Naby Keita
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,716
- 15,277
Tecno ya kuzidi laki 2 bora niende brand ya kueleweka
Mleta mada analipwa kwa Mwezi,ni mwajiriwa wa Techno.Mtoa mada umelipwa bei gani?
Sio unasikia bali kuwa muwazi kwamba wewe ni mfanyakazi wa techno upo hapa kwa ajili ya sales promotion kwa brand yenu mpya,hii pia itasaidia watu kukuamini hiki unachotangaza na pia kujibu maswali ya watu na kuondoa hofu yao juu ya simu hizi za Techno.Wanazo mbili, hii Phantom 6 na 6+ hii ya 6+ ndio naskia ina MP21.
Eti wanasema ukiagiza Phantom6 yenye ukubwa wa ROM 32GB,RAM 3GB,kamera mbili za nyuma zenye 13MP na 5MP,muonekano wa kuvutia pamoja na uwezo wake wa ajabu wa kuingiza chaji kwa haraka unapewa mizawadi kibao.
Bei ya kuagiza yaani Pre-Order ni 50,000/= (Elfu hamsini) Halafu baadaye unamalizia kiasi kitakachokuwa kimebaki, unapewa zawadi na simu yako.
Kilichonivutia zaidi ni kwamba na Mshkaji Alikiba atakuwepo na mtu anayeagiza hiyo Phantom6 yao anapiga nae picha.
Mi nimeona kwenye mtandao wao tu na wanasema hii itafanyika kuanzia saa 8 kamili mchana kwenye viwanja vya City Mall Posta Dar siku ya jumamosi ya tarehe 8 Oktoba 2016.
new member rudi fb unawajua tecno au una wapigia ki tanzaniaTecno sio simu yakuweza kushindana na samsung iPhone lg kwakifupi haina soko dunian
si kuwajua tu nmeshatumia sananew member rudi fb unawajua tecno au una wapigia ki tanzania
Tecno sio simu wewe bali midoli ya watoto.new member rudi fb unawajua tecno au una wapigia ki tanzania
Kwasabu mi napenda simu za Tecno huwa ni mfuatiliaji sana na mara nyingi hata kama mtu simu ya Tecno inamsumbua, naweza kumwelekeza. Kwa ufupi sifanyi kazi Tecno ila napenda sana Tecno na nafahamu mambo mengi kuhusu Tecno. Wazo lako ni zuri sana Frank Wanjiru, nashukuru aise, ila ukitaka kuuliza we niulize.Sio unasikia bali kuwa muwazi kwamba wewe ni mfanyakazi wa techno upo hapa kwa ajili ya sales promotion kwa brand yenu mpya,hii pia itasaidia watu kukuamini hiki unachotangaza na pia kujibu maswali ya watu na kuondoa hofu yao juu ya simu hizi za Techno.
Midoli ya watoto kwako, ila kwa mimi ninaetumia Tecno, ni simu bomba sana.Tecno sio simu wewe bali midoli ya watoto.
Wabongo acheni hizo, mi kuwashirikisha fursa hii tu nimekosea? Ndio maana madili yakitokea watu huwa wananyamaza. Mi nimekuwa mfuatiliaji wa karibu wa simu za Tecno, kama unahitaji kuuliza we niulize kwani kuna wakati huwa hata narekebisha settings.Mleta mada analipwa kwa Mwezi,ni mwajiriwa wa Techno.
Ukijaribu kutumia Tecno ya zaidi ya laki mbili ndio utaamini ubora wake, ukitaka kitu rahisi utapata kisicho na ubora mi nilinunua Tecno Camon C9, ndio ninayotumia sahivi ni simu moja ninayoipenda sana! Usinunue za laki laki.Tecno ya kuzidi laki 2 bora niende brand ya kueleweka
Tatizo watu huwa hamuelewi simu ambayo sio mchina labda ni iPhone, zote ni mchina, sasa nikuulize wewe unatumia simu gani?Du!!! Kuna watu bado mnatumia mchina w tecno n uyo mshikaji wako nae anaitumia iyo tecno kweli JPM kabana.
Samsung,Nokia,Motorola na Blackberry kumbe ni kampuni za Kichina?asante mfanyakazi wa techno kwa kutuambia Siri hii.Tatizo watu huwa hamuelewi simu ambayo sio mchina labda ni iPhone, zote ni mchina, sasa nikuulize wewe unatumia simu gani?
Kama mtu kweli una matumizi hasa ya smartphone mbali ya kupiga na kupigiwa simu na kutuma SMS techno sio simu ya kutumia.Ukijaribu kutumia Tecno ya zaidi ya laki mbili ndio utaamini ubora wake, ukitaka kitu rahisi utapata kisicho na ubora mi nilinunua Tecno Camon C9, ndio ninayotumia sahivi ni simu moja ninayoipenda sana! Usinunue za laki laki.
Huyo mjinga mwambie haujamlazimisha kununuaMi nimewashirkisha wanaopenda, we kama hupendi basi nyamaza, usitukane.
Mkuu mbona unatumia nguvu nyingi kuwaelewesha watu wanaokariri brandTatizo watu huwa hamuelewi simu ambayo sio mchina labda ni iPhone, zote ni mchina, sasa nikuulize wewe unatumia simu gani?
Ndiyo kwani uongo?Mbona hata ukifungua imeandikwa Made in China, tatizo lako moja, sio kila bidhaa kutoka China ni mbaya, elewa bro.Samsung,Nokia,Motorola na Blackberry kumbe ni kampuni za Kichina?asante mfanyakazi wa techno kwa kutuambia Siri hii.
Hayo ni maoni yako mbona watu tunatunmia hadi kutumiana madocument makubwa, lakini hata hazisumbui, tatizo inawezekana either hujui kutumia smartphone au unayo ya laki.Kama mtu kweli una matumizi hasa ya smartphone mbali ya kupiga na kupigiwa simu na kutuma SMS techno sio simu ya kutumia.