engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Mwezi mmoja tangu mamlaka za Romania kuanza kuwatoza kodi wachawi, watabiri na wapiga ramli nchini humo wamelaani sheria mpya itakayowalazimu kulipa faini, iwapo utabiri wao hautakuwa wa kweli.
Malkia wa uchawi
Mwezi Januari mwaka huu serikali ilibadili sheria na kuwatambua rasmi wachawi, na kuwataka walipe kodi kwa kazi yao hiyo.
Hatua hiyo iliwakasirisha mno wapiga ramli hao kiasi cha kutishia kuitupia serikali uchawi mzito.
wiki iliyopita, muswada wa sheria umewasilishwa katika bunge la nchi hiyo kuwataka walipe faini, ikiwa utabiri wanaotoa kwa wateja usipotokea.
Mmoja wa wakuu wa masuala ya uchawi, Malkia wa uchawi Bratara Buzea amesema "Hawawezi kuwatupia lawama wachawi, wanatakiwa pia kutazama upande wa pili" amesema.
Mchawi huyo amesema atapigana kufa na kupona kuhakikisha muswada huo haupitishwi bungeni.
Malkia Bratara amesema wakati mwingine utabiri wao hautokei kama wanavyobashiri kwa kuwa wateja huwapa taarifa zisizo za kweli.
"Wengine hawasemi ukweli tarehe zao za kuzaliwa, au majina yao halisi, hiyo inasababisha dawa kutofanya kazi" amesema mwanaharakati huyo wa nguvu za giza.
Mtandao wa habari wa Scotsman.com unasema wakosoaji wanadai kuwa hatua hiyo ni ya kupoteza lengo kwa wananchi, kwani nchi hiyo ina matatizo mengi.
Malkia wa uchawi
Mwezi Januari mwaka huu serikali ilibadili sheria na kuwatambua rasmi wachawi, na kuwataka walipe kodi kwa kazi yao hiyo.
Hatua hiyo iliwakasirisha mno wapiga ramli hao kiasi cha kutishia kuitupia serikali uchawi mzito.
wiki iliyopita, muswada wa sheria umewasilishwa katika bunge la nchi hiyo kuwataka walipe faini, ikiwa utabiri wanaotoa kwa wateja usipotokea.
Mmoja wa wakuu wa masuala ya uchawi, Malkia wa uchawi Bratara Buzea amesema "Hawawezi kuwatupia lawama wachawi, wanatakiwa pia kutazama upande wa pili" amesema.
Mchawi huyo amesema atapigana kufa na kupona kuhakikisha muswada huo haupitishwi bungeni.
Malkia Bratara amesema wakati mwingine utabiri wao hautokei kama wanavyobashiri kwa kuwa wateja huwapa taarifa zisizo za kweli.
"Wengine hawasemi ukweli tarehe zao za kuzaliwa, au majina yao halisi, hiyo inasababisha dawa kutofanya kazi" amesema mwanaharakati huyo wa nguvu za giza.
Mtandao wa habari wa Scotsman.com unasema wakosoaji wanadai kuwa hatua hiyo ni ya kupoteza lengo kwa wananchi, kwani nchi hiyo ina matatizo mengi.