Walimu walipwa fedha zao dirishani!

Ibrah

JF-Expert Member
Mar 22, 2007
2,729
528
Wadau, tunajua kuwa serikali imeanza kuwalipa Waalimu madai yao ya muda mrefu. Jana nimepata habari ya kushtua na kushangaza sana kuwa Walimu wanalipwa pesa zao cash kwa kupanga foleni dirishani kwa karani wa fedha!

Maoni yangu:
Hii ni kinyume na kanuni na taratibu za utoaji fedha kwa watumishi wa Serikali, mbona mishahara wanelipwa kupitia benki kulikoni madai haya? Kunani? Je walimu ambao wapo safarini au likizo za ugonjwa itakuwaje? Nimeambiwa kuwa hairuhusiwi Mwalimu kuchukuliwa pesa na mtu yoyote (whic is good). Lakini ikiwa Mwalimu akirudi baada ya likizo ya ugonjwa na kukuta zoezi limepiata itakuwahe? Maana tunajua katika Idara zote za Serikali hakuana Idara zinazoongiza kwa wizi na ufujaji wapesa kama Halmashauri za Miji ambazo ndizo zinawalipa Waalimu.

Nionavyo mimi hii ni loop hole nyingine ya Waalimu kuibiwa maana Mwalimu hana namna ya kuja stahili zake maana analipwa taslimu na akitaka kudai haki zake baadaye atatumia vigezo gani? Maana kama kuna mapunjo na amelipwa kwa hundi anaweza kuwa na kumbukumbu na ushahidi wa kuthibitisha kuwa amepunjwa kwa kutoa photocopy ya hundi ambayo kwayio alilipwa stahili zake.
 
1-Ibrah nafikiri unapolipwa dirishani haimaanishi RISITI au Kumbukumbu yoyote hupewi...Kama hawatoi kumbukumbu hapo itakuwa tatizo.

2- Kama ulivyosikia kuwa Hakuna Mjumbe kutumwa, kila mwalim lazima achukue mwenyewe, that means ambaye hajapata HAKI yake even after some months itakuwepo.....Kama forgery siwezi comment..maana hata Bank zinafanya Forgeries...like EPA etc..

3. Labda wale ambao wanaumwa na ambao wanahitaji Fungu hilo liwasaidie hapo nafikiri Njia ingine inaweza tumika....pia siwezi comment kwasasa!!!

4. Wale waalim ambao Majina yao Hayapo, Wahusika tunaomba muyaingize majina yao haraka ktk registers zenu ili wapewe HAKI zao...
 
Chuma, hivi ni kweli utaratibu wa malipo serikalini ndiyo ulivyo? Nakumbuka mwaka 2003 Serikali ilifuta utaratibu wa kupokelea pesa dirishani na Wafanyakazo wote wakaamriwa wafungue akaunti benki (NMB).
 
Back
Top Bottom