Yombayomba
JF-Expert Member
- Aug 23, 2006
- 818
- 214
Hebu tazameni hii picha ya hawa waheshimiwa wanatembelea miradi kijijini na kukutana na wanavijiji, hivi kweli hawana nguo zinazoendana na hali halisi ya mazingira wanayoenda kutembelea? natumaini juzi mliona picha ya ma seneta wa marekani walivyovaa walipoenda kukagua miradi inayofadhiliwa na nchi yao, walivaa kutokana na mazingira wanayokwenda, yaani wanavaa kama wanaenda kula bata majengoni? Hii ni kuonyesha hawako karibu na jamii wanayoiwakilisha.