Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
KATIBA NI NINI NA VIPI INAVYOTAKIWA IWE
Katiba ..ni maandiko maalum yanyoweka utaratibu wa namna gani utawala, bunge na mahakama
zitafanya shughuli zao. Katiba vile vile inaweka namna haki za wananchi zitavyoshughulikiwa na Serikali.
(Tizama Kitabu cha B.R.Atre Legislative Drafting 2nd Edn, pg 200)
Kwa maana fupi kabisa, Katiba ni makubaliano maalum ya kanuni, utaratibu na mazoea ya chombo fulani yaliyowekwa pamoja na ambayo yanatoa mfumo, muundo na kazi ya chombo hicho. Pale tunapozungumia katiba ya nchi
Hii inaonesha wazi kuwa Katiba ndio msingi mkuu wa sheria zote, na hakuna chombo kinachoweza kuichezea kwa kuibadilisha ovyo ovyo ila kwa utaratbu maalum uliowekwa. Na ndio maana huko Marekani kesi muhimu ya Marbury vs. Madison ikaamuliwa ya kuwa:
..kwa sababu Katiba ndio sheria kuu ya nchi (kama ilivyo ibara ya VI ya Katiba ya Marekani) na kwa sababu ni mamlaka ya Mahkama kutekelza sheria hizo kwa vitendo, inamaanisha kwamba sheria nyengine za nchi,na hata sheria zinazopitishwa na Bunge (congress) zinaopotofautinana na kifungu chochote cha Katiba, basi sheria hizo zinatoa nafasi kwa Katiba, na sheria hizo lazima ziainishwe na Mahkama zetu kuwa ni batili.
Katiba pia inatoa mfumo au utaratibu wa kisheria kwa nchi husika juu ya muundao wa Serikali yake, vyombo vyake vya kisiasa na mahusiano baina ya wananchi na serikali na pia mahusiano baina ya wananchi wenyewe.Katiba ya nchi vile vile ni kama mkataba ambapo wananchi wenyewe na taifa hilo wamekubali kuwa mkataba huo utumike katika kuwaongoza wao na Serikali yao, pamoja na kukubaliana ni namna gani vyombo vya dola vitafanya kazi. Katiba ni lazima iwepo katika nchi ili kukinga matatizo yanayoweza kujitokeza ikiwa kila mwananchi atafuata utaratibu wake, au kila mkondo wa Serikali utafanya wanachokitaka. Katiba ni kanuni maalum ambazo zina lengo la kuiweka jamii pamoja, jamii ambayo itaishi katika mazingira ya amani na utulivu bila ya kuwa na migongano kwa lengo la kuleta maendeleo katika nchi hiyo.
VIPI KATIBA INATAKIWA IWE ?
Aliyekuwa Jaji Mkuu wa Marekani Sir. John Marshall, alisema katika kesi maarufu ya Mc. Culloch Vs. Maryland 4 wheat 316 (US 1819) kwamba Katiba yao ni Katiba ambayo:
Ina lengo la kushi miaka kadhaa ijayo, na kwa hivyo iwe inaweza kuhimili misukosuko kadhaa ya binaadamu.
Lakini ili nisipotoshe maana halisi aliyoielezea Bw. Johm Marshall, yeye alisema kwa lugha ya Kiingereza kuwa:
Our constitution .is a Constitution intended to endure for ages to come, and consequently to be adapted to the various crises of human affair
Sasa basi Katiba yetu ya Tanzania na kwa maana pana Katiba ya nchi nyengine yoyote, ambayo ni sheria mama ya nchi,lazima ilenge huko alikokuona Bw. Jonh Marshall. Inatakiwa iwe inakidhi haja ya mabadiliko ya nchi kisiasa na kiuchumi. Inatakiwa iwe ni nyumbufu (flexible) kukubaliana na ukuwaji wa mabadiliko kadhaa ya taifa husika, na wakati huo huo misingi yake mikuu iwe bado inaongoza taifa hilo na watu wake bila ya kutetereka.
Katiba nzuri ya nchi, na ambavyo ndivyo inavyotakiwa iwe, ni kama ile aliyoielezea Jaji Sower katika kesi ya Tuffuor v. A. of Ghana (1980) A.G. 637, 674 kwamba Katiba ya nchi ni chombo ambacho kinakidhi matakwa ya wananchi na kwamba vile vile inaonesha historia yao. Hivyo basi katiba yoyote ile nilazima itizamwE kuwa ni dira, na ni:
..alama muhimu (land mark) katika kuwaoneshea watu njia ya maendeleo. Ndani yake mna tama na malengo (hopeS and aspirations) kwa kupata maisha mazuri. Katiba ina misingi yake ya sheria (its letter of the law) na ina malengo yake (its spirit). Katiba ndio kichwa cha mikondo mitatu ya utawala ambapo kila mkondo unafanya wajibu wake ..na uwezo wao unatokana na Katiba hiyo, Katiba inaelezea pia namna ya kuibadilisha ..kwa maana hiyo lugha inayotumika katika Katiba ni lazima iwe ina fikiriwa kama ni kitu kinachoishi (living organism) ambacho kinakua na kuendelea ..(capable of growth and development).
Katiba ..ni maandiko maalum yanyoweka utaratibu wa namna gani utawala, bunge na mahakama
zitafanya shughuli zao. Katiba vile vile inaweka namna haki za wananchi zitavyoshughulikiwa na Serikali.
(Tizama Kitabu cha B.R.Atre Legislative Drafting 2nd Edn, pg 200)
Kwa maana fupi kabisa, Katiba ni makubaliano maalum ya kanuni, utaratibu na mazoea ya chombo fulani yaliyowekwa pamoja na ambayo yanatoa mfumo, muundo na kazi ya chombo hicho. Pale tunapozungumia katiba ya nchi
Hii inaonesha wazi kuwa Katiba ndio msingi mkuu wa sheria zote, na hakuna chombo kinachoweza kuichezea kwa kuibadilisha ovyo ovyo ila kwa utaratbu maalum uliowekwa. Na ndio maana huko Marekani kesi muhimu ya Marbury vs. Madison ikaamuliwa ya kuwa:
..kwa sababu Katiba ndio sheria kuu ya nchi (kama ilivyo ibara ya VI ya Katiba ya Marekani) na kwa sababu ni mamlaka ya Mahkama kutekelza sheria hizo kwa vitendo, inamaanisha kwamba sheria nyengine za nchi,na hata sheria zinazopitishwa na Bunge (congress) zinaopotofautinana na kifungu chochote cha Katiba, basi sheria hizo zinatoa nafasi kwa Katiba, na sheria hizo lazima ziainishwe na Mahkama zetu kuwa ni batili.
Katiba pia inatoa mfumo au utaratibu wa kisheria kwa nchi husika juu ya muundao wa Serikali yake, vyombo vyake vya kisiasa na mahusiano baina ya wananchi na serikali na pia mahusiano baina ya wananchi wenyewe.Katiba ya nchi vile vile ni kama mkataba ambapo wananchi wenyewe na taifa hilo wamekubali kuwa mkataba huo utumike katika kuwaongoza wao na Serikali yao, pamoja na kukubaliana ni namna gani vyombo vya dola vitafanya kazi. Katiba ni lazima iwepo katika nchi ili kukinga matatizo yanayoweza kujitokeza ikiwa kila mwananchi atafuata utaratibu wake, au kila mkondo wa Serikali utafanya wanachokitaka. Katiba ni kanuni maalum ambazo zina lengo la kuiweka jamii pamoja, jamii ambayo itaishi katika mazingira ya amani na utulivu bila ya kuwa na migongano kwa lengo la kuleta maendeleo katika nchi hiyo.
VIPI KATIBA INATAKIWA IWE ?
Aliyekuwa Jaji Mkuu wa Marekani Sir. John Marshall, alisema katika kesi maarufu ya Mc. Culloch Vs. Maryland 4 wheat 316 (US 1819) kwamba Katiba yao ni Katiba ambayo:
Ina lengo la kushi miaka kadhaa ijayo, na kwa hivyo iwe inaweza kuhimili misukosuko kadhaa ya binaadamu.
Lakini ili nisipotoshe maana halisi aliyoielezea Bw. Johm Marshall, yeye alisema kwa lugha ya Kiingereza kuwa:
Our constitution .is a Constitution intended to endure for ages to come, and consequently to be adapted to the various crises of human affair
Sasa basi Katiba yetu ya Tanzania na kwa maana pana Katiba ya nchi nyengine yoyote, ambayo ni sheria mama ya nchi,lazima ilenge huko alikokuona Bw. Jonh Marshall. Inatakiwa iwe inakidhi haja ya mabadiliko ya nchi kisiasa na kiuchumi. Inatakiwa iwe ni nyumbufu (flexible) kukubaliana na ukuwaji wa mabadiliko kadhaa ya taifa husika, na wakati huo huo misingi yake mikuu iwe bado inaongoza taifa hilo na watu wake bila ya kutetereka.
Katiba nzuri ya nchi, na ambavyo ndivyo inavyotakiwa iwe, ni kama ile aliyoielezea Jaji Sower katika kesi ya Tuffuor v. A. of Ghana (1980) A.G. 637, 674 kwamba Katiba ya nchi ni chombo ambacho kinakidhi matakwa ya wananchi na kwamba vile vile inaonesha historia yao. Hivyo basi katiba yoyote ile nilazima itizamwE kuwa ni dira, na ni:
..alama muhimu (land mark) katika kuwaoneshea watu njia ya maendeleo. Ndani yake mna tama na malengo (hopeS and aspirations) kwa kupata maisha mazuri. Katiba ina misingi yake ya sheria (its letter of the law) na ina malengo yake (its spirit). Katiba ndio kichwa cha mikondo mitatu ya utawala ambapo kila mkondo unafanya wajibu wake ..na uwezo wao unatokana na Katiba hiyo, Katiba inaelezea pia namna ya kuibadilisha ..kwa maana hiyo lugha inayotumika katika Katiba ni lazima iwe ina fikiriwa kama ni kitu kinachoishi (living organism) ambacho kinakua na kuendelea ..(capable of growth and development).