Waosha magari wanaiharibu Shekilango Rd

mfianchi

Platinum Member
Jul 1, 2009
11,855
8,253
Nakwera na tabia sugu ya jamaa wanaosha magari pembezoni mwa barabara ya Shekilango Sinza hasa kuanzia eneo la Mori hadi City Food restraurant mbele kidogo kwenye kituo cha mabasi pale kwa Remi,madhara ya uoshwaji huo wa magari ni
1.Bara bara inamong'onyoka na madimbwi ya maji yamefanya mashimo makubwa(kwenye sehemu ya waendayo kwa miguu) kiasi kwamba wapita kwa miguu sasa hupita kwenye barabara kuu yenye magari ambapo ni hatari kwa usalama.
2.Magari yaoshwayo huziba njia ya wapita kwa miguu
3.Kumwagiwa maji machafu pale upitapo karibu kwani jamaa wanapomwagia gari(kusafisha )hawaangalia kama kuna watu wanapita.

Pendekezo langu ni kwa mamlaka zinazohusika kukomesha hili jambo kwanza kwa kuyashika magari yanaoshwa hayo maeneo,na kutoa faini kubwa kwa kufanya hivyo naamini hakuna mtu atakayepeleka gari lake lioshwe hapo na waosha magari watakosa magari ya kuyaosha.
Mwisho tunawaomba wenye magari jamani hayo magari mnaweza kuoshea majumbani kwenu au sehemu maalumu za kuogesha,tutunze barabara zetu na mazingira kwani wenye magari ndio mtakuwa watu wa kwanza kulalamika barabara ikianza kuwa kama mashimo ya Tora bora au Kandahar
 
So una suggest wakaoshee wapi? je wametengewa maeneo maalumu? na hao wateja wao wanalitambua hilo? wewe umechukua hatua gani? kuandika hapa JF?
 
Pendekezo langu ni kwa mamlaka zinazohusika kukomesha hili jambo kwanza kwa kuyashika magari yanaoshwa hayo maeneo,na kutoa faini kubwa kwa kufanya hivyo naamini hakuna mtu atakayepeleka gari lake lioshwe hapo na waosha magari watakosa magari ya kuyaosha.
Mwisho tunawaomba wenye magari jamani hayo magari mnaweza kuoshea majumbani kwenu au sehemu maalumu za kuogesha,tutunze barabara zetu na mazingira kwani wenye magari ndio mtakuwa watu wa kwanza kulalamika barabara ikianza kuwa kama mashimo ya Tora bora au Kandahar

Unadhani hao vijana ajira yao itakapo kufa watafanya kazi gani ingali hawana elimu? Ninge kuona wa maana sana kama unge sema watafutiwe maeneo maalumu ili wafanyie kazi zao hapo...

Hawa vijana inawezekana hapo mwanzoni kabla ya kujiajiri na hiyo kazi ya uoshaji wa magari walikuwa vibaka, na sasa wame ondokana na hiyo kazi wameamua kujiajiri wenyewe ili kujikimu kimaisha...

Hawa vijana wanapata pesa yao nzuri sana kwa gari moja wanaosha wa tsh 2000 n a kwa siku wana weza kuosha hadi gari 5 kwa mtu mmoja,
mtaani kwangu kuna sehemu hawa vijana wanaosha magari na mimi huwa na waunga mkono kwa kupeleka gari langu pale wanioshee,maana hao vijana ni wa mtaani kwangu.

Na cha kushangaza kuna car wash hapo hapo hao vijana wanapo osha magari kwa maji machafu na wateja wengi wanakimbilia kwa hawa vijana na car wash imefungwa kwa kukosa wateja.
 
Unadhani hao vijana ajira yao itakapo kufa watafanya kazi gani ingali hawana elimu? Ninge kuona wa maana sana kama unge sema watafutiwe maeneo maalumu ili wafanyie kazi zao hapo...

Hawa vijana inawezekana hapo mwanzoni kabla ya kujiajiri na hiyo kazi ya uoshaji wa magari walikuwa vibaka, na sasa wame ondokana na hiyo kazi wameamua kujiajiri wenyewe ili kujikimu kimaisha...

Hawa vijana wanapata pesa yao nzuri sana kwa gari moja wanaosha wa tsh 2000 n a kwa siku wana weza kuosha hadi gari 5 kwa mtu mmoja,
mtaani kwangu kuna sehemu hawa vijana wanaosha magari na mimi huwa na waunga mkono kwa kupeleka gari langu pale wanioshee,maana hao vijana ni wa mtaani kwangu.

Na cha kushangaza kuna car wash hapo hapo hao vijana wanapo osha magari kwa maji machafu na wateja wengi wanakimbilia kwa hawa vijana na car wash imefungwa kwa kukosa wateja.
Kutokua na ajira sio maanake ndio uvunje sheria,kila mtu akidai afanye anavyotaka kwa kisingizio cha ajira ndio mwanzo wa watu kufanya mambo ya hovyo hovyo basi itabidi,je itakuwa sawa kwa mfano mtu afunge Ng'ombe wake pale mjini Posta eti kwa kisingizio cha kujipatia kipato,na tujalibu kulinganisha mambo je ni lipi jema watu wagongwe na magari au barabara ziharibike au waosha magari waendelea na shughuli zao/ kwa hakika ni upuuzi kusema waosha magari wabaki kisa wanapata mkate,
 
Back
Top Bottom