Waarabu, watu wenye itikadi na misimamo mikali wameinyima Palestina kuwa taifa.

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,641
46,295
Wayahudi au wengine wakiwaita mazayuni ni watu ambao wameishi Palestina/Israel tangu takribani miaka 1200 kabla ya Kristo. Historia yao ni ndefu sana na ipo katika vitabu vya dini na visivyo vya kidini kuonyesha wamekuwepo hapo walipo sasa kwa muda wote. Hapo Israel ndio nyumbani kwao hasa.

Tawala au Himaya mbalimbali zimekuwa zikiwafukuza na kuwatawanya duniani kote lakini wamekuwa wakirudi, na hata katika huko kutawanywa kwao sio wote huondoka katika ardhi yao.

Tofauti na jamii nyingine Wayahudi ni watu wasiojichanganya au kupoteza mila na tamaduni zao popote wanapokwenda jambo mojawapo linalowafanya kuwa walengwa rahisi wa chuki katika maeneo wanayofikia.

Baada ya wengi wao kutawanyika kwa muda mrefu katika maeneo mbalimbali karne ya 20 kwa sababu nyingi walijikita na kujielekeza kurudi kwa wingi katika ardhi ambayo wazazi wao waliishi kwa karne zote. Hapo ndipo vurumai za kila aina zilipoanza lakini baya zaidi ni kwamba waliokuwa wakifikiria hiyo ardhi yote ya Israel ni yao, Wapalestina na Waarabu wengine walikataa kata kata kuwatambua kama ni sehemu ya ardhi hiyo.

Waarabu wakiwa na msimamo mkali walikataa mpango wa Umoja wa mataifa wa azimio 181 wa mwaka 1947 kuunda mataifa mawili ya Israel na Palestina. Israel walichofanya wakachukua sehemu yao na kuanza kujitanua hata katika maeneo ya Wapalestina nyakati za viongozi wenye msimamo mkali kama huyu Benjamin Netanyahu waziri wao mkuu wa sasa.

Huu mgogoro umeshapelekea hata kuuwawa kwa waziri mkuu wa Israel Yitzhak Rabin mwaka 1995 na Muisrael mwenye msimamo mkali kutokana kuonekana kwamba alikuwa akiurejea mpango wa mataifa mawili kupitia Oslo Accords kwa nguvu sana.

Kuna wakati Mahomoud Abbas,kiongozi wa Wapalestina upande wa West Bank aliwahi kusema yalikuwa ni makosa makubwa kwao Wapalestina na Waarabu kuukataa mpango wa UN wa mataifa mawili wa mwaka 1947.

Pia watu wenye msimamo mkali upande wa Israel kama Waziri mkuu wa sasa, Netanyahu wamekuwa wakifanya jitihada zote kuhakikisha suala la mataifa mawili Halifanikiwi pia, mpotezaji mkubwa katikati ya haya yote amekuwa Palestina kwa sababu imeendelea kudhoofika huku Israel ikipata nguvu zaidi na kuwa mtawala wa eneo lote.
 
Hamas kamatieni hapo hapo hivi vibandiko uchwara huku visiwapotezeeni malengo yenu
 
Wayahudi au wengine wakiwaita mazayuni ni watu ambao wameishi Palestina/Israel tangu takribani miaka 1200 kabla ya Kristo. Historia yao ni ndefu sana na ipo katika vitabu vya dini na visivyo vya kidini kuonyesha wamekuwepo hapo walipo sasa kwa muda wote. Hapo Israel ndio nyumbani kwao hasa.

Tawala au Himaya mbalimbali zimekuwa zikiwafukuza na kuwatawanya duniani kote lakini wamekuwa wakirudi, na hata katika huko kutawanywa kwao sio wote huondoka katika ardhi yao.

Tofauti na jamii nyingine Wayahudi ni watu wasiojichanganya au kupoteza mila na tamaduni zao popote wanapokwenda jambo mojawapo linalowafanya kuwa walengwa rahisi wa chuki katika maeneo wanayofikia.

Baada ya wengi wao kutawanyika kwa muda mrefu katika maeneo mbalimbali karne ya 20 kwa sababu nyingi walijikita na kujielekeza kurudi kwa wingi katika ardhi ambayo wazazi wao waliishi kwa karne zote. Hapo ndipo vurumai za kila aina zilipoanza lakini baya zaidi ni kwamba waliokuwa wakifikiria hiyo ardhi yote ya Israel ni yao, Wapalestina na Waarabu wengine walikataa kata kata kuwatambua kama ni sehemu ya ardhi hiyo.

Waarabu wakiwa na msimamo mkali walikataa mpango wa Umoja wa mataifa wa azimio 181 wa mwaka 1947 kuunda mataifa mawili ya Israel na Palestina. Israel walichofanya wakachukua sehemu yao na kuanza kujitanua hata katika maeneo ya Wapalestina nyakati za viongozi wenye msimamo mkali kama huyu Benjamin Netanyahu waziri wao mkuu wa sasa.

Huu mgogoro umeshapelekea hata kuuwawa kwa waziri mkuu wa Israel Yitzhak Rabin mwaka 1995 na Muisrael mwenye msimamo mkali kutokana kuonekana kwamba alikuwa akiurejea mpango wa mataifa mawili kupitia Oslo Accords kwa nguvu sana.

Kuna wakati Mahomoud Abbas,kiongozi wa Wapalestina upande wa West Bank aliwahi kusema yalikuwa ni makosa makubwa kwao Wapalestina na Waarabu kuukataa mpango wa UN wa mataifa mawili wa mwaka 1947.

Pia watu wenye msimamo mkali upande wa Israel kama Waziri mkuu wa sasa, Netanyahu wamekuwa wakifanya jitihada zote kuhakikisha suala la mataifa mawili Halifanikiwi pia, mpotezaji mkubwa katikati ya haya yote amekuwa Palestina kwa sababu imeendelea kudhoofika huku Israel ikipata nguvu zaidi na kuwa mtawala wa eneo lote.
Hebu kaa ujiulize imekuwaje mzungu benjamini netanyahu atawale middle east ilhali yeye kiasili si mtu wa middle east?

Ilikuwaje hawa wazungu wenye msimamo mkali wakawa wayahudi?


Na ukae ukijua muyahudi pure hana tofauti yoyote na mwarabu kimuonekano

Dunia ina siri nyingi mojawapo ni hii ya mzungu kuwa mtawala sehemu ambapo hana asili napo hta kidogo

Ni kama raisi wa nigeria awe mwarabu

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Hebu kaa ujiulize imekuwaje mzungu benjamini netanyahu atawale middle east ilhali yeye kiasili si mtu wa middle east?

Ilikuwaje hawa wazungu wenye msimamo mkali wakawa wayahudi?


Na ukae ukijua muyahudi pure hana tofauti yoyote na mwarabu kimuonekano

Dunia ina siri nyingi mojawapo ni hii ya mzungu kuwa mtawala sehemu ambapo hana asili napo hta kidogo

Ni kama raisi wa nigeria awe mwarabu

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Netanyahu ni mzungu kama walivyo Najib Mikati, Waziri mkuu wa Lebanon, Mfalme Abdullah II wa Jordan au Hafez Al-Assad aliyekuwa Rais wa Syria.
 
Pia watu wenye msimamo mkali upande wa Israel kama Waziri mkuu wa sasa, Netanyahu wamekuwa wakifanya jitihada zote kuhakikisha suala la mataifa mawili Halifanikiwi pia, mpotezaji mkubwa katikati ya haya yote amekuwa Palestina kwa sababu imeendelea kudhoofika huku Israel ikipata nguvu zaidi na kuwa mtawala wa eneo lote.
Kwanini nchi za kiarabu haziwasaidii waarabu wenzao kupata ardhi katika nchi hizo? Niliona uzi humu ukisema Saudi Arabia pekee ndiyo inakubaliana na Israel, kwa mantiki hiyo nchi zingine zote zingeungana kuwapa ardhi wapalestina kwenye maeneo yao
 
Kwanini nchi za kiarabu haziwasaidii waarabu wenzao kupata ardhi katika nchi hizo? Niliona uzi humu ukisema Saudi Arabia pekee ndiyo inakubaliana na Israel, kwa mantiki hiyo nchi zingine zote zingeungana kuwapa ardhi wapalestina kwenye maeneo yao
Nafikiri sababu kubwa ni za kiusalama, Wapalestina wanahama na mgogoro wao, itikadi zao kali na kinyongo dhidi ya Israel na wote ambao wanaona wameshirikiana na Israel kuwakandamiza.

Mwaka 1951 Mpalestina alimuua Mfalme wa Jordan kwa risasi katika msikiti wa Al-Aqsa,

Wapalestina waliwahi kukaribishwa Jordan wakaanzisha vita nchini humo mwaka 1970 wakijaribu kuupindua ufalme wa Jordan.

Wapalestina walihusika kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe Lebanon mwaka 1975.

Mataifa ya jirani itakuwa wanaona ni vigumu sana kuwadhibiti wakiwakubali kwa mamilioni katika nchi zao, nchi kama Misri na Lebanon zina matatizo makubwa ya makundi ya msimamo mkali kwa kuanzia.
 
Wapalestina walihusika kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe Lebanon mwaka 1975.

Mataifa ya jirani itakuwa wanaona ni vigumu sana kuwadhibiti wakiwakubali kwa mamilioni katika nchi zao, nchi kama Misri na Lebanon zina matatizo makubwa ya makundi ya msimamo mkali kwa kuanzia.
Asante sana mkuu umenipa somo ambalo sikuwahi kulipata hapo kabla
 
Nafikiri sababu kubwa ni za kiusalama, Wapalestina wanahama na mgogoro wao, itikadi zao kali na kinyongo dhidi ya Israel na wote ambao wanaona wameshirikiana na Israel kuwakandamiza.

Mwaka 1951 Mpalestina alimuua Mfalme wa Jordan kwa risasi katika msikiti wa Al-Aqsa,

Wapalestina waliwahi kukaribishwa Jordan wakaanzisha vita nchini humo mwaka 1970 wakijaribu kuupindua ufalme wa Jordan.

Wapalestina walihusika kuanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe Lebanon mwaka 1975.

Mataifa ya jirani itakuwa wanaona ni vigumu sana kuwadhibiti wakiwakubali kwa mamilioni katika nchi zao, nchi kama Misri na Lebanon zina matatizo makubwa ya makundi ya msimamo mkali kwa kuanzia.
Acha uongo kama hujui uliza au soma historia vizuri…

He died at the age of 63 from cancer in 1999 and was succeeded by his eldest son, Abdullah II. Eti alipigwa risasi na mpalestina kwenye msikiti wa Al- Aqsa
 
Acha uongo kama hujui uliza au soma historia vizuri…

He died at the age of 63 from cancer in 1999 and was succeeded by his eldest son, Abdullah II. Eti alipigwa risasi na mpalestina kwenye msikiti wa Al- Aqsa

sawa antie Rita zainabu [mention]Ritz [/mention]
 
Kwanini nchi za kiarabu haziwasaidii waarabu wenzao kupata ardhi katika nchi hizo? Niliona uzi humu ukisema Saudi Arabia pekee ndiyo inakubaliana na Israel, kwa mantiki hiyo nchi zingine zote zingeungana kuwapa ardhi wapalestina kwenye maeneo yao
Ndio ndoto zenu ili wapalestine waondoshwe kwenye ardhi zao kama mlivyo fanya huko nyuma
Hilo suala watu waliishalistukia zamani poleni sana jaribuni miaka mingine kwamwaka huu mmechemsha
Hamas kamatieni hapo hapo mpaka magaidi waondoke ukanda wa ghaza kinguvu
 
Acha uongo kama hujui uliza au soma historia vizuri…

He died at the age of 63 from cancer in 1999 and was succeeded by his eldest son, Abdullah II. Eti alipigwa risasi na mpalestina kwenye msikiti wa Al- Aqsa
Go to hell
 
Back
Top Bottom