Wana CCM na wana UKAWA tulieni tujenge Tanzania yetu

Khantwe

JF-Expert Member
Dec 20, 2012
59,410
119,115
Ni ukweli ulio wazi kuwa Dr. John Pombe Magufuli ndo raisi wa JMT...ni raisi wa watanzania na sio raisi wa CCM...whether tunampenda au hatumpendi yeye ndo rais...whether tulimchagua au hatukumchagua ila ndo ameshakuwa.

Hatuna budi kusahau maumivu na maisha yaendelee tujenge nchi yetu. Kinachonishangaza hawa wenzetu wa ccm ni kama wamejimilikisha rais,wanaona kama ni wa kwao wao ndio maana hawaishiwi mipasho,full kuzodoana hata kwenye mambo ya kawaida yanayohitaji majadiliano ya kawaida.... Wanamabadiliko tumekuwa kama wakimbizi nchi hii.

Huku mtaani hawaachi kuimba zile nyimbo zao za 'tumejipanga,mwaka huu wataisoma' Mmejipanga kwa lipi tena au mmepanga kutusomesha kwa lipi? Acheni hizo wadau.

Rais ili afanikishe mipango yake na ili atimize ilani ya chama chake anahitaji ushirikiano wa kila Mtanzania kwa nafasi yake...sasa mambo ya kuimbiana mipasho wakati uchaguzi umepita mnataka kutengeneza Tanzania ya namna gani? Mnataka tuendelee kugawanyika kwa misingi ya kisiasa wakati Tanzania yetu moja ili iweje? Msidharau 40% ni kubwa sana kama kundi hili la watu likiamua kuwanyima ushirikiano.

Majadiliano ya kwamba Magufuli anafaa au hafai kwa kipindi hiki mimi naona hayana tija maana kampeni zilishaisha na mtu ameshaapishwa....binafsi watu wanaonitumia vimeseji vya kumsifia au kumponda Magufuli nimewapiga stop... Huu sio muda wa kusifiana au kudongoana,mtu hajamaliza hata wiki tangu aapishwe,utendaji wake hatujauona hebu tuweni na subira then tuone utekelezaji wa yale aliyoyasema.

Ushauri wangu kwa wana-UKAWA naomba tuwe watulivu japo najua tuna maumivu ila tujitahidi kurudisha moyo nyuma na tuwape ushirikiano viongozi wetu waliochaguliwa.

Tuijenge Tanzania yetu, mabadiliko tunayotaka yanaweza kutokea hata chini ya viongozi hawahawa japo mfumo wao umeoza ila hatuwezi kusubiria miaka mingine mitano tukingoja mabadiliko. Mabadiliko yanaweza yasitokee kwa kiwango kile tunachotaka sisi ila ni lazima tuhakikishe walau tunasogea hatua kadhaa.

Mimi yangu ni hayo tu na huo ni ushauri wangu kwa watanzania wenzangu. Ukiona nimeandika pumba au post hii haijafikia kiwango chako pita kimyakimya.
 
Ni ukweli ulio wazi kuwa Dr. John Pombe Magufuli ndo raisi wa JMT...ni raisi wa watanzania na sio raisi wa CCM...whether tunampenda au hatumpendi yeye ndo rais...whether tulimchagua au hatukumchagua ila ndo ameshakuwa...hatuna budi kusahau maumivu na maisha yaendelee tujenge nchi yetu. Kinachonishangaza hawa wenzetu wa ccm ni kama wamejimilikisha rais,wanaona kama ni wa kwao wao ndio maana hawaishiwi mipasho,full kuzodoana hata kwenye mambo ya kawaida yanayohitaji majadiliano ya kawaida.... Wanamabadiliko tumekuwa kama wakimbizi nchi hii..
Huku mtaani hawaachi kuimba zile nyimbo zao za 'tumejipanga,mwaka huu wataisoma' Mmejipanga kwa lipi tena au mmepanga kutusomesha kwa lipi? Acheni hizo wadau..... Rais ili afanikishe mipango yake na ili atimize ilani ya chama chake anahitaji ushirikiano wa kila Mtanzania kwa nafasi yake...sasa mambo ya kuimbiana mipasho wakati uchaguzi umepita mnataka kutengeneza Tanzania ya namna gani? Mnataka tuendelee kugawanyika kwa misingi ya kisiasa wakati Tanzania yetu moja ili iweje? Msidharau 40% ni kubwa sana kama kundi hili la watu likiamua kuwanyima ushirikiano.
Majadiliano ya kwamba Magufuli anafaa au hafai kwa kipindi hiki mimi naona hayana tija maana kampeni zilishaisha na mtu ameshaapishwa....binafsi watu wanaonitumia vimeseji vya kumsifia au kumponda Magufuli nimewapiga stop... Huu sio muda wa kusifiana au kudongoana,mtu hajamaliza hata wiki tangu aapishwe,utendaji wake hatujauona hebu tuweni na subira then tuone utekelezaji wa yale aliyoyasema.
Ushauri wangu kwa wana-UKAWA naomba tuwe watulivu japo najua tuna maumivu ila tujitahidi kurudisha moyo nyuma na tuwape ushirikiano viongozi wetu waliochaguliwa..... Tuijenge Tanzania yetu,mabadiliko tunayotaka yanaweza kutokea hata chini ya viongozi hawahawa....japo mfumo wao umeoza ila hatuwezi kusubiria miaka mingine mitano tukingoja mabadiliko....mabadiliko yanaweza yasitokee kwa kiwango kile tunachotaka sisi ila ni lazima tuhakikishe walau tunasogea hatua kadhaa.
Mimi yangu ni hayo tu...na huo ni ushauri wangu kwa watanzania wenzangu. Ukiona nimeandika pumba au post hii haijafikia kiwango chako pita kimyakimya.
Mkuu wapiga Kura wengi wa ccm ni wanawake tena wengi wao ni mama wa nyumbani huko uswahilini manzese,kigogo,tandale,tandika wao zaidi ya uswahili they know nothing more
 
Mkuu wapiga Kura wengi wa ccm ni wanawake tena wengi wao ni mama wa nyumbani huko uswahilini manzese,kigogo,tandale,tandika wao zaidi ya uswahili they know nothing more

Ni tabu sana...kwamba uchaguzi umeisha tunatakiwa tujenge nchi wao hawana habari
 
Mimi mwana ukawa, siwezi tulia, roho bado inanikereketa kwa yaliyotokea, bado nina hasira na ma ccm.
 
Mimi mwana ukawa, siwezi tulia, roho bado inanikereketa kwa yaliyotokea, bado nina hasira na ma ccm.

Kadri unavyopata hasira ndivyo unavyozidi kuumia....ukizingatia kuwa hakuna unachoweza kubadilisha
 
Kadri unavyopata hasira ndivyo unavyozidi kuumia....ukizingatia kuwa hakuna unachoweza kubadilisha

Acha niendelee kuumia hata kwa miaka 27 kama Mandela kwani naamini ipo siku ya ukombozi wa kweli toka kwa kaburu ccm.
 
Mi naona wanamabadiliko ni watu wenye hekima ya Mungu kabisa.Yaani pamoja na hoja ya uchakachuaji wamekaa kimya bila vurugu! Hawa mataarabu wa ccm sijui wamekula miwashawasha hawa! Eti umejipanga,wataisoma, huna kazi unaimbia watu wataisoma wakati wewe ndiyo unaisoma number.Isee hii kali kweli.
 
Munao toa sifa Kwa rais Kwa wiki moja ya ikulu wakati hats serikali haijaundwa ,mnanisikitisha sana ,hebu mpeni nafasi afanye kwanza hivyo mnaalika watu WA kumcrash Kwa kila ambalo watakuwa hawakubaliani nalo wao kama mwanakijiji alivyokuwa against serikali ya Kikwete na Lowasa,halafu hizi Mrema type leadership measure's ndiyo zitammaliza mapemaaa,nasubiri kuona mengi kama safari iliyopita,Rais alianzia kwenye Masoko akaenda Ngurudoto iliyobaki ni historia sikumbuki zaidi
 
Kwa sasa tuwe kitu kimoja hadi wakati wa uchaguzi ujao. Kwa kipindi hiki tuungane tuitoe nchi kwenye mkwamo. Rais Magufuli sio mbaya ni mtu ambaye atatufisha pazuri sana japo kweli mfumo japokuwa ni kweli maumivi kuisha itachukua muda lakini tuvumilie
 
Naomba wanaccm wote wavumilie furaha yao maana hali ilikuwa mbaya kweli sasa unachomokea kwenye tundu la sindano kweli lazima upagawe kwa eneo hilo wanapaswa. But u need to avoid excessive happness ili usipate matatizo mengine. Upo uwezekano ukumchagu au ulimchagua lakini kwa sasa ndiye na kama ndivyo apewe ushirikiano. Kipimo cha kwanza ni siku mia moja za utawala wake kwa sasa mimi binafsi siwezi kusema juu ya utendaji wake TUSUBIRi
 
Back
Top Bottom