Habari kwa hisani ya www.novakambota.com
Ikiwa ni siku moja tangu tovuti iripoti juu ya madai ya Mrisho Gambo ktukanwa na mmoja wa madiwani wa Monduli aitwaye Isaack Caprion, juhudi za tovuti hii kupata undani wa undani wa sakata hilo zimeendela kuzaa mtunda baada kufanikiwakuzungumza na mmoja wa madiwani kutoka Monduli ambaye pia ni mtu wa karibu wa Bw Issack.
Diwani huyo amemwambia mwandishi wa habari hii kuwa Bw Issack hakuwahi kumtukana wala kumtumia message Gambo .ndugu mwandishi nimemuuliza huyo Issaack na ameniambia yeye hajawahi kumtukana wala kumtumia message Bw Mrisho Gambo bali waliwahi kukutana kwa mazunumzo na kamwe hajawahi kumtukana , wanahabari kuweni makini na Gambo yaelekea ansaka umaarufu wa bei chee ndiyo maana amekuja na zushi huu aliakaririwa Diwani huyo.
Tovuti hii imefanikiwa kuzungumza na wadau mbalimbali kuhusiana na sakata hilo ambalo linazidi kuchukua sura mpya ambapo wengi wao wametoa wito kwa CCM kuwa na tabia ya kusuluhisha migogoro inayojitokeza ndani ya chama wao kwa wao badala ya kusubiri au kukimbilia kwa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii hatua ambayo inazidi kubomoa badala ya kujenga.