BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Wachina wampuuza Magufuli ujenzi barabara ya Mbagala Wednesday, 18 May 2011 20:12
Dk John Magufuli
Ummy Muya
Mwananchi
KAMPUNI ya Chico ambayo ilishinda zabuni ya kujenga barabara ya Zakhiem hadi Tanita, imeshindwa kutekeleza agizo la Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, kutaka iwe imeanza kazi ndani ya siku kumi.
Mei 7, mwaka huu, Waziri Magufuli alitoa siku kumi kwa kampuni hiyo iwe imeanza kazi, vinginevyo serikali ingefuta zabuni hiyo na mkandarasi kulazimika kulipa faini na kufutiwa kibali cha kufanya kazi nchini.
Hata hivyo, hadi jana kampuni hiyo ilikuwa haijatekeleza agizo hilo wala kuweka vyombo eneo la kazi.
Taarifa zilizopatikana jana zilieleza kuwa, Dk Magufuli alimwandikia barua mkandarasi huyo kumjulisha kusudio la serikali kusitisha mkataba wake kutokana na uzembe. Kwa mujibu wa taarifa hizo, baada ya hapo wizara inaandaa taratibu za kisheria kushughulikia suala hilo, baada ya mhandisi huyo kushindwa kutekeleza agizo la waziri.
Msemaji wa Wizara wa Ujenzi, Martin Ntemo, alisema alisema mkandarasi huyo hajaanza kazi, licha ya waziri kumtaka kufanya hivyo ndani ya siku kumi. Mkataba ni kama mahakama, kwa hiyo mkandarasi huyo siyo kwamba anaogopwa, bali tayari taratibu za kimkataba zitachukuliwa kama alivyosema waziri, alisema Ntemo. Ntemo alikiri mkandarasi huyo kutopeleka vifaa eneo la kazi, licha ya kupewa karipio kali na waziri Magufuli.
Ameandikiwa barua kwa mujibu wa sheria kwa sababu suala la mkataba lilifanyika kisheria, hata hili la kusitisha mkataba wake kwa kushindwa kufanya kazi kwa wakati na kutozingatia karipio alilopewa pia linafanywa kisheria, alisema. Mei 7, mwaka huu, akiwa kwenye ziara ya kukagua barabara, Waziri Magufuli alimwagiza mkandarasi huyo ambaye tayari amelipwa Sh1.27 bilioni kati ya Sh5 bilioni za kujenga barabara yenye umbali wa kilomita 1.5.
Dk Magufuli alishangaa kuona ujenzi haujaanza miezi saba tangu mkandarasi huyo alipwe fedha hiyo. Mkataba huo ulisaniwa Novemba mwaka jana.
Dk John Magufuli
Ummy Muya
Mwananchi
KAMPUNI ya Chico ambayo ilishinda zabuni ya kujenga barabara ya Zakhiem hadi Tanita, imeshindwa kutekeleza agizo la Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, kutaka iwe imeanza kazi ndani ya siku kumi.
Mei 7, mwaka huu, Waziri Magufuli alitoa siku kumi kwa kampuni hiyo iwe imeanza kazi, vinginevyo serikali ingefuta zabuni hiyo na mkandarasi kulazimika kulipa faini na kufutiwa kibali cha kufanya kazi nchini.
Hata hivyo, hadi jana kampuni hiyo ilikuwa haijatekeleza agizo hilo wala kuweka vyombo eneo la kazi.
Taarifa zilizopatikana jana zilieleza kuwa, Dk Magufuli alimwandikia barua mkandarasi huyo kumjulisha kusudio la serikali kusitisha mkataba wake kutokana na uzembe. Kwa mujibu wa taarifa hizo, baada ya hapo wizara inaandaa taratibu za kisheria kushughulikia suala hilo, baada ya mhandisi huyo kushindwa kutekeleza agizo la waziri.
Msemaji wa Wizara wa Ujenzi, Martin Ntemo, alisema alisema mkandarasi huyo hajaanza kazi, licha ya waziri kumtaka kufanya hivyo ndani ya siku kumi. Mkataba ni kama mahakama, kwa hiyo mkandarasi huyo siyo kwamba anaogopwa, bali tayari taratibu za kimkataba zitachukuliwa kama alivyosema waziri, alisema Ntemo. Ntemo alikiri mkandarasi huyo kutopeleka vifaa eneo la kazi, licha ya kupewa karipio kali na waziri Magufuli.
Ameandikiwa barua kwa mujibu wa sheria kwa sababu suala la mkataba lilifanyika kisheria, hata hili la kusitisha mkataba wake kwa kushindwa kufanya kazi kwa wakati na kutozingatia karipio alilopewa pia linafanywa kisheria, alisema. Mei 7, mwaka huu, akiwa kwenye ziara ya kukagua barabara, Waziri Magufuli alimwagiza mkandarasi huyo ambaye tayari amelipwa Sh1.27 bilioni kati ya Sh5 bilioni za kujenga barabara yenye umbali wa kilomita 1.5.
Dk Magufuli alishangaa kuona ujenzi haujaanza miezi saba tangu mkandarasi huyo alipwe fedha hiyo. Mkataba huo ulisaniwa Novemba mwaka jana.