Makaayamawe
JF-Expert Member
- Feb 21, 2009
- 341
- 9
Wanajeshi wampiga trafiki kikatili wadai kucheleweshwa Ubungo Dar
Kikundi cha askari wa usalama barabarani wakimsikiliza Mkuu wa kituo cha usalama barabarani mkoa wa Kinondoni, ASP Awadhi Haji (katikati) akiwasiliana kwa radio mara baada askari aliyekuwa akiongoza magari katika makutano ya Ubungo, Sajini Thomas Mayapila (kulia) kupigwa na askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) waliokuwa wakitoka Mwenge kwa mabasi, kwa madai ya kuwachelewesha safari yao.Na Mwandishi Wetu
ASKARI wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), jana walimshambulia na kumpiga askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Sajenti Thomas Mayapila, wakidai aliwachelewesha kupita eneo la Ubungo.
Tukio hilo lilitokea jana asubuhi wakati Thomas akiwa kazini kuongoza magari katika makutano ya Barabara za Morogoro, Sam Nujoma na Mandela, Ubungo, eneo ambalo kwa kawaida huwa na misululu mirefu ya magari nyakati za asubuhi na jioni.
Tukio hilo lilitokea saa 1:35 asubuhi wakati trafiki huyo akiendelea na kazi yake ya kuongoza magari katika eneo hilo, akionekana kutofahamu kuwa kulikuwa na magari matatu ya JWTZ yaliyokuwa yakitokea Barabara ya Sam Nujoma na kuelekea Buguruni.
Tofauti na siku ambazo JWTZ huwa na shughuli rasmi, magari hayo matatu- 1931 JW08,1908 JW08 na Land Rover Defender lenye namba 2994 JW08- hayakuwa yakiongozwa na gari lenye king'ora wala ishara yoyote.
Baada ya magari hayo kupita eneo la makutano ya barabara hizo, maarufu kama Ubungo Mataa, wanajeshi wawili walishuka mmoja akiwa na cheo cha staff sargent ambaye alishika mkanda wake mkononi na dereva wa basi, na kumtupia maneno ya vitisho trafiki huyo na baadaye kuanza kumpiga makofi na ngumi.
Hata hivyo, trafiki huyo alionekana kuwa mkakamavu baada ya kutumia mbinu nyingi za kujihami, zilizowafanya wanajeshi wengine washuke kwenye magari yao na kwenda kumchangia.
Wingi wa wanajeshi hao waliokuwa wakimgombea mithili ya kunguru kwenye mzoga, ulimshinda polisi huyo na akajikuta akiangushwa chini na kukanyagwa shingoni mithili ya kuku anayesubiri kuchinjwa.
Wakati wakiendeleza ukatili huo, wanajeshi hao walikuwa wakimkejeli trafiki huyo na kazi yake, kana kwamba si chochote na kudai alikuwa akiwachelewesha kwenda kutekeleza majukumu yao, huku polisi huyo akihoji uhalali wa kumvamia na kumpiga.
"Kwa nini mnanipiga na mimi nipo kazini kama ninyi, niambieni sababu ya kunipiga... na mimi ninatimiza wajibu wangu hapa. Nimeajiriwa na serikali kama nyinyi," alilalama Sajenti Thomas wakati akipigwa na wanajeshi hao.
Umati uliokuwa ukishuhudia kipigo hicho ulikuwa ukimshangilia trafiki huyo kwa ujasiri wake wa kujihami na kuwazomea wanajeshi hao kabla ya askari mwenye cheo cha Luteni Kanali kutokea na kuamuru askari wenzake kumwacha trafiki huyo. Wote wakaingia kwenye magari yao na kuondoka eneo hilo.
Tukio hilo lililodumu kwa takriban dakika 18, lilisababisha magari yaliyokuwa kwenye msululu kutosogea na hivyo kuongeza msongamano kwenye eneo hilo linalohitaji uongozi wa ziada nyakati za asubuhi na jioni wakati watu wakielekea makazini na kurejea nyumbani.
"Ni kama sinema ya bure kuona mwajiriwa mmoja wa serikali anatimiza wajibu wake halafu mwajiriwa mwingine wa serikali anatokea na kuingilia utendaji huo na kumhukumu.Hii inatushangaza sisi wananchi tunaoamini kuwa wote wapo kututumikia," alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Dakika chache baada ya askari hao kuondoka, walifika trafiki wengine sita wa vyeo tofauti akiwemo mrakibu msaidizi wa polisi, Awadh Haji ambaye ni mkuu wa kituo cha usalama barabarani cha Kinondoni.
Haji alimpa pole Sajenti Thomas na kumshauri aende kando ya barabara kujipumzisha na baadaye Thomas aliondolewa eneo la tukio na afande Haji akiongozana na wenzake wawili waliotumia gari aina ya Toyota Chaser namba T370AZR na kuacha wananchi wakiwashangilia.
Baadhi ya wananchi waliokuwa eneo hilo walisema wako tayari kutoa ushahidi iwapo trafiki huyo atakwenda mahakamani na kuwashtaki askari hao.
"Unajua si mchezo, umepambana na askari wote wale waliokuwa wanataka kukuonea duh, unastahili pongezi na kuongezwa cheo. Tutatoa ushahidi wetu ukienda mahakamani, tupo tayari," alisema mmoja wa mashuhuda kabla ya Sajenti Thomas kuondolewa eneo la tukio.
Mwananchi ilitaarifiwa kuwa trafiki huyo aliandika maelezo yake kituo cha Oysterbay.
Tayari Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na JWTZ wameunda tume ya pamoja kuchunguza tukio hilo kwa siku moja, anaripoti Ummy Muya.
Kamanda mwandamizi wa polisi wa kanda ya Dar es salaam, Suleiman Kova, akiwa ofisini alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea nyakati za asubuhi, lakini mpaka anazungumza na Mwananchi bado tume hiyo haikuwa imemkabidhi taarifa za tukio hilo.
Ni kweli leo asubuhi kulitokea tukio hilo la wanajeshi kumpiga askari wa usalama barabarani katika eneo la Ubungo, lakini hatufahamu ni nini hasa kilichosababisha wanajeshi hao kufanya kitendo hicho, alisema.
Wananchi wema walinifikishia taarifa kwa njia ya simu wakati wa tukio. Kutokana na kuwa na mahusiano mazuri, tumeunda tume ya pamoja ambayo mpaka leo jioni (jana) taarifa itakuwa tayari.
Wakati huohuo, Kamanda Kova alithibitisha kukamatwa kwa watu watatu ambao wanasadikika kuwa walipanga njama za kwenda kuiba katika duka moja la kubaidishia fedha Mei 8 eneo la Kariakoo.
Kamanda Kova alisema waliwakamata watu hao Jumapili iliyopita na kuwataja kuwa ni Abdallah Mohamed, 25, mkazi wa Yombo Kisiwani, ambaye Kova alikutwa na bastola aina ya Chinese inayotumiwa na vyombo vya dola ambayo inasadikiwa mtuhumiwa aliifuta namba. Mtuhumiwa mwingine, kwa mujibu wa Kova, ni Hatibu Ibrahim, 29, ambaye ni mkazi wa Mtoni Kichangani na Hassain Mzava, 39, maarufu Mzungu ambaye anaishi Yombo.
Kikundi cha askari wa usalama barabarani wakimsikiliza Mkuu wa kituo cha usalama barabarani mkoa wa Kinondoni, ASP Awadhi Haji (katikati) akiwasiliana kwa radio mara baada askari aliyekuwa akiongoza magari katika makutano ya Ubungo, Sajini Thomas Mayapila (kulia) kupigwa na askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) waliokuwa wakitoka Mwenge kwa mabasi, kwa madai ya kuwachelewesha safari yao.Na Mwandishi Wetu
ASKARI wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), jana walimshambulia na kumpiga askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Sajenti Thomas Mayapila, wakidai aliwachelewesha kupita eneo la Ubungo.
Tukio hilo lilitokea jana asubuhi wakati Thomas akiwa kazini kuongoza magari katika makutano ya Barabara za Morogoro, Sam Nujoma na Mandela, Ubungo, eneo ambalo kwa kawaida huwa na misululu mirefu ya magari nyakati za asubuhi na jioni.
Tukio hilo lilitokea saa 1:35 asubuhi wakati trafiki huyo akiendelea na kazi yake ya kuongoza magari katika eneo hilo, akionekana kutofahamu kuwa kulikuwa na magari matatu ya JWTZ yaliyokuwa yakitokea Barabara ya Sam Nujoma na kuelekea Buguruni.
Tofauti na siku ambazo JWTZ huwa na shughuli rasmi, magari hayo matatu- 1931 JW08,1908 JW08 na Land Rover Defender lenye namba 2994 JW08- hayakuwa yakiongozwa na gari lenye king'ora wala ishara yoyote.
Baada ya magari hayo kupita eneo la makutano ya barabara hizo, maarufu kama Ubungo Mataa, wanajeshi wawili walishuka mmoja akiwa na cheo cha staff sargent ambaye alishika mkanda wake mkononi na dereva wa basi, na kumtupia maneno ya vitisho trafiki huyo na baadaye kuanza kumpiga makofi na ngumi.
Hata hivyo, trafiki huyo alionekana kuwa mkakamavu baada ya kutumia mbinu nyingi za kujihami, zilizowafanya wanajeshi wengine washuke kwenye magari yao na kwenda kumchangia.
Wingi wa wanajeshi hao waliokuwa wakimgombea mithili ya kunguru kwenye mzoga, ulimshinda polisi huyo na akajikuta akiangushwa chini na kukanyagwa shingoni mithili ya kuku anayesubiri kuchinjwa.
Wakati wakiendeleza ukatili huo, wanajeshi hao walikuwa wakimkejeli trafiki huyo na kazi yake, kana kwamba si chochote na kudai alikuwa akiwachelewesha kwenda kutekeleza majukumu yao, huku polisi huyo akihoji uhalali wa kumvamia na kumpiga.
"Kwa nini mnanipiga na mimi nipo kazini kama ninyi, niambieni sababu ya kunipiga... na mimi ninatimiza wajibu wangu hapa. Nimeajiriwa na serikali kama nyinyi," alilalama Sajenti Thomas wakati akipigwa na wanajeshi hao.
Umati uliokuwa ukishuhudia kipigo hicho ulikuwa ukimshangilia trafiki huyo kwa ujasiri wake wa kujihami na kuwazomea wanajeshi hao kabla ya askari mwenye cheo cha Luteni Kanali kutokea na kuamuru askari wenzake kumwacha trafiki huyo. Wote wakaingia kwenye magari yao na kuondoka eneo hilo.
Tukio hilo lililodumu kwa takriban dakika 18, lilisababisha magari yaliyokuwa kwenye msululu kutosogea na hivyo kuongeza msongamano kwenye eneo hilo linalohitaji uongozi wa ziada nyakati za asubuhi na jioni wakati watu wakielekea makazini na kurejea nyumbani.
"Ni kama sinema ya bure kuona mwajiriwa mmoja wa serikali anatimiza wajibu wake halafu mwajiriwa mwingine wa serikali anatokea na kuingilia utendaji huo na kumhukumu.Hii inatushangaza sisi wananchi tunaoamini kuwa wote wapo kututumikia," alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Dakika chache baada ya askari hao kuondoka, walifika trafiki wengine sita wa vyeo tofauti akiwemo mrakibu msaidizi wa polisi, Awadh Haji ambaye ni mkuu wa kituo cha usalama barabarani cha Kinondoni.
Haji alimpa pole Sajenti Thomas na kumshauri aende kando ya barabara kujipumzisha na baadaye Thomas aliondolewa eneo la tukio na afande Haji akiongozana na wenzake wawili waliotumia gari aina ya Toyota Chaser namba T370AZR na kuacha wananchi wakiwashangilia.
Baadhi ya wananchi waliokuwa eneo hilo walisema wako tayari kutoa ushahidi iwapo trafiki huyo atakwenda mahakamani na kuwashtaki askari hao.
"Unajua si mchezo, umepambana na askari wote wale waliokuwa wanataka kukuonea duh, unastahili pongezi na kuongezwa cheo. Tutatoa ushahidi wetu ukienda mahakamani, tupo tayari," alisema mmoja wa mashuhuda kabla ya Sajenti Thomas kuondolewa eneo la tukio.
Mwananchi ilitaarifiwa kuwa trafiki huyo aliandika maelezo yake kituo cha Oysterbay.
Tayari Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na JWTZ wameunda tume ya pamoja kuchunguza tukio hilo kwa siku moja, anaripoti Ummy Muya.
Kamanda mwandamizi wa polisi wa kanda ya Dar es salaam, Suleiman Kova, akiwa ofisini alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea nyakati za asubuhi, lakini mpaka anazungumza na Mwananchi bado tume hiyo haikuwa imemkabidhi taarifa za tukio hilo.
Ni kweli leo asubuhi kulitokea tukio hilo la wanajeshi kumpiga askari wa usalama barabarani katika eneo la Ubungo, lakini hatufahamu ni nini hasa kilichosababisha wanajeshi hao kufanya kitendo hicho, alisema.
Wananchi wema walinifikishia taarifa kwa njia ya simu wakati wa tukio. Kutokana na kuwa na mahusiano mazuri, tumeunda tume ya pamoja ambayo mpaka leo jioni (jana) taarifa itakuwa tayari.
Wakati huohuo, Kamanda Kova alithibitisha kukamatwa kwa watu watatu ambao wanasadikika kuwa walipanga njama za kwenda kuiba katika duka moja la kubaidishia fedha Mei 8 eneo la Kariakoo.
Kamanda Kova alisema waliwakamata watu hao Jumapili iliyopita na kuwataja kuwa ni Abdallah Mohamed, 25, mkazi wa Yombo Kisiwani, ambaye Kova alikutwa na bastola aina ya Chinese inayotumiwa na vyombo vya dola ambayo inasadikiwa mtuhumiwa aliifuta namba. Mtuhumiwa mwingine, kwa mujibu wa Kova, ni Hatibu Ibrahim, 29, ambaye ni mkazi wa Mtoni Kichangani na Hassain Mzava, 39, maarufu Mzungu ambaye anaishi Yombo.