Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wadau:
Kila mara huwa najiuliza: Kwa nini ile sheria ya kuwaweka watu kizuizini bila ya kufunguliwa mashitaka (Preventive Detention Act) bado ipo hadi leo hii?
Hiyo sheria kandamizi haijaondolewa na tangu ujio wa siasa za vyama vingi haijawahi kutumiwa na kiongozi yoyote wa nchi. Kwa maneno mengine sheria hiyo ipo kisheria lakini siyo halali.
Hivi hawa viongozi wa serikali ya CCM wa sasa hivi hawaoni umuhimu wa kuiondoa? Hawaoni kwamba inaweza kuwarudia wao wenyewe.
Nasema hivi kwa sababu hatujui Mwenyezi Mungu ameipangia Tanzania yetu hii kitu gani – katika miaka ijayo huwezi kujua katupangia nini.
Siombei machafuko, lakini kwa madudu viongozi wa CCM wanayowafanyia Watanzania, wanaweza kujikuta wametupwa nje ya uongozi-kama ilivyotokea katika nchi nyingi tu Barani humu, na sikioni kitu chochote kinachoweza kuniridhisha kuwa nchi hii ni ya kipekee yaani unique.
Madudu yanayofanywa na viongozi wetu ni yaleyale waliyokuwa wakiyafanya hao wengine kwa wananchi wao na kujikuta wako nje.
Sasa wapinzani wakishika nchi wanaweza kupata urahisi mkubwa wa kuwashughulikia mafisadi hawa wa CCM walioko katika uongozi sasa kwa sababu sheria hiyo haitahitaji ushahidi thabiti wa ufisadi hao. Serikali mpya inaweza kuwasweka ndani wakaozea huko, na ikawa haijavunja sheria wala Katiba.
Ikitokea hivyo, hivi wafuasi wa CCM (yaani wapinzani) kweli watapata nguvu ya kuilalamikia serikali hiyo mpya?
CCM lazima itumie akili. Kuna kila dalili sheria hii inaweza kuwarudia wao.
Nawasilisha.
Kila mara huwa najiuliza: Kwa nini ile sheria ya kuwaweka watu kizuizini bila ya kufunguliwa mashitaka (Preventive Detention Act) bado ipo hadi leo hii?
Hiyo sheria kandamizi haijaondolewa na tangu ujio wa siasa za vyama vingi haijawahi kutumiwa na kiongozi yoyote wa nchi. Kwa maneno mengine sheria hiyo ipo kisheria lakini siyo halali.
Hivi hawa viongozi wa serikali ya CCM wa sasa hivi hawaoni umuhimu wa kuiondoa? Hawaoni kwamba inaweza kuwarudia wao wenyewe.
Nasema hivi kwa sababu hatujui Mwenyezi Mungu ameipangia Tanzania yetu hii kitu gani – katika miaka ijayo huwezi kujua katupangia nini.
Siombei machafuko, lakini kwa madudu viongozi wa CCM wanayowafanyia Watanzania, wanaweza kujikuta wametupwa nje ya uongozi-kama ilivyotokea katika nchi nyingi tu Barani humu, na sikioni kitu chochote kinachoweza kuniridhisha kuwa nchi hii ni ya kipekee yaani unique.
Madudu yanayofanywa na viongozi wetu ni yaleyale waliyokuwa wakiyafanya hao wengine kwa wananchi wao na kujikuta wako nje.
Sasa wapinzani wakishika nchi wanaweza kupata urahisi mkubwa wa kuwashughulikia mafisadi hawa wa CCM walioko katika uongozi sasa kwa sababu sheria hiyo haitahitaji ushahidi thabiti wa ufisadi hao. Serikali mpya inaweza kuwasweka ndani wakaozea huko, na ikawa haijavunja sheria wala Katiba.
Ikitokea hivyo, hivi wafuasi wa CCM (yaani wapinzani) kweli watapata nguvu ya kuilalamikia serikali hiyo mpya?
CCM lazima itumie akili. Kuna kila dalili sheria hii inaweza kuwarudia wao.
Nawasilisha.