameliwa pesa zao na mmiliki wa makampuni hajulikani alipo
Sijui ni kwa nini watanzania hawabadiliki.
Kabla sijamalizia naomba nitoe ushauri. Kama unataka kuwekeza, nenda kwa kampuni zilizosajiliwa kwenye masoko ya uwekezaji. Pamoja na hilo ujitidhishe vitu vifuatavyo.
1. Iwe ni kampuni iliyosajiliwa na mamlaka zinasosimalia uwekezaji kama Capital Market and Security Authority.
2. Kampuni iwe inaandaa hesabu za wazi(public accounts) na zinandaliwa na mhasibu aliesajiliwa NBAA na pia zinakaguliwa na kampuni iliyosajiliwa NBAA kama kampuni ya ukaguzi. Pia hapa ujiridhishe na uwezo wa kampuni ya ukaguzi, haiwezekani kampuni ina mtaji wa Bilioni 20 ikaguliwe na kampuni ndogo ya ukaguzi. Hapo uwe na mashaka. Taarifa za wahasibu wlaiosajiliwa NBAA na wakaguzi zinapatikana kwenye website ya NBAA.
3. Kampuni iwe inalipa kodi TRA kwa kutumia hesabu ama vitabu vya hesabu. Kampuni yoyote inayofanya biashara halali na inapata faida lazima iwe inaandaa hesabu na zinapelekwa TRA kwa ajili ya makadirio ya kodi.
4. Kampuni inajaza marejeo ya Brela(File Annual returns). Kampuni yoyote inayofanya biashara halali lazima ijaze taarifa muhimu Brela kila mwaka. Taarifa hizi ni muhimu kwa sababu zinakupa picha ya kujua wamiliki, biashara wanayofanya, mabadiliko yoyote ya wamiliki ama wakurugenzi nk. Annual returns za Brela ni tofauti usajili wa Brela. So annual ni bora zaidi.
Hesabu zilizokaguliwa zinakupa picha ya wanachama wangapi, pesa iliyoko bank ni kiasi gani, faida iliyopatikana ni kiasi gani nk.
Uwekezaji usitumie rafiki ama ndugu yako akushauri, tafta wataalamu wa masuala ya fedha wakushauri. Leo hii unaweza kujifunza masuala muhimu ya fedha bila hata kua mhasibu. Unaingia YouTube, google, chat GPT unauliza kwenye vitabu vya hesabu niangalie wapi muhimu na kila unachokiangalia kinakwambia nini utapata majibu.
Usiweke hela yako mahala kwa kutumia ushawishi ama ushauri wa marafiki. Utapoteza pesa na utapata hasara.
Wadau mnaweza kuongeza nini watu waangalie wasijikute wanapigwa na upatu.
Siku zote wala chakula hutafta chakula kilichoiva wakile, wakikukuta umejikalia kama chakula kilichoiva lazima utaliwa tu.
Watanzania wakiwemo viongozi wa dini wametapeliwa na kampuni ya Upatu inayoitwa Best Capital Management ambayo ilikua na ofisi pale karibu na Ubalozi wa Marekani.
Kampuni hiyo ili kujiunga ulipaswa kua na mtaji usiopungua milioni 23 kama kianzio. Watu waliweka hadi Bilioni 1.
Mwanzoni mwa uwekezaji, watu walikua wanalipwa faida bila shida ila baadae malipo yakaanza kusua sua, ukienda ofisini hakuna mtu hapo ndio baadhi ya wawekezaji wakakimbia polisi, muwekezaji mkuu akakamatwa na baadhi ya mali kuuzwa na kulipwa wawekezaji lakini idadi kubwa ya wawekezaji wameliwa pesa zao na mmiliki wa makampuni hajulikani alipo
Sijui ni kwa nini watanzania hawabadiliki.
Kabla sijamalizia naomba nitoe ushauri. Kama unataka kuwekeza, nenda kwa kampuni zilizosajiliwa kwenye masoko ya uwekezaji. Pamoja na hilo ujitidhishe vitu vifuatavyo.
1. Iwe ni kampuni iliyosajiliwa na mamlaka zinasosimalia uwekezaji kama Capital Market and Security Authority.
2. Kampuni iwe inaandaa hesabu za wazi(public accounts) na zinandaliwa na mhasibu aliesajiliwa NBAA na pia zinakaguliwa na kampuni iliyosajiliwa NBAA kama kampuni ya ukaguzi. Pia hapa ujiridhishe na uwezo wa kampuni ya ukaguzi, haiwezekani kampuni ina mtaji wa Bilioni 20 ikaguliwe na kampuni ndogo ya ukaguzi. Hapo uwe na mashaka. Taarifa za wahasibu wlaiosajiliwa NBAA na wakaguzi zinapatikana kwenye website ya NBAA.
3. Kampuni iwe inalipa kodi TRA kwa kutumia hesabu ama vitabu vya hesabu. Kampuni yoyote inayofanya biashara halali na inapata faida lazima iwe inaandaa hesabu na zinapelekwa TRA kwa ajili ya makadirio ya kodi.
4. Kampuni inajaza marejeo ya Brela(File Annual returns). Kampuni yoyote inayofanya biashara halali lazima ijaze taarifa muhimu Brela kila mwaka. Taarifa hizi ni muhimu kwa sababu zinakupa picha ya kujua wamiliki, biashara wanayofanya, mabadiliko yoyote ya wamiliki ama wakurugenzi nk. Annual returns za Brela ni tofauti usajili wa Brela. So annual ni bora zaidi.
Hesabu zilizokaguliwa zinakupa picha ya wanachama wangapi, pesa iliyoko bank ni kiasi gani, faida iliyopatikana ni kiasi gani nk.
Uwekezaji usitumie rafiki ama ndugu yako akushauri, tafta wataalamu wa masuala ya fedha wakushauri. Leo hii unaweza kujifunza masuala muhimu ya fedha bila hata kua mhasibu. Unaingia YouTube, google, chat GPT unauliza kwenye vitabu vya hesabu niangalie wapi muhimu na kila unachokiangalia kinakwambia nini utapata majibu.
Usiweke hela yako mahala kwa kutumia ushawishi ama ushauri wa marafiki. Utapoteza pesa na utapata hasara.
Wadau mnaweza kuongeza nini watu waangalie wasijikute wanapigwa na upatu.