Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,902
- 4,626
.Wanefili ni nani? wanefili maana yake ni majitu makubwa, hawa majitu kama Goliathi, Ahimani, sheshai, Talmai, Safu, Lahmi nk walijulikana katika agano la kale.
Hawa walikuwa ni wanadamu waliozaliwa kutokana na mahusiano ya kimapenzi kati ya wana wa Mungu na binadamu, wana wa mungu hawa walikuwa ni malaika walioanguka(mapepo) ambao walioa wanawake binadamu waliwapata kwa nguvu za giza za mapepo hayo uhusiano huu ulisababisha kuzaliwa watoto Wanefili (MAJITU MAKUBWA) mwanzo 6:4.
Wanefili walikuwa kizazi kikubwa sana cha mashujaa maarufu ambao walifanya vitendo vya uovu mkubwa sana. Ukubwa na nguvu zao ulitokana na mchanganyiko wa chembe za damu ya mapepo na binadamu.
Hata hivyo kizazi hichi kiliangamizwa na gharika wakati wa NABII NUHU
View attachment 411514View attachment 413488 View attachment 413489 View attachment 413491
Katika uzao wa Adamu kuna mwendelezo wa uzao wa mwanamke na wa nyoka. Hata Bwana Yesu alikua akirifaa kwa kuwaambia baadhi ya watu "...enyi uzao wa nyoka..."
Hawa alidanganywa na kuangushwa na nyoka na baada ya jambo hili tuliona hawa akiwa na ujauzito na ni kipindi yeye pamoja na Adamu walifukuzwa paradiso.
Siri iliyopo hapa ni kwamba nyoka baada ya lile tukio la Edeni alibadilishwa maumbile.
Hivyo basi manafeli ni watoto waliotokana na kuona kati ya uzao wa Seti na kaini.