Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 975
- 47
Warioba abashiri mafisadi wa EPA kutikisa nchi
Tanzania kama Taifa lenye dola kamili (sovereign) litatikisika na kudhalilika mno machoni pa wananchi wake na katika jumuiya ya kimataifa, iwapo matajiri waliogushi na kuiba fedha za katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) hawatafikishwa mahakamani.
Onyo hilo limetolewa jana na waziri Mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba alipofanya mahojiano maalum na gazeti hili, ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Jaji Warioba alisema kimsingi hatua za awali zilizochukuliwa na serikali kukabiliana na mafisadi zina mwelekeo mzuri.
``Tutakuwa tumefanya makosa makubwa na ya kihistoria, kutowafikisha wezi kortini eti kwa sababu ni matajiri. Kosa hili litakuwa limeitikisa Tanzania kama nchi sovereign (Dola).
Watu wakijua kwamba katika nchi yao matajiri hawafikishwi mbele ya sheria (Mahakamani) hawatakuwa na imani na serikali yao, hawataiheshimu serikali,`` alisema na kuongeza:
``Kama matajiri wasipofikishwa mahakamani eti kwa ajili ya fedha walizo nazo, basi dola itakuwa imeweka rehani uwezo, madaraka na mamlaka yake kwa mafisadi.``
Sakata la EPA liliibuka katika hesabu wa BoT za mwaka 2005/06 ambapo iligundilika kwamba kiasi cha Sh bilioni 133 zilichotwa na makampuni fisadi 22.
Alisema hata kauli iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete juu ya umuhimu wa kurejeshwa kwa fedha hizo na wahusika kufikishwa mbele ya sheria, imetoa mwanga mzuri zaidi juu ya jambo hilo.
Hata hivyo Mwanasiasa huyo alionya kwamba kurudisha pesa hizo pekee, hakutoshi na wala si njia ya kumaliza kashfa hiyo ambayo imewaudhi wananchi kwa kiasi kikubwa.
Vilevile alisema kukaa kimya kutayafanya mataifa ya nje, na hata wahisani kuishangaa serikali na kuibeza.
``Lazima tujue na kuzingatia kwamba suala la EPA lilikuwa si lelemama, lile lilikuwa jambo kubwa, liliwahusisha watu wakubwa, na fedha zilizoibwa zilikuwa nyingi na mbinu zilizotumika zilikuwa za hali ya juu, kwa hiyo busara za hali ya juu ilibidi zitumike, na bado busara hizo zinahitajika japokuwa kilele cha yote ni mahakamani, hakuna uchochoro wa kukwepa korti,`` alisema.
Hata hivyo alisema baada ya kusikiliza mlolongo wa tatizo hilo, ni wazi kwamba waliofanikiwa kuiba fedha za EPA walifanya hivyo baada ya kughushi.
``Na kughushi kwenyewe ni kosa la jinai, achilia mbali wizi walioufanya,`` alisema.
Mbali na hivyo, Jaji Warioba alisema Watanzania wanayo haki ya kuwajua kwa majina watuhumiwa wa fedha za EPA na kujua kwa undani walitumia mbinu gani na kwa wakati upi, kutekeleza uovu huo.
Alisema hekima za serikali, ambazo zimesaidia kurejeshwa kwa baadhi ya fedha, zinapaswa kupongezwa, lakini makosa kama hayo yanaweza kujitokeza tena siku za usoni, iwapo kosa hilo halitawekwa bayana.
Jaji Warioba alisema kwa vile wahusika hao wamekubali kurejesha fedha hizo, na wengine wamepewa muda wa kuendelea kurudisha, ni wazi kwamba wamekiri kuhusika na kosa pamoja na kuiba.
``Hawa watu tunataka wajulikane na wakamatwe, itakuwa vigumu kubaini mbinu walizotumia kuiba na waliowasaidia, nje ya mahakama. Tukiacha hivi tutakuwa tumekalia tatizo ambalo linaweza kututafuna kama kansa siku zijazo,`` alisema.
Alisema kwa vyovyote waliochukua fedha hizo, wasingeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kiasi hicho, kama wasingepata masaada toka kwa maafisa wa juu.
Hadi sasa baada ya kugundulika wizi huo kufuatia ukaguzi wa kampuni ya Ernst & Young, serikali ilimfukuza kazi aliyekuwa gavana wa BoT, Marehemu Daudi Balali, na makapuni husika yametakiwa kurejesha fedha hizo.
Mwisho wa kurejesha fedha ni Oktoba 31, mwaka huu kabla ya Novemba mosi hatua za kisheria kuanza kuchukuliwa.
* SOURCE: Nipashe
Tanzania kama Taifa lenye dola kamili (sovereign) litatikisika na kudhalilika mno machoni pa wananchi wake na katika jumuiya ya kimataifa, iwapo matajiri waliogushi na kuiba fedha za katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) hawatafikishwa mahakamani.
Onyo hilo limetolewa jana na waziri Mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba alipofanya mahojiano maalum na gazeti hili, ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Jaji Warioba alisema kimsingi hatua za awali zilizochukuliwa na serikali kukabiliana na mafisadi zina mwelekeo mzuri.
``Tutakuwa tumefanya makosa makubwa na ya kihistoria, kutowafikisha wezi kortini eti kwa sababu ni matajiri. Kosa hili litakuwa limeitikisa Tanzania kama nchi sovereign (Dola).
Watu wakijua kwamba katika nchi yao matajiri hawafikishwi mbele ya sheria (Mahakamani) hawatakuwa na imani na serikali yao, hawataiheshimu serikali,`` alisema na kuongeza:
``Kama matajiri wasipofikishwa mahakamani eti kwa ajili ya fedha walizo nazo, basi dola itakuwa imeweka rehani uwezo, madaraka na mamlaka yake kwa mafisadi.``
Sakata la EPA liliibuka katika hesabu wa BoT za mwaka 2005/06 ambapo iligundilika kwamba kiasi cha Sh bilioni 133 zilichotwa na makampuni fisadi 22.
Alisema hata kauli iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete juu ya umuhimu wa kurejeshwa kwa fedha hizo na wahusika kufikishwa mbele ya sheria, imetoa mwanga mzuri zaidi juu ya jambo hilo.
Hata hivyo Mwanasiasa huyo alionya kwamba kurudisha pesa hizo pekee, hakutoshi na wala si njia ya kumaliza kashfa hiyo ambayo imewaudhi wananchi kwa kiasi kikubwa.
Vilevile alisema kukaa kimya kutayafanya mataifa ya nje, na hata wahisani kuishangaa serikali na kuibeza.
``Lazima tujue na kuzingatia kwamba suala la EPA lilikuwa si lelemama, lile lilikuwa jambo kubwa, liliwahusisha watu wakubwa, na fedha zilizoibwa zilikuwa nyingi na mbinu zilizotumika zilikuwa za hali ya juu, kwa hiyo busara za hali ya juu ilibidi zitumike, na bado busara hizo zinahitajika japokuwa kilele cha yote ni mahakamani, hakuna uchochoro wa kukwepa korti,`` alisema.
Hata hivyo alisema baada ya kusikiliza mlolongo wa tatizo hilo, ni wazi kwamba waliofanikiwa kuiba fedha za EPA walifanya hivyo baada ya kughushi.
``Na kughushi kwenyewe ni kosa la jinai, achilia mbali wizi walioufanya,`` alisema.
Mbali na hivyo, Jaji Warioba alisema Watanzania wanayo haki ya kuwajua kwa majina watuhumiwa wa fedha za EPA na kujua kwa undani walitumia mbinu gani na kwa wakati upi, kutekeleza uovu huo.
Alisema hekima za serikali, ambazo zimesaidia kurejeshwa kwa baadhi ya fedha, zinapaswa kupongezwa, lakini makosa kama hayo yanaweza kujitokeza tena siku za usoni, iwapo kosa hilo halitawekwa bayana.
Jaji Warioba alisema kwa vile wahusika hao wamekubali kurejesha fedha hizo, na wengine wamepewa muda wa kuendelea kurudisha, ni wazi kwamba wamekiri kuhusika na kosa pamoja na kuiba.
``Hawa watu tunataka wajulikane na wakamatwe, itakuwa vigumu kubaini mbinu walizotumia kuiba na waliowasaidia, nje ya mahakama. Tukiacha hivi tutakuwa tumekalia tatizo ambalo linaweza kututafuna kama kansa siku zijazo,`` alisema.
Alisema kwa vyovyote waliochukua fedha hizo, wasingeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kiasi hicho, kama wasingepata masaada toka kwa maafisa wa juu.
Hadi sasa baada ya kugundulika wizi huo kufuatia ukaguzi wa kampuni ya Ernst & Young, serikali ilimfukuza kazi aliyekuwa gavana wa BoT, Marehemu Daudi Balali, na makapuni husika yametakiwa kurejesha fedha hizo.
Mwisho wa kurejesha fedha ni Oktoba 31, mwaka huu kabla ya Novemba mosi hatua za kisheria kuanza kuchukuliwa.
* SOURCE: Nipashe