Hongera kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Hasa Rais wetu mpendwa kwa kupokea Wanafunzi wa Udaktari toka nchini Sudan.
Ikumbukwe nchi ya Sudan ipo katika vita vya wenyewe kwa wenyenye. Mungu akawape utulivu, wepesi na waendelee vema na masomo yao katika Chuo cha Kikuu cha tiba Muhimbili.
---
Wanafunzi 150 wa udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Tiba, Sayansi na Teknolojia (UMST) cha Khartoum nchini Sudan wamehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ili kukamilisha mwaka wao wa mwisho wa masomo.
Akiongea wakati wa kuwakaribisha wanafunzi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi amesema kuwa hali ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchini Sudani imesababisha kufungwa kwa Vyuo na baadhi ya shughuli kusimama hivyo Wataalamu hao kushindwa kuendelea na ratiba yao ya masomo ya kawaida.
“Wanafunzi hawa wapo mwaka wa tano wa shahada ya kwanza ya utabibu, ambapo katika mwaka huo, mafunzo hufanyika kwa vitendo zaidi, hivyo Madaktari hawa Wanafujzi watafanya mzunguko (Rotation) katika idara mbalimbali ikiwemo idara ya upasuaji chini ya usimamizi wa Madaktari bingwa ili kuhakikisha wanapata maarifa yanayotakiwa”
Amesema kuwa MNH itatoa fursa kwa Wataalamu hao kujifunza kama ambavyo inatoa kwa Wataalamu wengine wa ndani na nje ya Nchi na hata baada ya kumaliza masomo kama watapenda kufanya mafunzo tarajali (Intenship) MNH itawapa nafasi hiyo.
Kwa upande wake Ruba Anwar Salih ambaye ni Kiongozi wa kundi la Wanafunzi hao amesema kuwa wamefurahi kupata fursa ya kuendelea na masomo katika Hospitali kubwa na yenye wataalamu wa kutosha, ni imani yao kwamba watapata fursa nzuri ya kujifunza.
Pia soma: Rwanda yapokea wanafunzi wa udaktari kutoka Sudan
Ikumbukwe nchi ya Sudan ipo katika vita vya wenyewe kwa wenyenye. Mungu akawape utulivu, wepesi na waendelee vema na masomo yao katika Chuo cha Kikuu cha tiba Muhimbili.
---
Wanafunzi 150 wa udaktari kutoka Chuo Kikuu cha Tiba, Sayansi na Teknolojia (UMST) cha Khartoum nchini Sudan wamehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ili kukamilisha mwaka wao wa mwisho wa masomo.
Akiongea wakati wa kuwakaribisha wanafunzi hao, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi amesema kuwa hali ya mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yanayoendelea nchini Sudani imesababisha kufungwa kwa Vyuo na baadhi ya shughuli kusimama hivyo Wataalamu hao kushindwa kuendelea na ratiba yao ya masomo ya kawaida.
“Wanafunzi hawa wapo mwaka wa tano wa shahada ya kwanza ya utabibu, ambapo katika mwaka huo, mafunzo hufanyika kwa vitendo zaidi, hivyo Madaktari hawa Wanafujzi watafanya mzunguko (Rotation) katika idara mbalimbali ikiwemo idara ya upasuaji chini ya usimamizi wa Madaktari bingwa ili kuhakikisha wanapata maarifa yanayotakiwa”
Amesema kuwa MNH itatoa fursa kwa Wataalamu hao kujifunza kama ambavyo inatoa kwa Wataalamu wengine wa ndani na nje ya Nchi na hata baada ya kumaliza masomo kama watapenda kufanya mafunzo tarajali (Intenship) MNH itawapa nafasi hiyo.
Kwa upande wake Ruba Anwar Salih ambaye ni Kiongozi wa kundi la Wanafunzi hao amesema kuwa wamefurahi kupata fursa ya kuendelea na masomo katika Hospitali kubwa na yenye wataalamu wa kutosha, ni imani yao kwamba watapata fursa nzuri ya kujifunza.
Pia soma: Rwanda yapokea wanafunzi wa udaktari kutoka Sudan