Mto Songwe
JF-Expert Member
- Jul 17, 2023
- 6,120
- 12,548
Maswali yetu na tafakuri yetu yaweza kuwa msaada kupata mwanga kuhusu vifo vya ndugu zetu wawili hawa wa Kitanzania.
Tuanze na taarifa ya mwanzo ya mkasa huu wa hawa ndugu zetu hii hapa⤵️
Na Yusuf Jumah
BBC Swahili
CHANZO CHA PICHA, ISRAEL MFA
Serikali ya Israel imethibitisha utambulisho wa watu wawili kutoka Tanzania wanaoaminika kushikiliwa na Hamas tangu shambulio la Oktoba 7 dhidi ya jamii za kusini mwa Israel, karibu na mpaka na Gaza.
Joshua Loitu Mollel na Clemence Felix Mtenga walikuwa nchini Israel kama sehemu ya programu ya mafunzo ya kilimo, kulingana na taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel.
"Walitekwa nyara na magaidi wa Hamas na wanazuiliwa mateka huko Gaza," ujumbe huo ulisema. "Tafadhali ungana nasi kuwaombea warudi salama na mara moja."
Mollel na Mtenga walikuwa sehemu ya kundi la wanafunzi waliokuwa wakiishi Kibbutz Nahal Oz. Walikuwa wametoweka tangu mashambulizi hayo, lakini Israel ilikuwa bado haijathibitisha utambulisho wao au kuripoti kilichowapata.
Tanzania ilisema Alhamisi kuwa inafahamu kuhusu wanafunzi wawili waliopotea ambao ni sehemu ya kundi la Watanzania 260 nchini Israel, lakini bado haijathibitisha walipo. Watanzania tisa waliokuwa Israel walirejea nyumbani Oktoba 18.
BBC hapo awali ilizungumza na familia ya mmoja wao, Joshua Mollel, ambaye ni mmoja wa mwanafunzi hao lakini ikasema haikuwa imewasiliana naye tangu wakati wa shambulio hilo.
Habari hizo zinakuja huku kukiwa na majadiliano ya pendekezo la Hamas la kuwaachilia mateka.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amirabdollahian, alisema wiki iliyopita kwamba Hamas iko tayari kuwaachilia mateka lakini "ulimwengu unapaswa kuunga mkono kuachiliwa kwa Wapalestina 6,000" ambao wamekuwa wakishikiliwa katika jela za Israel.
"Viongozi wa vuguvugu la ukombozi la Hamas wametangaza kuwa tayari kuwaachilia wafungwa wasiokuwa wanajeshi na Iran, Uturuki na Qatar ziko tayari kutekeleza jukumu lao katika juhudi hii muhimu," alisema mwanadiplomasia huyo wa Iran.
Ubalozi wa Israel mjini Pretoria awali uliripoti kuwa raia wawili wa Afrika Kusini, raia wa Eritrea na raia mmoja wa Sudan pia walikuwa miongoni mwa waliofariki au kutoweka.
Tuje na taarifa ya mwisho ya hitimisho hii hapa⤵️
Gari la Shirika la Msalaba Mwekundu likiwa limewabeba mateka wa Israel wenye asili ya Russia Novemba 26,2023. Picha na Belal Al SABBAGH / AFPTV / AFP
Ona maoni
Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania siku ya Alhamisi imethibitisha kifo cha mmoja wa Watanzania ambaye “aliuawa mara baada ya kukamatwa na Hamas” wakati wa mashambulizi ya Oktoba 7, huko Kusini mwa Israel.
Siku ya Alhamisi Waziri wa Mambo ya Nje, Januari Makamba amesema mamlaka “imearifiwa na serikali ya Israel kuwa Joshua Mollel, mwanafunzi wa Kitanzania aliyekuwa akisoma nchini Israel, ambaye alipoteza mawasiliano tangu Oktoba 7, 2023…aliuawa mara baada ya kukamatwa na Hamas.”
Waziri Makamba alisema kupitia mtandao wa X kuwa mamlaka ya Tanzania inafanya mipango kwa familia ya Mollel, akiwemo baba yake, kwenda Israel na afisa wa serikali “kukutana na balozi wetu na maafisa wa Israel na kupata taarifa zaidi” kuhusiana na kifo chake.
Serikali ya Israel iliwataja wanafunzi wawili kutoka Tanzania waliokuwa wakisoma nchini Isreal -- Clemence Felix Mtenga mwenye umri wa miaka 22 na Joshua Loitu Mollel mwenye umri wa miaka 21.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania ilitangaza kifo cha Mtenga mwezi uliopita, bila ya kutoa maelezo kuhusu mauaji yake
Wanafunzi hao wawili ni miongoni mwa vijana wa Kitanzania wapatao 260 ambao walikwenda Israel kwa mafunzo ya kazi kwa vitendo katika kilimo cha kisasa chini ya mpango wa ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la AFP
Hizi taarifa zinazalisha maswali mengi sana yenye kuhitaji majawabu yalinyooka pasipo kuficha chochote wala kumuogopa yoyote wala imani yoyote ile.
1. Inabidi tuwekwe sawa Watanzania wote vijana wetu walitekwa oktoba 07 au waliuawa oktoba 07 ?
2. Kama walitekwa oktoba 07 miili yao imepatikana wapi na imepatwa na nani ?
3. Kama waliuawa oktoba saba kwa nini taarifa za mauaji yao hajikujumuhishwa na taarifa rasmi za wale wote waliouawa oktoba 07 ?
4. Kwa nini taarifa za vifo vya hawa Watanzania wawili zimekuja kimafungu mafungu moja mwezi Novemba nyengine mwezi Desemba ?
5. Kwa nini wizara ilikili haifahamu mahali walipo hawa Watanzania wawili halafu baadae inakuja kutujulisha mmoja kauawa Oktoba 07 mwengine taarifa yake mpaka leo imekuwa kimya ?
6. Serikali imefanya uchunguzi wowote wa kitabibu kuhusu vifo vya hawa Watanzania wawili ? Na uthibitisho wake ulikuwa upi ?
7. Kwanini Hamas mpaka sasa haijakili wala kupinga shutuma hizo za mauaji ya Watanzania hao wawili ?
Tuanze na taarifa ya mwanzo ya mkasa huu wa hawa ndugu zetu hii hapa⤵️
Israel yawatambua Watanzania wanaoshikiliwa mateka na Hamas
30 Oktoba 2023Na Yusuf Jumah
BBC Swahili
CHANZO CHA PICHA, ISRAEL MFA
Serikali ya Israel imethibitisha utambulisho wa watu wawili kutoka Tanzania wanaoaminika kushikiliwa na Hamas tangu shambulio la Oktoba 7 dhidi ya jamii za kusini mwa Israel, karibu na mpaka na Gaza.
Joshua Loitu Mollel na Clemence Felix Mtenga walikuwa nchini Israel kama sehemu ya programu ya mafunzo ya kilimo, kulingana na taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Israel.
"Walitekwa nyara na magaidi wa Hamas na wanazuiliwa mateka huko Gaza," ujumbe huo ulisema. "Tafadhali ungana nasi kuwaombea warudi salama na mara moja."
Mollel na Mtenga walikuwa sehemu ya kundi la wanafunzi waliokuwa wakiishi Kibbutz Nahal Oz. Walikuwa wametoweka tangu mashambulizi hayo, lakini Israel ilikuwa bado haijathibitisha utambulisho wao au kuripoti kilichowapata.
Tanzania ilisema Alhamisi kuwa inafahamu kuhusu wanafunzi wawili waliopotea ambao ni sehemu ya kundi la Watanzania 260 nchini Israel, lakini bado haijathibitisha walipo. Watanzania tisa waliokuwa Israel walirejea nyumbani Oktoba 18.
BBC hapo awali ilizungumza na familia ya mmoja wao, Joshua Mollel, ambaye ni mmoja wa mwanafunzi hao lakini ikasema haikuwa imewasiliana naye tangu wakati wa shambulio hilo.
Habari hizo zinakuja huku kukiwa na majadiliano ya pendekezo la Hamas la kuwaachilia mateka.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amirabdollahian, alisema wiki iliyopita kwamba Hamas iko tayari kuwaachilia mateka lakini "ulimwengu unapaswa kuunga mkono kuachiliwa kwa Wapalestina 6,000" ambao wamekuwa wakishikiliwa katika jela za Israel.
"Viongozi wa vuguvugu la ukombozi la Hamas wametangaza kuwa tayari kuwaachilia wafungwa wasiokuwa wanajeshi na Iran, Uturuki na Qatar ziko tayari kutekeleza jukumu lao katika juhudi hii muhimu," alisema mwanadiplomasia huyo wa Iran.
Ubalozi wa Israel mjini Pretoria awali uliripoti kuwa raia wawili wa Afrika Kusini, raia wa Eritrea na raia mmoja wa Sudan pia walikuwa miongoni mwa waliofariki au kutoweka.
Tuje na taarifa ya mwisho ya hitimisho hii hapa⤵️
Serikali ya Tanzania yathibitisha kifo cha raia wake aliyeuawa baada ya kukamatwa na Hamas
14 Desemba, 2023Gari la Shirika la Msalaba Mwekundu likiwa limewabeba mateka wa Israel wenye asili ya Russia Novemba 26,2023. Picha na Belal Al SABBAGH / AFPTV / AFP
Ona maoni
Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania siku ya Alhamisi imethibitisha kifo cha mmoja wa Watanzania ambaye “aliuawa mara baada ya kukamatwa na Hamas” wakati wa mashambulizi ya Oktoba 7, huko Kusini mwa Israel.
Siku ya Alhamisi Waziri wa Mambo ya Nje, Januari Makamba amesema mamlaka “imearifiwa na serikali ya Israel kuwa Joshua Mollel, mwanafunzi wa Kitanzania aliyekuwa akisoma nchini Israel, ambaye alipoteza mawasiliano tangu Oktoba 7, 2023…aliuawa mara baada ya kukamatwa na Hamas.”
Waziri Makamba alisema kupitia mtandao wa X kuwa mamlaka ya Tanzania inafanya mipango kwa familia ya Mollel, akiwemo baba yake, kwenda Israel na afisa wa serikali “kukutana na balozi wetu na maafisa wa Israel na kupata taarifa zaidi” kuhusiana na kifo chake.
Serikali ya Israel iliwataja wanafunzi wawili kutoka Tanzania waliokuwa wakisoma nchini Isreal -- Clemence Felix Mtenga mwenye umri wa miaka 22 na Joshua Loitu Mollel mwenye umri wa miaka 21.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Tanzania ilitangaza kifo cha Mtenga mwezi uliopita, bila ya kutoa maelezo kuhusu mauaji yake
Wanafunzi hao wawili ni miongoni mwa vijana wa Kitanzania wapatao 260 ambao walikwenda Israel kwa mafunzo ya kazi kwa vitendo katika kilimo cha kisasa chini ya mpango wa ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la AFP
Hizi taarifa zinazalisha maswali mengi sana yenye kuhitaji majawabu yalinyooka pasipo kuficha chochote wala kumuogopa yoyote wala imani yoyote ile.
1. Inabidi tuwekwe sawa Watanzania wote vijana wetu walitekwa oktoba 07 au waliuawa oktoba 07 ?
2. Kama walitekwa oktoba 07 miili yao imepatikana wapi na imepatwa na nani ?
3. Kama waliuawa oktoba saba kwa nini taarifa za mauaji yao hajikujumuhishwa na taarifa rasmi za wale wote waliouawa oktoba 07 ?
4. Kwa nini taarifa za vifo vya hawa Watanzania wawili zimekuja kimafungu mafungu moja mwezi Novemba nyengine mwezi Desemba ?
5. Kwa nini wizara ilikili haifahamu mahali walipo hawa Watanzania wawili halafu baadae inakuja kutujulisha mmoja kauawa Oktoba 07 mwengine taarifa yake mpaka leo imekuwa kimya ?
6. Serikali imefanya uchunguzi wowote wa kitabibu kuhusu vifo vya hawa Watanzania wawili ? Na uthibitisho wake ulikuwa upi ?
7. Kwanini Hamas mpaka sasa haijakili wala kupinga shutuma hizo za mauaji ya Watanzania hao wawili ?