BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Date::11/20/2008
Wananchi watawanywa kwa mabomu wakigombea kununua viwanja
Na Habel Chidawali, Dodoma
Mwananchi
POLISI wa kutuliza ghasia, FFU jana walilazimika kutumia mabomu ya machozi kurejesha amani, baada ya vurugu kubwa kutokea wakati wakazi wa Dodoma walipokuwa wakigombea kuingia ofisi za Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa ajili ya kununua viwanja.
Milio ya mabomu ya machozi na kelele zilitawala kwenye eneo hilo lililo katikati ya mji wa Dodoma, ambako zoezi la ugawaji wa viwanja 500 vilivyopimwa lilipoanza vibaya baada ya watu waliokesha kuwahi nafasi kwenye foleni ili waweze kununua viwanja mapema.
Viwanja hivyo vilivyo maeneo ya Ndachi vinauzwa Sh250,000 kwa kiwanja kidogo kabisa, Sh270,000 kwa kiwanja cha ukubwa wa kati wakati viwanja vikubwa zaidi vinauzwa Sh370,000.
Watu walikuwa wamewahi kujipanga kwenye foleni tangu juzi saa 4:00 usiku na hadi jana alfajiri ofisi hizo zilikuwa zimefurika watu kiasi cha kusababisha Barabara ya Nne (ya Msikiti wa Nunge) kutopitika na kulazimisha magari kutumia njia nyingine kuelekea kwenye shughuli zao.
Baadhi ya watu waliofika eneo hilo juzi usiku walilazimika kupokezana na ndugu, ili waweze kwenda kula na wengine kulala na kurejea jana alfajiri kusubiri kumilikishwa viwanja vipya.
Lakini, vurugu zililipuka baada ya wananchi hao waliokesha eneo hilo na wengine kuwahi alfajiri, kuona wenzao waliofika asubuhi wakifanya ujanja wa kujipenyeza na kupewa nafasi ya kuwahi kuingia ndani ya ofisi, huku polisi waliokuwa wakisimamia utaratibu wakionekana kubariki vitendo hivyo.
Hapo ndipo walipoanza kurushiana maneno makali kabla ya kuanza mapigano yaliyosababisha FFU kuitwa eneo hilo na kutumia nguvu kutuliza ghasia. Polisi hao waliwapanga upya wananchi na kuanza kuingia ofisini kwa utaratibu.
Wengi wa watu waliokuwepo ofisi za CDA ni wananchi kutoka katika mitaa ya Njedengwa, Mtube, Mjimwema na Bochela ambako mamlaka hiyo iliendesha bomoabomoa katika siku za karibuni na kukosa makazi, hali iliyowafanya wawe na matumaini kuwa zoezi la ugawaji viwanja lingewapendelea.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Omary Mganga alisema kuwa baada ya kupata taarifa hizo, aliwatuma vijana wake kwenda kutuliza ghasia hizo, lakini akafafanua kuwa hakuwatuma kwenda kupiga mabomu katikati ya mji na akaahidi kuwa atalitolea ufafanuzi zaidi suala hilo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa CDA, Martin Kitila alisema kuwa zoezi hilo ni zuri na kwamba, litakuwa endelevu kutokana na ukweli kuwa liliwashirikisha watu wa tabaka zote.
Kitila alisema kuwa jana ilikuwa ni siku ya kugawa viwanja 500 katika eneo la Ndachi, lakini akaongeza kuwa wataendelea kugawa viwanja kadri watakavyokuwa wamepima na akawaomba wale wote watakaokosa kwa awamu hii wasubiri awamu ijayo.
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, zoezi la ugawaji viwanja liliwashirikisha wadau mbalimbali vikiwemo vyombo vya dola, Takukuru na watu mbalimbali ambao walifika kuona jinsi zoezi hilo linavyoendeshwa.
Alisema uongozi wa CDA hauhusiki na tukio la jana kwa kuwa kazi hiyo alipewa mtu mwingine na kuwafanya wafanyakazi wa CDA kuwa na mapumziko jana.
Katika siku za hivi karibuni, CDA wamekuwa wakilalamikiwa kuhusu kuchelewesha kukamilisha zoezi la upimaji viwanja na kuendesha bomoabomoa kwa nyumba za watu na hivyo kuwakosesha makazi. Suala hilo liliwakasirisha madiwani na kutoa tamko.
Viwanja mkoani Dodoma vimekuwa lulu tangu vyuo vya elimu ya juu vianze kuongezeka na hivyo kusababisha biashara ya nyumba kuwa juu kutokana na wanafunzi na wahadhiri kupanga nje ya maeneo ya vyuo.
Mbali na vyuo, shughuli nyingi za kiserikali, semina na Bunge la Jamhuri ya Muungano zinazofanyika mkoani humo zinaufanya mji huo uzidi kuchangamka, huku kukamilika kwa ujenzi wa barabara zinazoingia mkoani humo kukizidi kuingiza watu wengi zaidi.
Wananchi watawanywa kwa mabomu wakigombea kununua viwanja
Na Habel Chidawali, Dodoma
Mwananchi
POLISI wa kutuliza ghasia, FFU jana walilazimika kutumia mabomu ya machozi kurejesha amani, baada ya vurugu kubwa kutokea wakati wakazi wa Dodoma walipokuwa wakigombea kuingia ofisi za Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa ajili ya kununua viwanja.
Milio ya mabomu ya machozi na kelele zilitawala kwenye eneo hilo lililo katikati ya mji wa Dodoma, ambako zoezi la ugawaji wa viwanja 500 vilivyopimwa lilipoanza vibaya baada ya watu waliokesha kuwahi nafasi kwenye foleni ili waweze kununua viwanja mapema.
Viwanja hivyo vilivyo maeneo ya Ndachi vinauzwa Sh250,000 kwa kiwanja kidogo kabisa, Sh270,000 kwa kiwanja cha ukubwa wa kati wakati viwanja vikubwa zaidi vinauzwa Sh370,000.
Watu walikuwa wamewahi kujipanga kwenye foleni tangu juzi saa 4:00 usiku na hadi jana alfajiri ofisi hizo zilikuwa zimefurika watu kiasi cha kusababisha Barabara ya Nne (ya Msikiti wa Nunge) kutopitika na kulazimisha magari kutumia njia nyingine kuelekea kwenye shughuli zao.
Baadhi ya watu waliofika eneo hilo juzi usiku walilazimika kupokezana na ndugu, ili waweze kwenda kula na wengine kulala na kurejea jana alfajiri kusubiri kumilikishwa viwanja vipya.
Lakini, vurugu zililipuka baada ya wananchi hao waliokesha eneo hilo na wengine kuwahi alfajiri, kuona wenzao waliofika asubuhi wakifanya ujanja wa kujipenyeza na kupewa nafasi ya kuwahi kuingia ndani ya ofisi, huku polisi waliokuwa wakisimamia utaratibu wakionekana kubariki vitendo hivyo.
Hapo ndipo walipoanza kurushiana maneno makali kabla ya kuanza mapigano yaliyosababisha FFU kuitwa eneo hilo na kutumia nguvu kutuliza ghasia. Polisi hao waliwapanga upya wananchi na kuanza kuingia ofisini kwa utaratibu.
Wengi wa watu waliokuwepo ofisi za CDA ni wananchi kutoka katika mitaa ya Njedengwa, Mtube, Mjimwema na Bochela ambako mamlaka hiyo iliendesha bomoabomoa katika siku za karibuni na kukosa makazi, hali iliyowafanya wawe na matumaini kuwa zoezi la ugawaji viwanja lingewapendelea.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Omary Mganga alisema kuwa baada ya kupata taarifa hizo, aliwatuma vijana wake kwenda kutuliza ghasia hizo, lakini akafafanua kuwa hakuwatuma kwenda kupiga mabomu katikati ya mji na akaahidi kuwa atalitolea ufafanuzi zaidi suala hilo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa CDA, Martin Kitila alisema kuwa zoezi hilo ni zuri na kwamba, litakuwa endelevu kutokana na ukweli kuwa liliwashirikisha watu wa tabaka zote.
Kitila alisema kuwa jana ilikuwa ni siku ya kugawa viwanja 500 katika eneo la Ndachi, lakini akaongeza kuwa wataendelea kugawa viwanja kadri watakavyokuwa wamepima na akawaomba wale wote watakaokosa kwa awamu hii wasubiri awamu ijayo.
Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, zoezi la ugawaji viwanja liliwashirikisha wadau mbalimbali vikiwemo vyombo vya dola, Takukuru na watu mbalimbali ambao walifika kuona jinsi zoezi hilo linavyoendeshwa.
Alisema uongozi wa CDA hauhusiki na tukio la jana kwa kuwa kazi hiyo alipewa mtu mwingine na kuwafanya wafanyakazi wa CDA kuwa na mapumziko jana.
Katika siku za hivi karibuni, CDA wamekuwa wakilalamikiwa kuhusu kuchelewesha kukamilisha zoezi la upimaji viwanja na kuendesha bomoabomoa kwa nyumba za watu na hivyo kuwakosesha makazi. Suala hilo liliwakasirisha madiwani na kutoa tamko.
Viwanja mkoani Dodoma vimekuwa lulu tangu vyuo vya elimu ya juu vianze kuongezeka na hivyo kusababisha biashara ya nyumba kuwa juu kutokana na wanafunzi na wahadhiri kupanga nje ya maeneo ya vyuo.
Mbali na vyuo, shughuli nyingi za kiserikali, semina na Bunge la Jamhuri ya Muungano zinazofanyika mkoani humo zinaufanya mji huo uzidi kuchangamka, huku kukamilika kwa ujenzi wa barabara zinazoingia mkoani humo kukizidi kuingiza watu wengi zaidi.