Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,926
- 31,169
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) katika Wilaya ya Arusha, kimepata pigo kubwa baada ya viongozi na wanachama wake 92 kuamua kujiunga na TLP.
Wanachama hao walipokelewa juzi katika ofisi za TLP Kata ya Sokoni katika hafla iliyohudhuriwa pia na viongozi wa vyama vya upinzani mkoani Arusha.
Wanaccm hao wa CCM wanatoka katika Kata ya Sokoni yenye idadi kubwa katika Manispaa ya Arusha na inayowakilishwa na Diwani wa TLP, Michael Kivuyo tangu mwaka 2000.
Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa kadi za TLP na kurejesha za CCM, viongozi hao na wanachama hao walisema wameamua kujiondoa katika chama hicho baada ya kuona kuwa viongozi wa CCM mkoani Arusha hawana dhamira ya kweli ya kuwasaidia wananchi.
Katibu Mwenezi wa CCM Tawi la Muriet, Salma Jumanne ambaye pia alikuwa katibu wa jumuiya ya wanawake wa CCM tawi hilo, alisema uamuzi wa kujiondoa CCM unalenga katika kutafuta chama mbadala ambacho viongozio wake watawasaidia wananchi.
Tumeona kwamba viongozi wa CCM mkoani Arusha, hawana mikakati bora ya maendeleo kwa wananchi, ni watu waliojawa na ubinafsi," alidai mwanachama mwingine.
Sourc:Mwananchi.
Huku Arusha bahati mbaya wakazi wake wengi hawana habari na CHADEMA.
Mpambano ni baina ya CCM na TLP.Kata ya Sokoni na Sombeti inawapiga kura wengi na mara zote ukitaka kushinda kiti cha ubunge Arusha ni kuhakikisha unashinda hizi kata mbili.
Tusisahau hakuna cha operesheni Sangara wa Zinduka wala hakuna kiongozi yoyote wa ngazi ya juu aliyehusika na zoezi la kuigaragaza CCM.Somo kubwa kwa wapinzani ni ushirikiano kwasababu kila chama kuna mahali kinakubalika zaidi ni vyema na busara kukubali na si kuparurana na kutoa nafasi kwa CCM kupita kwa urahisi.
Wanachama hao walipokelewa juzi katika ofisi za TLP Kata ya Sokoni katika hafla iliyohudhuriwa pia na viongozi wa vyama vya upinzani mkoani Arusha.
Wanaccm hao wa CCM wanatoka katika Kata ya Sokoni yenye idadi kubwa katika Manispaa ya Arusha na inayowakilishwa na Diwani wa TLP, Michael Kivuyo tangu mwaka 2000.
Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa kadi za TLP na kurejesha za CCM, viongozi hao na wanachama hao walisema wameamua kujiondoa katika chama hicho baada ya kuona kuwa viongozi wa CCM mkoani Arusha hawana dhamira ya kweli ya kuwasaidia wananchi.
Katibu Mwenezi wa CCM Tawi la Muriet, Salma Jumanne ambaye pia alikuwa katibu wa jumuiya ya wanawake wa CCM tawi hilo, alisema uamuzi wa kujiondoa CCM unalenga katika kutafuta chama mbadala ambacho viongozio wake watawasaidia wananchi.
Tumeona kwamba viongozi wa CCM mkoani Arusha, hawana mikakati bora ya maendeleo kwa wananchi, ni watu waliojawa na ubinafsi," alidai mwanachama mwingine.
Sourc:Mwananchi.
Huku Arusha bahati mbaya wakazi wake wengi hawana habari na CHADEMA.
Mpambano ni baina ya CCM na TLP.Kata ya Sokoni na Sombeti inawapiga kura wengi na mara zote ukitaka kushinda kiti cha ubunge Arusha ni kuhakikisha unashinda hizi kata mbili.
Tusisahau hakuna cha operesheni Sangara wa Zinduka wala hakuna kiongozi yoyote wa ngazi ya juu aliyehusika na zoezi la kuigaragaza CCM.Somo kubwa kwa wapinzani ni ushirikiano kwasababu kila chama kuna mahali kinakubalika zaidi ni vyema na busara kukubali na si kuparurana na kutoa nafasi kwa CCM kupita kwa urahisi.