Wasomi wa CCM

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Nilikutana na kijana mmoja wa kwetu Pemba ambae siku nyingi sijamuona hapa Dar. Nikamuuliza vipi salama na mabomu ya Mbagala na mbona sijakuona siku nyingi kwetu Pemba ? Alinijibu, ya Mbagala salama lakini hayo mabomu ya Pemba ndio yalionikimbiza na sina hamu ya kurudi kwa miaka hii. Ndipo akanipa mkasa huu hapa chini:

Kuna wakati fulani wa Uchaguzi, kulizuka kile kilichoitwa uripuaji wa mabomu Pemba. Yeye alikuwa ni mmoja katika vijana waliokamatwa Pemba akihusishwa na uripuaji huo.

Akapelekwa katika kikao kimoja wapo cha dola kuhojiwa. Wakati anahojiwa, Mkuu wa Mkoa, akamwambia Kamanda wa Polisi, "Huyu niachie miyee"

Mkuu wa Mkoa akamuuliza yule kijana, "Wewe umesoma skuli?" Jibu "Ndio" Gavana akauliza tena "Mpaka darasa la ngapi?" Jibu, "Form IV" Gavana akaendelea, " Umesoma masomo gani?". Jibu likawa, "Masomo yote" Akaendelea Mkuu, " Hapana, nataka unitajie hassa"

Kijana akaanza kutaja, " English, Kiswahili, Gegraphy ....n.k. Alipofika Physics, Mkuu wa Mkoa akamwambia Kamanda " Huyu aweza". :D

Ndipo kijana huyo akenda kuchezea mkong'oto uliomhamisha kwao mpaka leo.

Wana JF, hio ndio evidence ambayo ili m-convict huyo kijana, na yote kutokana na wasomi wa CCM ,ambao eti mtu kasoma somo la fizikia basi atakuwa na uwezo wa kutengeneza na kupasua mabomu.

Na huo ndio mkasa niliotaka na nyinyi muusikie!!!
 
Nilikutana na kijana mmoja wa kwetu Pemba ambae siku nyingi sijamuona hapa Dar. Nikamuuliza vipi salama na mabomu ya Mbagala na mbona sijakuona siku nyingi kwetu Pemba ? Alinijibu, ya Mbagala salama lakini hayo mabomu ya Pemba ndio yalionikimbiza na sina hamu ya kurudi kwa miaka hii. Ndipo akanipa mkasa huu hapa chini:

Kuna wakati fulani wa Uchaguzi, kulizuka kile kilichoitwa uripuaji wa mabomu Pemba. Yeye alikuwa ni mmoja katika vijana waliokamatwa Pemba akihusishwa na uripuaji huo.

Akapelekwa katika kikao kimoja wapo cha dola kuhojiwa. Wakati anahojiwa, Mkuu wa Mkoa, akamwambia Kamanda wa Polisi, "Huyu niachie miyee"

Mkuu wa Mkoa akamuuliza yule kijana, "Wewe umesoma skuli?" Jibu "Ndio" Gavana akauliza tena "Mpaka darasa la ngapi?" Jibu, "Form IV" Gavana akaendelea, " Umesoma masomo gani?". Jibu likawa, "Masomo yote" Akaendelea Mkuu, " Hapana, nataka unitajie hassa"

Kijana akaanza kutaja, " English, Kiswahili, Gegraphy ....n.k. Alipofika Physics, Mkuu wa Mkoa akamwambia Kamanda " Huyu aweza". :D

Ndipo kijana huyo akenda kuchezea mkong'oto uliomhamisha kwao mpaka leo.

Wana JF, hio ndio evidence ambayo ili m-convict huyo kijana, na yote kutokana na wasomi wa CCM ,ambao eti mtu kasoma somo la fizikia basi atakuwa na uwezo wa kutengeneza na kupasua mabomu.

Na huo ndio mkasa niliotaka na nyinyi muusikie!!!

Asante na pole kwa huyo msomi wa fizikia.

Mkuu, maswala ya Pemba ni doa kubwa ambalo halita kaa lifute juu ya uso wa Tanzania kwa siku za hivi karibuni. Hata kule You Tube kuna ile picha askari walivo kuwa wana wapiga na kuwanyanyasa wana CUFkwa kuwagalagaza kwenye tope, haitakaa initoke kichwani mwangu, na mbaya zaidi, it there for the whole world to see! Afu eti kisiwa cha Amani?
 
Mwiba,
Vipi hakukupa stori ya kupaka vinyesi katika skuli, au ile ya kwenda haja kubwa visimani?
 
Jee kwani hao wa ibara ya vinyesi maskuli na uchafuzi wa visima unafikiri si wasomi? Wanaelewa fika mambo ya Biology, na Chemistry.
 
Mwiba,
Vipi hakukupa stori ya kupaka vinyesi katika skuli, au ile ya kwenda haja kubwa visimani?

Kibunango we wacha tu ,ila wapemba waliwaperemba na kuwajua mmoja baada ya mwingine ,hii ndio sifa iliyoko Pemba ,hebu fikiria wameweza kuwangamua wote waliofyatua risasi na kuua na mmoja walimnadi mwizi pale Unguja na kumtoa roho kwa kumpiga kipigo cha paka mwizi mwengine amehamishiwa bara.

Ila kwa taarifa tu hayo yaliopita huko Unguja na Pemba ujue sasa ndio yanaitambalia Tanganyika na muda si mrefu utaanza kusikia vishindo vya kushindwa na kukataliwa na wananchi. CCM wanapoanza visa vya aina hii ujue wameshang'amua kuwa hawapendwi tena ,huko Tanganyika watafanya yote watachoma moto nyumba ,watatia vinyesi na mengi zaidi ambayo wanayajua wao ,jitayarisheni na vituko vya wafuasi wa Sultani CCM.
 
Back
Top Bottom