ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Dunia bado inakua, leo nimeamini!
Nikiwa ktk matembezi yangu, wiki jana, maeneo ya chang'ombe hapa dodoma nikakuta mkusanyiko wa watu nje ya nyumba moja ya kupanga. Kama kawaida ya watu wenye tabia kama yangu ya nyatunyatu, nikasogea walau nipate cha kujifunza. Baada ya kuwauliza nilowakuta, kulikoni wanawake wanagombana, nkaambiwa huo ni ugomvi kati ya mke na mama mkwe wake. Kisa? Wanagombea kitovu cha mtoto kilichoanguka jioni ile. Mama mkwe anakitaka ili akakifanyie utaratibu kadiri ya mila zao, ili hali mama wa kachanga hako naye alikuwa anakitaka kitovu cha mwanawe iili akakitunze kadiri ya mila zao. Hapo ndo mgogoro ulipojikita. Ulikuwa ni mtiti wa kufa mtu kwani kwa yeyote alokuwa akipita karibu angeshawishika kutaka kujua kinachoendelea.
Niwaulize wanajf, hivi kwa karne hii ya 21, issue ya kitovu inaweza ikawa na msaada gani ktk kujiletea maendeleo? Kuna ubaya gani mtu anaoweza kuupata kutokana na 'mismanagement' ya kitovu chake cha utotoni? Ktk maisha yetu haya ya 'kiswahili swahili' nmepatwa na mashaka na natamani hata kumuuliza mamsapu wangu vilipo vitovu vya wanangu, nshaingiwa na woga mie kutokana na hili tukio!
Hebu walimwengu nijuzeni kuhusu umuhimu wa hivi vitovu vya watoto ktk makuzi yao na maisha yao ya baadae, nimeogopa kweli.
Nisaidieni nijue ukweli na umuhimu wa kuwa na hivyo vitovu vya watoto vinavokatika/dondoka wiki chache baada ya kuzaliwa! Upssssssssssssssssss!
Nikiwa ktk matembezi yangu, wiki jana, maeneo ya chang'ombe hapa dodoma nikakuta mkusanyiko wa watu nje ya nyumba moja ya kupanga. Kama kawaida ya watu wenye tabia kama yangu ya nyatunyatu, nikasogea walau nipate cha kujifunza. Baada ya kuwauliza nilowakuta, kulikoni wanawake wanagombana, nkaambiwa huo ni ugomvi kati ya mke na mama mkwe wake. Kisa? Wanagombea kitovu cha mtoto kilichoanguka jioni ile. Mama mkwe anakitaka ili akakifanyie utaratibu kadiri ya mila zao, ili hali mama wa kachanga hako naye alikuwa anakitaka kitovu cha mwanawe iili akakitunze kadiri ya mila zao. Hapo ndo mgogoro ulipojikita. Ulikuwa ni mtiti wa kufa mtu kwani kwa yeyote alokuwa akipita karibu angeshawishika kutaka kujua kinachoendelea.
Niwaulize wanajf, hivi kwa karne hii ya 21, issue ya kitovu inaweza ikawa na msaada gani ktk kujiletea maendeleo? Kuna ubaya gani mtu anaoweza kuupata kutokana na 'mismanagement' ya kitovu chake cha utotoni? Ktk maisha yetu haya ya 'kiswahili swahili' nmepatwa na mashaka na natamani hata kumuuliza mamsapu wangu vilipo vitovu vya wanangu, nshaingiwa na woga mie kutokana na hili tukio!
Hebu walimwengu nijuzeni kuhusu umuhimu wa hivi vitovu vya watoto ktk makuzi yao na maisha yao ya baadae, nimeogopa kweli.
Nisaidieni nijue ukweli na umuhimu wa kuwa na hivyo vitovu vya watoto vinavokatika/dondoka wiki chache baada ya kuzaliwa! Upssssssssssssssssss!