Wanaojuta ni wengi na wanaoharibu si haba pia

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,648
698,191
Nadhani kuna laana kwenye hizi teuzi za kisiasa kwa wateuliwa wengi.. Nasema ni laana kwakuwa wanakuwa kama wamerukwa na akili kutokana na matendo, matamshi na maamuzi yao hasa wanapokuwa mbele ya makamera ya waandishi wa habari:

. Huchanganyikiwa.
. Utu huwatoka.
. Hujisahau walikotoka, na kushindwa kutafakari yajayo.
. Hukosa adabu na heshima.
. Huwa na ukatili wa ajabu n.k

Akili zao huwabadilika hata kama ni wasomi kwa maana ya kufaulu mitihani na kupata vyeti. Wakishapigwa chini akili huwarudi na kuanza kuwa wanyenyekevu na watu wa kujuta mno.

Msikilize Kigwangala anavyojutia kuwacharaza viboko askari wa wanyamapori mbele ya kadamnasi. Watu wazima na familia zao kuwadhalilisha namna ile. Leo hayupo pale alipokuwa kuna mzimu wenye kumtia hofu mno unamuandama na anajutia matendo yake yale.

Msikilize Gambo anavyolalama! Anahisi kuonewa, anahisi kuchukiwa, anahisi kufanyiwa vitendo viovu! Huyu ndio Gambo RC mwenye nguvu nyakati zake wa kuitwa ofisi ya DC akajieleze.. Ni Gumbo huyu leo hii wa kubebewa condom na lotion nyumbani kwake ili vitumikeje?

Makonda mla bata namba moja duniani kijana mjivuni katili aliyejawa dharau leo anaishi kama digidigi, hana misafara tena! Hana wasaidizi hana walinzi, hana uwezo tena wa kumpigia simu rais na kuweka loud speaker.. Ama kweli maisha hayana formula.

Sabaya.. Kukamatwa kwake watu walifanya sherehe wiki nzima wakila na kunywa! Huyu ndio yule alikuwa anaingia popote na kufanya lolote na asifanywe kitu na yeyote yule... Sasa hivi ni hata rufaa zake zinawekewa mapingamizi na aliokuwa nao pamoja.

Hawa ni mifano michache kama key figures! Lakini list ni ndefu sana.. Kuna wale wasaliti na waliounga juhudi, kuna kina Dr. Mihogo, bro wangu Kakurwa nknk.. Leo hii wanaishi kwa wasiwasi kutojiamini na majuto makubwa

Waliopo kwenye chart kwasasa kuna baadhi wamegutuka! Kwamba kuna kesho, baadhi wanarudia makosa yale yale ya wenzao! Kauli na matendo yao bi kama vile watabaki hapo walipo milele. OLE WAO!

Hawa ni masikio ya kufa hayasikii dawa ama wameyatia nta wasisikie. Baadhi watamaliza mwaka nasisi mtaani! Tutawakaribisha bila kinyongo! Baadhi mwakani. Wengine kabla ya 2025 na wengine baada ya hapo! Tuwaombee wote.

Kuna yule DC kamchapa binti kofi la uso! Kuna huyu diwani kawacharaza vikongwe bakora! Watu ambao ni sawa ama zaidi ya wazazi wake! Laana inayomjia atakuja kuweweseka mitandaoni!

 
ASANTE KWA NARRATION NZURI KUTUKUMBUSHA KUWA KUNA KESHO!
NAONGEZA, WALAANIWE WOTE HAO ULIOWATAJA NA WENGINE WA IVYO! TUWAUIZE AZORY GWANDA, BEN SAANANE , MAWAZO NA WENGINE WAKO WAPI? WANAWEZA WAKAWA NA CLUE WAHUNI, WAUAJI WAKUBWA
Mzee Rwajabe.. With tragedy end...!
 
Uzi Bora kabisa, naangalia hawa viongozi nawaona kabisa Wana matatizo makubwa. Kigwa lazima atawehuka siku siyo nyingi, Gambo huyu tunahesabu tu siku.

Namtafakari Waziri wa Fedha, najisikia vibaya, elimu yake ana itukana wazi wazi bila aibu.
 
MASIKINI HUYU BABA!
Source #1:

Source #2:

MAMBOSASA AMEIBUA MASWALI MAGUMU 12 KUHUSU KIFO CHA LWAJABE

Juzi niliandika kuwa Leopold Lwajabe, aliyekuwa Mkurugenzi wa miiradi ya Umoja wa Ulaya nchini (EU) katika Wizara ya Fedha na Mipango, ambaye alikutwa ananinginia mwisho wa wiki, kabla ya kifo chake alilazimishwa kuandika wosia, wahusika wakauchomkea ofisini kwake kwa siri ili kuficha mazingira ya kifo chake.

Leo jioni nimemsikia Lazaro Mambosasa, Kamanda za Polisi Kanda ya Dar es Salaam, akithibitisha andiko langu kwa kulitokea maelezo, hasa kuhusu WOSIA. Mtu yeyote anayejua saikolojia, anaelewa kwanini Mambosasa amejitokeza kuzungumzia wosia huo.

Katika andiko langu la awali lililosambaa kwenye mitandao ya kijamii nilisema:

INASIKITISHA: YA NDANI KUHUSU KIFO CHA LWAJABE

Dotto James, Katibu Mkuu Hazina (mpwa wa Raid Magufuli) ambaye ni bosi wa Leopold Lwajabe anatuhumiwa kuwa na mkono katika sakata la kifo cha LWAJABE.

Juzi kabla mwili haujapatikana Dotto alikuwa na vikao vya siri na polisi wasio na sare kujadili statement waliyopika kuhusu marehemu. Yeye alijulishwa kifo Jumamosi usiku, na Jumapili alishinda na hao polisi.

Lwajabe alikuwa akilalamika juu ya watu wanaomfuata kutaka hela za kitengo cha EU hapo wizarani. Alipokataa walimtisha kuwa wanamjua kila kitu na kuwa yeye ni raia wa Rwanda.

Katika kipindi hiki cha kuhangaishwa kwake, familia yake huko Karagwe ilihojiwa na maafisa usalama kuhusu uraia wake mara kadhaa.

Alipotekwa mara ya kwanza wiki moja iliyopita, alisainishwa makaratasi ya ofisi na kisha akalazimishwa kuwapa password ya ATM card na fedha zake zikachukuliwa zote.

Alirudushwa na gari la Noah na kutupwa jirani na kwake Kinyerezi. Waliomrudisha hawakutaka kujulikana. Gari jingine liliendelea kuzunguka eneo hilo kwa siku mbili kuchunguza kina nani wanafika na kutoka.

Yeye alikuwa kama amechanganyikiwa na akawa anatoa hadithi zinazojichanganya. Mwenyewe alitishwa kuwa akisema yaliyomtokea watarudi kummaliza. Wamemmaliza kimya kimya! Alipotekwa mara ya pili, wiki hii iliyoisha juzi, polisi waliendelea kuwatuliza ndugu zake kuwa ataonekana ndani ya saa 72, wakawaonya wasisemeseme sana.

Chanzo kutoka ofisi ya ZCO kinadai watekaji wake si polisi ila ni watu wenye nguvu waliokuwa wanawaagiza polisi mambo ya kufanya. Lwajabe alifanyiwa unyama mkubwa. Alilawitiwa na kupigwa picha. Alilazimishwa kuandika barua kuwa amejiua kwa sababu ya matatizo yake binafsi na kwamba asilaumiwe yeyote. Alilazimishwa kuandika wosia na ukapelekwa na kuingizwa ofisini kwake. Wauaji walimfunga kamba na kumtupa kichakani Mkuranga.

Kisha waliwaelekeza polisi waende kuchukua mwili na kuuweka hospitali. Polisi hawakwenda na camera kuchukua picha za eneo wala kuchukua alama za vidole mwilini. Mmoja wa wapelelezi ni ndugu ya marehemu, na alipogundulika polisi walisitisha jitihada zote za kupika ripoti. Ukweli ulio wazi ni kwamba kuna kundi maalumu la siri serikalini lipo juu ya kila taasisi, na linachotaka ni fedha. Ni ujambazi wa kidola. Inasikitisha sana!

MASWALI YANAYOIBULIWA NA MAMBOSASA:

Kauli ya Mambosasa kuwa Lwajabe alijiua na aliandika wosia huo uliokutwa ofisini mwake, imethibitisha nilichoandika awali, na imeibua maswali mengine kadhaa.

Hapa naweka maswali 12 ya msingi ya haraka haraka ambayo Mambosasa angepaswa kuyajibu:

1. Mtu ambaye ameshaamua kujiua kwa kujinyonga mtini, hadi anaandika wosia na kuuacha ofisini, kwa nini atoke Dar es Salaam asafiri na kupita miti yote hadi Mkuranga, huku nyumbani kwake Kinyerezi kumejaa miti ya miembe ambayo ingemfaa kwa jambo hilo?

2. Lwajabe aliondoka nyumbani kwake akiwa amevaa shati. Amekutwa mortuary Mkuranga akiwa na tisheti. Kama Mambosasa ni mkweli, kwa nini hadi sasa dereva wake, karani wake na ndugu zake hawajahojiwa juu ya mabadiliko haya ya mavazi?

3. Kwanini polisi waliamua kumuondoa eneo la "kujinyongea" na kumpeleka mortuary bila kuita ndugu zake, wakati walikuwa na RB namba za kupotea kwake? Walikuwa na haraka ya nini?

4. Kwanini polisi hawakutumia forensic equipments ili kurahisisha uchunguzi?

5. Kwanini polisi hawakutaka ndugu wa marehemu kushiriki katika post-mortem na kwanini hawakuwapa taarifa za awali za uchunguzi?

6. Kwanini serikali ilijua wosia wa marehemu kabla ya kifo kutangazwa. Kwa nini polisi walikuwa wanamtafuta marehemu mezani kuliko vichakani?

7. Kabla ya kifo chake, kwanini maofisa usalama mkoani Kagera walisumbua familia yake na kuchukua maelezo yao baada ya Lwajabe kutekwa mara ya kwanza? Kwa nini mdogo wa marehemu aitwaye Meneja Byase alihojiwa na TISS kipindi marehemu ametekwa mara ya kwanza? Walihoji kuhusu nini, na mbona Mambosasa hasemi haya?

8. Kwanini Katibu Mkuu Hazina, Dotto James, alikuwa anamlazimisha Lwajabe aende likizo ya wiki mbili baada ya kuwa ametekwa mara ya kwanza?

9. Kwanini askari wa Kikosi Kazi (Task force) wasichukuliwe alama za vidole ili kulinganisha na alama za vidole kwenye baadhi ya vitu vilivyochukuliwa na askari aliyewatoroka na akaviacha kituo cha polisi Mburahati?

10. Kwanini polisi walikazana kutaka ndugu wa marehemu wasisemeseme na kwamba ndugu yao angeonekana ndani ya saa 72 baada ya kutekwa? Walijuaje? Lengo lao lilikuwa nini?

11. Kwanini Katibu Mkuu Dotto alizuia kifo cha Lwajabe kutangazwa Jumamosi jioni wakati mwili ulishaonekana?

12. Lwajabe aliporudishwa mara ya kwanza baada ya kutekwa, gari la Noah jeusi lilikuwa linazunguka mtaani kwake. Watu walilitilia shaka, wakachukua namba zake na kuwajulisha polisi. Mbona hadi sasa polisi hawajatoa taarifa juu ya hatua walizochukua dhidi ya gari hilo wala hawajasema ni la nani?

Bora Mambosasa angekaa kimya. Kama anatumwa aseme, awaeleza wanaomtuma kuwa wanaoelezwa kumsikiliza wana akili timamu, na wanachikozwa kusema mengine ambayo wasingeyasema iwapo asingesema.

Ndiyo, walimtisha Lwajabe asiseme wazi alichotendwa, lakini hakuna siri ya watu wawili.

Sawa, wafanye mizaha hii, lakini watambue kuwa damu ya Lwajabe ina thamani kama ilivyo damu ya Mambosasa. Tuheshimu utu wa wenzetu! Utu wetu ni bora kuliko vyeo na madaraka ya wanaomtuma kudhihaki uhai wa Lwajabe!

Imeandikwa na Ngurumo

Tunachokijua:
 
2015 imbeba laana zao nyingi na zinawatesa na zita watesa sababu 5 ya mwisho hipo nayo 2025.

Na itaandikwa historia 2025 ijawahi tokea na kubaki watu midomo wazi.

5 uwezi kuigawa na ukiondoa inabaki 202.nayo iwezi kugawanyina.

hata wakijumlisha 2+0+2+5=9 nayo iwezi kugawanyika.

Inaonyesha kutakuwa na nguvu kubwa ya wananchi kuchoka na hasira ambazo zitapelekea aibu wakishindwa kujitetea huku nchi ikiwa kwenye kamba nyekundu ya maamuzi ya hatima yao kuanzia uchumi,mbeleni na n.k
 
2015 imbeba laana zao nyingi na zinawatesa na zita watesa sababu 5 ya mwisho hipo nayo 2025.

Na itaandikwa historia 2025 ijawahi tokea na kubaki watu midomo wazi.

5 uwezi kuigawa na ukiondoa inabaki 202.nayo iwezi kugawanyina.

hata wakijumlisha 2+0+2+5=9 nayo iwezi kugawanyika.

Inaonyesha kutakuwa na nguvu kubwa ya wananchi kuchoka na hasira ambazo zitapelekea aibu wakishindwa kujitetea huku nchi ikiwa kwenye kamba nyekundu ya maamuzi ya hatima yao kuanzia uchumi,mbeleni na n.k
Kivyovyote vile hiyo ni namba witiri.. 20 + 25 = 75 au 2 + 0+ 2+ 5 = 9
 
Nadhani kuna laana kwenye hizi teuzi za kisiasa kwa wateuliwa wengi.. Nasema ni laana kwakuwa wanakuwa kama wamerukwa na akili kutokana na matendo, matamshi na maamuzi yao hasa wanapokuwa mbele ya makamera ya waandishi wa habari:

. Huchanganyikiwa.
. Utu huwatoka.
. Hujisahau walikotoka, na kushindwa kutafakari yajayo.
. Hukosa adabu na heshima.
. Huwa na ukatili wa ajabu n.k

Akili zao huwabadilika hata kama ni wasomi kwa maana ya kufaulu mitihani na kupata vyeti. Wakishapigwa chini akili huwarudi na kuanza kuwa wanyenyekevu na watu wa kujuta mno.

Msikilize Kigwangala anavyojutia kuwacharaza viboko askari wa wanyamapori mbele ya kadamnasi. Watu wazima na familia zao kuwadhalilisha namna ile. Leo hayupo pale alipokuwa kuna mzimu wenye kumtia hofu mno unamuandama na anajutia matendo yake yale.

Msikilize Gambo anavyolalama! Anahisi kuonewa, anahisi kuchukiwa, anahisi kufanyiwa vitendo viovu! Huyu ndio Gambo RC mwenye nguvu nyakati zake wa kuitwa ofisi ya DC akajieleze.. Ni Gumbo huyu leo hii wa kubebewa condom na lotion nyumbani kwake ili vitumikeje?

Makonda mla bata namba moja duniani kijana mjivuni katili aliyejawa dharau leo anaishi kama digidigi, hana misafara tena! Hana wasaidizi hana walinzi, hana uwezo tena wa kumpigia simu rais na kuweka loud speaker.. Ama kweli maisha hayana formula.

Sabaya.. Kukamatwa kwake watu walifanya sherehe wiki nzima wakila na kunywa! Huyu ndio yule alikuwa anaingia popote na kufanya lolote na asifanywe kitu na yeyote yule... Sasa hivi ni hata rufaa zake zinawekewa mapingamizi na aliokuwa nao pamoja.

Hawa ni mifano michache kama key figures! Lakini list ni ndefu sana.. Kuna wale wasaliti na waliounga juhudi, kuna kina Dr. Mihogo, bro wangu Kakurwa nknk.. Leo hii wanaishi kwa wasiwasi kutojiamini na majuto makubwa

Waliopo kwenye chart kwasasa kuna baadhi wamegutuka! Kwamba kuna kesho, baadhi wanarudia makosa yale yale ya wenzao! Kauli na matendo yao bi kama vile watabaki hapo walipo milele. OLE WAO!

Hawa ni masikio ya kufa hayasikii dawa ama wameyatia nta wasisikie. Baadhi watamaliza mwaka nasisi mtaani! Tutawakaribisha bila kinyongo! Baadhi mwakani. Wengine kabla ya 2025 na wengine baada ya hapo! Tuwaombee wote.

Kuna yule DC kamchapa binti kofi la uso! Kuna huyu diwani kawacharaza vikongwe bakora! Watu ambao ni sawa ama zaidi ya wazazi wake! Laana inayomjia atakuja kuweweseka mitandaoni!

View attachment 2448613
Binadam tumeumbwa na haya! Lakini ogopa sana fyuzi ikiachia unaweza Fanya jambo zito
 
Nadhani kuna laana kwenye hizi teuzi za kisiasa kwa wateuliwa wengi.. Nasema ni laana kwakuwa wanakuwa kama wamerukwa na akili kutokana na matendo, matamshi na maamuzi yao hasa wanapokuwa mbele ya makamera ya waandishi wa habari:

. Huchanganyikiwa.
. Utu huwatoka.
. Hujisahau walikotoka, na kushindwa kutafakari yajayo.
. Hukosa adabu na heshima.
. Huwa na ukatili wa ajabu n.k

Akili zao huwabadilika hata kama ni wasomi kwa maana ya kufaulu mitihani na kupata vyeti. Wakishapigwa chini akili huwarudi na kuanza kuwa wanyenyekevu na watu wa kujuta mno.

Msikilize Kigwangala anavyojutia kuwacharaza viboko askari wa wanyamapori mbele ya kadamnasi. Watu wazima na familia zao kuwadhalilisha namna ile. Leo hayupo pale alipokuwa kuna mzimu wenye kumtia hofu mno unamuandama na anajutia matendo yake yale.

Msikilize Gambo anavyolalama! Anahisi kuonewa, anahisi kuchukiwa, anahisi kufanyiwa vitendo viovu! Huyu ndio Gambo RC mwenye nguvu nyakati zake wa kuitwa ofisi ya DC akajieleze.. Ni Gumbo huyu leo hii wa kubebewa condom na lotion nyumbani kwake ili vitumikeje?

Makonda mla bata namba moja duniani kijana mjivuni katili aliyejawa dharau leo anaishi kama digidigi, hana misafara tena! Hana wasaidizi hana walinzi, hana uwezo tena wa kumpigia simu rais na kuweka loud speaker.. Ama kweli maisha hayana formula.

Sabaya.. Kukamatwa kwake watu walifanya sherehe wiki nzima wakila na kunywa! Huyu ndio yule alikuwa anaingia popote na kufanya lolote na asifanywe kitu na yeyote yule... Sasa hivi ni hata rufaa zake zinawekewa mapingamizi na aliokuwa nao pamoja.

Hawa ni mifano michache kama key figures! Lakini list ni ndefu sana.. Kuna wale wasaliti na waliounga juhudi, kuna kina Dr. Mihogo, bro wangu Kakurwa nknk.. Leo hii wanaishi kwa wasiwasi kutojiamini na majuto makubwa

Waliopo kwenye chart kwasasa kuna baadhi wamegutuka! Kwamba kuna kesho, baadhi wanarudia makosa yale yale ya wenzao! Kauli na matendo yao bi kama vile watabaki hapo walipo milele. OLE WAO!

Hawa ni masikio ya kufa hayasikii dawa ama wameyatia nta wasisikie. Baadhi watamaliza mwaka nasisi mtaani! Tutawakaribisha bila kinyongo! Baadhi mwakani. Wengine kabla ya 2025 na wengine baada ya hapo! Tuwaombee wote.

Kuna yule DC kamchapa binti kofi la uso! Kuna huyu diwani kawacharaza vikongwe bakora! Watu ambao ni sawa ama zaidi ya wazazi wake! Laana inayomjia atakuja kuweweseka mitandaoni!

View attachment 2448613
Diwani wa ccm tena🤣🤣
 
Back
Top Bottom