Mlendamboga
JF-Expert Member
- Sep 14, 2011
- 664
- 334
Wahitimu wa kidato cha sita waliochelewa kuripoti kambini tarehe 11/6/2023 wamezuiwa kuripoti na kuungana na wenzao. Zaidi ya vijana 150 katika kambi ya JKT Mafinga wamerejeshwa wakati wakiripoti jana 12/6/2023 siku moja baada ya tarehe ya mwisho.
Kwa wale waliofika jana jioni walipewa hifadhi mpaka asubuhi kwaajili ya usalama wao na leo asubuhi wametakiwa kurejea kwao. Nidhamu ya jeshi ni msingi wa jeshi imara! walidhani ni kule sekondari mtu anavuta wiki mbili mbele baada ya shule kufunguliwa.
Wazazi kama mwanao alienda JKT tarehe 12/6 wasiliana naye ama mtumie nauli yupo nje anapunga upepo!
Kwa wale waliofika jana jioni walipewa hifadhi mpaka asubuhi kwaajili ya usalama wao na leo asubuhi wametakiwa kurejea kwao. Nidhamu ya jeshi ni msingi wa jeshi imara! walidhani ni kule sekondari mtu anavuta wiki mbili mbele baada ya shule kufunguliwa.
Wazazi kama mwanao alienda JKT tarehe 12/6 wasiliana naye ama mtumie nauli yupo nje anapunga upepo!