Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Kila mtu sasa anashangilia kuwa CCM inajisafisha kwa kuwatema watuhumiwa wote wa ufisadi, miezi michache iliyopita tuliambiwa kuwa CCM ni chama kinachofuata utawala wa sheria kwamba kisingewaacha makada wake waliokuwa na tuhuma za ufisadi kwa kuwa tuhuma hizo zilikuwa hazijathibitishwa na kila mtu alishangilia (akiwemo Chiligati, Makamba, na wengine wengi), leo hii hao hao ambao sisi tulikuwa tunawaona hawafai kupewa fursa ya kuendelea kuwa viongozi kwa sababu ya tuhuma hizo wanaanza kuenguliwa na tunaambiwa kuwa huu ni mkakati wa chama kujisafisha...
Binafsi siamini kuwa kuna utashi wa kweli kuwawajibisha makada wote wa CCM wanaotuhumiwa na ufisadi bali ni janja ya nyani kuendelea kula mahindi yetu. CCM ndicho kilicho madarakani, kina dola, kina vyombo vya uchunguzi na hakikuonyesha dalili za kulishughulikia tatizo la ufisadi tangia 2006 pale tuhuma nyingi zilipoanza kuzagaa kuwa tunaliwa, uchunguzi wa Kagoda bado unaendelea na haieleweki utaisha lini.. kila mtu aliambiwa kuwa hawa walirejesha sehemu ya hela waliyokuwa wamechukua na wakasamehewa (bila hata kufikishwa mahakamani tukaujua ukweli) na bado serikali bado inafanya uchunguzi sijui ni nini ambacho wanachunguza....
Natoa wito kwa watanzania wote wapenda haki wasidanganyike na uhuni huu wa CCM bali tukaze kamba kelele tunazopiga sasa zinaanza kuwatia hofu tusipumuzike mpaka pale tutakapo wafikisha mahakamani wale wote wanajulikana kama untouchables, tuwa Housin Mubaraka hawa wahuni
Binafsi siamini kuwa kuna utashi wa kweli kuwawajibisha makada wote wa CCM wanaotuhumiwa na ufisadi bali ni janja ya nyani kuendelea kula mahindi yetu. CCM ndicho kilicho madarakani, kina dola, kina vyombo vya uchunguzi na hakikuonyesha dalili za kulishughulikia tatizo la ufisadi tangia 2006 pale tuhuma nyingi zilipoanza kuzagaa kuwa tunaliwa, uchunguzi wa Kagoda bado unaendelea na haieleweki utaisha lini.. kila mtu aliambiwa kuwa hawa walirejesha sehemu ya hela waliyokuwa wamechukua na wakasamehewa (bila hata kufikishwa mahakamani tukaujua ukweli) na bado serikali bado inafanya uchunguzi sijui ni nini ambacho wanachunguza....
Natoa wito kwa watanzania wote wapenda haki wasidanganyike na uhuni huu wa CCM bali tukaze kamba kelele tunazopiga sasa zinaanza kuwatia hofu tusipumuzike mpaka pale tutakapo wafikisha mahakamani wale wote wanajulikana kama untouchables, tuwa Housin Mubaraka hawa wahuni