Waliokuwa Watumishi Feki 13,000 walipwa Bilioni 35 na NSSF

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,115
49,836
Nssf imesema imewalipa Watumishi Feki zaidi ya 13,000 takribani Bilioni 35 kama Rais Samia alivyoagiza.

Ikumbukwe hao walioitwa Watumishi Feki walifukuzwa utumishi na Marehemu Magufuli Kwa visingizio vya kukosa vyeti bila ya kulipwa hata senti Moja.

My Take
Mpaka hapa Rais Samia ana mtaji wa kura 13*000 kutoka Kwa Watumishi Feki.

---

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi za Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Hosea Kashimba amesema, wametumia zaidi ya Sh35 bilioni mpaka sasa kuwalipa waliokuwa watumishi wa umma 13,000 waliobainika kuwa na vyeti feki.

Kishimba amesema hayo leo Alhamisi, Agosti 31, 2023 jijini Dar es Salaam katika kikao kazi baina ya mfuko huo na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.

"Hatuna madai ya watumishi wa vyeti feki, pengine ambao bado labda hawajui au walirudi kijijini, lakini wakija wanalipwa haraka kwani tumeweka dawati maalum," amesema Kishimba na kuongeza:

"Tunataka huruma ya mheshimiwa Rais aliyoitoa wanaipata kwa wakati na tumejipanga vyema."

Kishimba amesema baada ya tangazo,"kutoka kuwa una cheti feki wengine walikimbia, sasa baada ya tangazo la kuanza kutoa mafao wanakuja na wakija tunafuatilia utumishi, tukiona michango yao tunawapa mafao."

Mwaka 2022, Rais Samia Suluhu Hassan alitaka watumishi hao waliobainika kuwa na vyeti feki na kuondolewa katika utumishi wa umma walipwe mafao yao.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma
IMG-20221026-WA0046-755x1024.jpg
 
Nssf imesema imewalipa Watumishi Feki zaidi ya 13,000 takribani Bilioni 35 kama Rais Samia alivyoagiza.

Ikumbukwe hao walioitwa Watumishi Feki walifukuzwa utumishi na Marehemu Magufuli Kwa visingizio vya kukosa vyeti bila ya kulipwa hata senti Moja.

My Take
Mpaka hapa Rais Samia ana mtaji wa kura 13*000 kutoka Kwa Watumishi Feki.
Kwani si ni haki yao Kulipwa?
Na walikatwa 5% Percent kila mwezi kwenye mishahara yao...i
Hivyo kulipwa kwao sio Hisani ni Haki yao...
 
Nssf imesema imewalipa Watumishi Feki zaidi ya 13,000 takribani Bilioni 35 kama Rais Samia alivyoagiza.

Ikumbukwe hao walioitwa Watumishi Feki walifukuzwa utumishi na Marehemu Magufuli Kwa visingizio vya kukosa vyeti bila ya kulipwa hata senti Moja.

My Take
Mpaka hapa Rais Samia ana mtaji wa kura 13*000 kutoka Kwa Watumishi Feki.

---

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi za Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Hosea Kashimba amesema, wametumia zaidi ya Sh35 bilioni mpaka sasa kuwalipa waliokuwa watumishi wa umma 13,000 waliobainika kuwa na vyeti feki.

Kishimba amesema hayo leo Alhamisi, Agosti 31, 2023 jijini Dar es Salaam katika kikao kazi baina ya mfuko huo na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.

"Hatuna madai ya watumishi wa vyeti feki, pengine ambao bado labda hawajui au walirudi kijijini, lakini wakija wanalipwa haraka kwani tumeweka dawati maalum," amesema Kishimba na kuongeza:

"Tunataka huruma ya mheshimiwa Rais aliyoitoa wanaipata kwa wakati na tumejipanga vyema."

Kishimba amesema baada ya tangazo,"kutoka kuwa una cheti feki wengine walikimbia, sasa baada ya tangazo la kuanza kutoa mafao wanakuja na wakija tunafuatilia utumishi, tukiona michango yao tunawapa mafao."

Mwaka 2022, Rais Samia Suluhu Hassan alitaka watumishi hao waliobainika kuwa na vyeti feki na kuondolewa katika utumishi wa umma walipwe mafao yao.

Chanzo: Mwananchi
Kibwengo mkuu ukimchunguza na yeye anacheti fek indo maana anawabeba wenzake pumbafu zake
 
Kwani si ni haki yao Kulipwa?
Na walikatwa 5% Percent kila mwezi kwenye mishahara yao...i
Hivyo kulipwa kwao sio Hisani ni Haki yao...
Hata mwizi ana haki? umeingia kazini kwa njia haramu, hata kama alifanya kazi halali, lakini bado hawakustahili kuwepo ofisini, wapo wenye sifa waliokosa nafasi kwa kuzuiwa na hao matapeli, hao walitakiwa kuwa magereza badala ya kulipwa..
 
Hata mwizi ana haki? umeingia kazini kwa njia haramu, hata kama alifanya kazi halali, lakini bado hawakustahili kuwepo ofisini, wapo wenye sifa waliokosa nafasi kwa kuzuiwa na hao matapeli, hao walitakiwa kuwa magereza badala ya kulipwa..
Hao wenye sifa walishindwa kwenye usaili na sio kazi ya wenye vyeti fake kuthibitisha vyeti vyao kabla ya Kupewa kazi.

Ukishampa kazi na akawa anafanya vyema since then harafu uje kusema ana Cheti fake wewe ni mbumbumbu tuu

Mwisho standard 7 sio vyeti fake,Hawa wote walitimuliwa na Mwendazake Kwa sababu hakuwa na pesa za Kuendesha Nchi ndio maana hata Baada ya kuwatimua alishindwa Kuajiri replacement pia.
 
Back
Top Bottom