Wapewe posho ya mazingira magumu (hardship allowance)

Black Walker

Senior Member
Oct 8, 2018
107
238
Naomba kuwasilisha hii hoja kwa Mheshimiwa Rais, waziri wa ajira na kazi, waziri wa utumishi na waziri wa Tamisemi.

Kuna hili kundi la wanandoa ambao ni wajiriwa wenu na wametanganishwa wako wanakaa mikoa au wilaya mbalimbali kiasi kwamba hawapati muda mzuri wa kuwa pamoja kama wenza muda mwingi wanapitia magumu ya kisaikolojia na matatizo mengine kwa familia zao.

Hali kama hii, na changamoto nyingine nyingi wanazopitia haipaswi kuchukuliwa kwa ukawaida bali izingatiwe kwamba na wao sasa wanastahili kupatiwa posho ya mazingira magumu kila mmoja.

Posho hii itakuwa inatolewa kwa hawa wenza kama kifuta jasho na itakoma pale ambapo mmojawapo atafanikiwa kuhamia kwa mwenzake.

Ikumbukwe kwamba tunaoana kwa lengo moja kubwa la kuwa pamoja na wenza wetu ili tuweze kutatua matatizo yetu tukiwa pamoja kitendo cha kutenganisha ni kama mmoja amerudishwa kwa wazazi wake.

Hali hii imepelekea leo ndoa nyingi kuvunjika na malezi ya watoto kuyumbayumba, mbali na hapo pia imepelekea maendeleo ya familia kusuasua kwani kumekuwepo na mgawanyo wa kipato na tena usiombe kwa wenye mishahara ya kawaida/chini.

Hali ya maumivu makali wanapitia watumishi wa kawaida lakini kwa maboss zetu kwa kutambua umuhimu wa ndoa, akihama anahama na mwenza wake.

Mbaya zaidi unakuta wanaweka vigezo eti ukitaka kuhama utafute mtu wa kubadilishana nae! Huu nao ni uonevu kama uonevu mwingine.

Fikiria maumivu ya ndoa kuvunjika.

Fikiria maumivu ya mzazi mmoja kukaa mbali na watoto wake kwa miaka, hisia za upendo wa watoto hudhihirika bayana pale wanapotuona na pale unapoaga ukienda kuwasalimia kipindi cha likizo. Ukiondoka vilio hutanda kama unaenda kufa na hawatakuona tena, yote haya ni maumivu.

Fikiria pia migogoro ya hapa na pale ambayo chanzo chake chaweza kuwa huo umbali.

Maumivu ya wenza kuleteana magonjwa n.k

HIVYO POSHO YA MAZINGIRA MAGUMU NI MUHIMU na endapo litatekelezwa waajiri wengi hawatakuwa wanakalia mafaili ya watu kwa muda mrefu bila kupitisha maombi yao maana watakuwa wanaogopa hizi gharama.

Karibu ni kwa michango.

Nawasilisha.

NUKIA KIBABE ISHI KIUNGWANA.
 
"inapelekea ndoa nyingi kuvunjika na malezi ya watoto kuyumba yumba"

kuna kizazi cha hovyo kinatengenezwa ila hawa viongozi wetu wanajifanya hawakioni,

huku wao wengi wakiwa wazazi wao wametoka kipindi kuna viongozi wenye utu waliokuwa wakipenda usawa wakiongozwa na nyerere!

Muda utasema kwa hichi kizazi cha nyoka kinavyozidi kukuwa bila maadili!
 
Nchi za wenzetu dawa yake ni UHAMISHO WA MASAA 24 kumfuata mwenza.

Tatizo Africa haki za binadamu ni jambo la ziada na sio lazima.

Unakuta vijana walikuwa wachumba Chuoni au wakati wa kusoma Mungu si Athumani wakapata kazi after school life then wanaamua kufunga ndoa ili wawe karibu kazi inaingilia kati inawatenganisha wanaanza stress life mpaka wanahisi kupata kazi imekuwa ni mkosi.

Uhamisho wa kumfuata Mwenza uwe uhamisho wa masaa 24
 
Na ku support mkuuu Hilo ndoa ya mbali inatesa sanaaa mume Yuko mbez beach mke Yuko katavi ndan ndan Mungu atusaidie long distance inatesa Sanaa ufunge safar Kumuona mwenza safar siku mbil haswa halmashauri za ndani
 
Naomba kuwasilisha hii hoja kwa Mheshimiwa Rais, waziri wa ajira na kazi, waziri wa utumishi na waziri wa Tamisemi.

Kuna hili kundi la wanandoa ambao ni wajiriwa wenu na wametanganishwa wako wanakaa mikoa au wilaya mbalimbali kiasi kwamba hawapati muda mzuri wa kuwa pamoja kama wenza muda mwingi wanapitia magumu ya kisaikolojia na matatizo mengine kwa familia zao.

Hali kama hii, na changamoto nyingine nyingi wanazopitia haipaswi kuchukuliwa kwa ukawaida bali izingatiwe kwamba na wao sasa wanastahili kupatiwa posho ya mazingira magumu kila mmoja.

Posho hii itakuwa inatolewa kwa hawa wenza kama kifuta jasho na itakoma pale ambapo mmojawapo atafanikiwa kuhamia kwa mwenzake.

Ikumbukwe kwamba tunaoana kwa lengo moja kubwa la kuwa pamoja na wenza wetu ili tuweze kutatua matatizo yetu tukiwa pamoja kitendo cha kutenganisha ni kama mmoja amerudishwa kwa wazazi wake.

Hali hii imepelekea leo ndoa nyingi kuvunjika na malezi ya watoto kuyumbayumba, mbali na hapo pia imepelekea maendeleo ya familia kusuasua kwani kumekuwepo na mgawanyo wa kipato na tena usiombe kwa wenye mishahara ya kawaida/chini.

Hali ya maumivu makali wanapitia watumishi wa kawaida lakini kwa maboss zetu kwa kutambua umuhimu wa ndoa, akihama anahama na mwenza wake.

Mbaya zaidi unakuta wanaweka vigezo eti ukitaka kuhama utafute mtu wa kubadilishana nae! Huu nao ni uonevu kama uonevu mwingine.

Fikiria maumivu ya ndoa kuvunjika.

Fikiria maumivu ya mzazi mmoja kukaa mbali na watoto wake kwa miaka, hisia za upendo wa watoto hudhihirika bayana pale wanapotuona na pale unapoaga ukienda kuwasalimia kipindi cha likizo. Ukiondoka vilio hutanda kama unaenda kufa na hawatakuona tena, yote haya ni maumivu.

Fikiria pia migogoro ya hapa na pale ambayo chanzo chake chaweza kuwa huo umbali.

Maumivu ya wenza kuleteana magonjwa n.k

HIVYO POSHO YA MAZINGIRA MAGUMU NI MUHIMU na endapo litatekelezwa waajiri wengi hawatakuwa wanakalia mafaili ya watu kwa muda mrefu bila kupitisha maombi yao maana watakuwa wanaogopa hizi gharama.

Karibu ni kwa michango.

Nawasilisha.

NUKIA KIBABE ISHI KIUNGWANA.
Hoja nzuri,

Mi pia nilitaka ku address issue hii, mi binafsi sihitaji hata hiyo posho, nikiangalia vile familia zinavyo farakana kisa wenza kutenganishwa inanisikitisha sana,

Serikali imeweka muda wa miaka 3 bila kuhama ktk kituo kimoja, hii ni mbaya sana kwa wenza, na familia kwa ujumla hasa kwenye malezi ya watoto.

Kuna wakati inabd watoto wabaki na baba labda kwakuwa mazingira ya kazi aliyopo mama siyo favourable ukilinganisha na aliyopo baba, na baba kwa malezi ya watoto hawapo vizuri.

Serikali ipunguze muda wa kuhama kwa watu wenye ndoa ili kuboresha malezi ya watoto na mahusiano ya wenza, pia kuwapunguzia gharama za maisha
 
Back
Top Bottom