Wadau wapinga Rais Samia na Makamu wake kuingia na Viti binafsi Kanisani, yadaiwa ni kujikweza

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
119,024
221,637
Kwenye Ibada Maalum ya kumbukumbu ya miaka 23 ya kifo cha Mwalimu Nyerere, iliyofanyika huko Mkoani Kagera, Viongozi kadhaa wa Kitaifa wamehudhuria, akiwemo Mh Rais Samia Suluhu na Makamu wake, Dr Philipo Mpango , Tunawapongeza kwa jambo hilo.

Sitaki kurudia yaliyotokea ili nisiwachoshe, lakini Kitendo cha Rais na Makamu wake kuingia na Viti vyao vya enzi ndani ya kanisa kimepingwa na wadau wengi, huku wakitahadharisha viongozi kuacha kujiona ni wa kipekee, ukweli ni kwamba HAWANA UPEKEE WOWOTE, ukiachilia mbali vyeo walivyo navyo hawana tofauti yoyote nyingine na sisi wengine.

Kitendo cha kuingia na Masofa yao Kanisani ni DHARAU KWA WAUMINI na Kanisa kwa ujumla, na kinapaswa kukemewa ili kisirudiwe tena, kama hawataki kukaa kwenye mabenchi ya kanisa, basi wasiingie kwenye Makanisa, waishie nje na hotuba zao.

Ziko Picha kadhaa zikiwaonyesha Joe Biden wa Marekani na Haikainde Hichilema wa Zambia wakiwa wameheshimu madhabau na kukalia Mabenchi ya kanisa, mbona walishiriki ibada na wakamaliza kwa amani tu, hawa viongozi wetu wana upekee gani hawa?

JamiiForums50470737_680x454.jpg


Angalizo: Sina chuki yoyote na viongozi hawa.
 
Wewe hupaswi kuwalaumu hao viongozi moja kwa moja.

Erythrocyte!
Umeandika as if walikuja wamebeba viti vyao,wakati ukweli ni kwamba kama ni kasoro imetokea.na kama ni kulaumiwa ni hao waliokuwa na jukumu la maandalizi na sidhani kama ni maagizo ya Mheshimiwa Rais wala Makamu wake.

Wao wameingia na kuelekezwa mahali walipoandaliwa kukaa.

Baadhi ya vitu sio lazima uvipinge kwa sababu havina tija kwa maendeleo chanya wala havitowi fundisho lolote kwa jamii.

Pia kuwa pingapinga sio alama ya elimu bali ni dalili za ubishi usio na tija pia.

Rais akipanda basi mnasema kadharauliwa,je kipi afanye ili awafurahishe?

Mtaendeleza bifu la kukaa benchi mpaka 2025?

Si mtafika mmechoka Sana?

Mnyonge mnyongeni ila haki yake apewe.
 
Wewe hupaswi kuwalaumu gao viongozi moja kwa moja.

Umeandika as if walikuja wamebeba viti vyao,wakati ukweli ni kwamba kama ni kasoro imetokea.Wa kulaumiwa ni hao waliokuwa na jukumu la maandalizi na sidhani kama ni maagizo ya Mheshimiwa Rais wala Makamu wake.

Baadhi ya vitu sio lazima uvipinge kwa sababu havina tija kwa maendeleo chanya wala havitowi fundisho lolote kwa jamii.
Rais akipanda basi mnasema kadharauliwa,je kipi afanye ili awafurahishe?

Mnyonge mnyongeni ila haki yake apewe.
Vinatoa fundisho kubwa sana.
Fuatilia viongozi wanaopenda kujitofautisha wawapo katikati ya umati, utajua kuwa kuna tofauti na wale wanaojichanganya.

Baba wa taifa alikuwa anakaa kijiwe cha kahawa na wananchi. JPM, alitumia viti vya kawaida.

Fuatilia kama mama kuna picha amekaa na wananchi wa kawaida na akawa comfortable! Yeye na JK. ni wa 'kishua' zaidi!😀🙌
 
Mkuu mimi nakuunga mkono siku zote ila kwa hili sidhani kama inabidi liwe ishu sana, hajawahi kufanya hivyo kabla so inawezekana kuna harufu sio nzuri wat wa Usalama wamenusa, hiyo ni kazi yao, tuache wenye kazi yao waifanye, likitokea la kutokea ni sisi hao hao tutakaosema National Security ni wazembe, CCM ya leo sio ile ya Mwalimu Nyerere.
 
Vinatoa fundisho kubwa sana.
Fuatilia viongozi wanaopenda kujitofautisha wawapo katikati ya umati, utajua kuwa kuna tofauti na wale wanaojichanganya.

Baba wa taifa alikuwa anakaa kijiwe cha kahawa na wananchi. JPM, alitumia viti vya kawaida.

Fuatilia kama mama kuna picha amekaa na wananchi wa kawaida na akawa comfortable! Yeye na JK. ni wa 'kishua' zaidi!😀🙌
Unakaa nao ili iweje??
 
Usifananishe madhabahu na vitu vya kipumbavu.
Hao ni marais wa nchi kuna suala zima la ulinzi. Vipi kama viti vya hapo hapo kanisani vikawekewa mabomu na yakawamaliza? Huoni kama huo ni uzembe wa ulinzi.

Hii amani inatudanganya sana, tunashindwa kufikiria kwa kina.
 
Vinatoa fundisho kubwa sana.
Fuatilia viongozi wanaopenda kujitofautisha wawapo katikati ya umati, utajua kuwa kuna tofauti na wale wanaojichanganya.

Baba wa taifa alikuwa anakaa kijiwe cha kahawa na wananchi. JPM, alitumia viti vya kawaida.

Fuatilia kama mama kuna picha amekaa na wananchi wa kawaida na akawa comfortable! Yeye na JK. ni wa 'kishua' zaidi!
Narudia kusema kwamba hivyo viti wamevikuta tayari vimewekwa na wao wamefanya kufuata maelekezo ya wapi pa kukaa.

Hatujaona mahali pakionyeshwa wao kugoma kukalia bench na kuagizwa waletewe hivyo viti.

Rais huwa hapangi bali hipangiwa na kanati maalum ya maandalizi,chini ya kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa husika kwa ushirikiano na TISS.

Tumieni ubongo kufikiri vema bafala ya kuutumia ku-bet mchana kutwa galafu mkija JFmnakuwa hoi.
 
Back
Top Bottom