Wapendwa na mimi nina langu jambo nahitaji kushauriwa

Kwa uhakika zaidi akapime ujauzito msitoe endapo atapatkana Na majibu yu mjamzito leeni mwana kulitaka ndie mwana kulipewa
 
Mzee umepiga siku ya 14 toka siku ya kwanza alipopata MP, imo hiyo kaka,bora upige changu kuliko mwanafunzi.
 
Ataelewa?

Maana jamaa atakuwa anaiwaza miaka 30 ya jela saa hizi!
Ataelewa tu alipomfanyia kitendo cha kumjaza mimba hakuwaza hata kama huyu n mwanafunzi bado? Ameshafanya ndio anauliza nn kitafata kibaya zaidi Kwa wote mwanafunzi Na mjamzito hawakuwaza magonjwa wamehofia mimba tu aisee
 
Habari za Leo ndg zangu wa damu;

Awali ya yote nipende kumshukru Mungu kwa pumzi zake ambazo hazilipiwi na anaendelea kunilinda hadi siku hii.

Swala langu ndg zangu ni dogo au kubwa kulingana na wew utakavyolichukulia, ila linahitaji usaidizi wa mawazo.

Imepita mwezi sasa tangu nikutane kimapenzi tena bila kinga na huyu binti ninayemleta kwenu kwa ajili ya kushauriana. Binti huyu kwa sasa yupo form six (jina la shule kapuni kwa usalama wake na wangu), na wakati nakutana naye kimapenz tarehe 30/06/2016 alikuwa kwa Mara ya kwanza kaingia kwenye MP yake tarehe 17/06/2016, basi baada ya hapo sikukutana naye tena na tayari wakawa wamefungua shule.

Wiki iliyopita alianza kunipigia simu akilalamika kuwa haoni siku zake (yaan baada ya siku 28 za kawaida za MP yake), basi nikawa nimemsihi nikisema yawezekana ni mabadiliko ya kawaida tu, wiki ya kwanza ikapita, basi wiki hii inayomalizikia Leo, amekuwa akilalamika kila siku, Mara anajisikia homa, Mara kizunguzungu, Mara anaishiwa nguvu, Mara kichefuchefu yaani mambo kibao.

Sasa hadi Leo hii binti huyu hajaona siku zake, na hali hiyo inaendelea, nimemtumia hela kidogo aende hospital ili tujue tatizo linaloendelea na akachukue na kipimo cha Mimba.

Jambo linalonitatiza hapa, je ni kweli kuwa ishara za mimba zinaanza katika early stages (hatua za swali) kama anavyofanya yeye au usanii wake tu?
Je ikigundulika kweli ana mimba, sheria inasemaje kuhusu students (wanafunzi) ambao ni above 18 (zaidi ya miaka 18, yeye ana 21 sasa kwa maana alirudia na yuko private )?
Je ikitokea hivyo, nimruhusu atoe mimba? (Kwa Imani yangu sitaki hata kusikia neno kutoa mimba, yaan atoe huku nikihusika, by the way mie sina hata mtoto) if that the case (kama ni hivyo) nifanyeje?

Tushauriane, matusi yako na unaweza kuyaporomosha bila hiana lakini hiki ndio kinanisibu wadau..

Ahsanteni na Jumapili njema
Nenda mahakamani au kituo chochote cha polisi uwaeleze tatizo lako watakusaidia
 
Back
Top Bottom