Waandishi wetu wa habari na lafudhi mbovu

Usiruhusu makosa ya kawaida kwakuwa hatima yake huwa ni haya tunayo jadili hapa.

Sasa hivi hapa namsikia msomaji wa habari toka 88.5 MHz anasema matanki ya mafuta katika kinu cha kuzalisha umeme nchini Palestina yameRIpuka

Wakati huohuo Mwananchi.co.tz kwenye habari yenye kichwa cha habari "Ajali yaua Baba na mwana .... Badala ya kuandika Toyota Coaster wameandika Coastal
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Ajali-ya-gari-yaua-baba--mwanaye/-/1597296/2402590/-/12bbh7bz/-/index.html

hiyo ni yaweza kuwa editing error au mhusika ameshindwa kutofautisha maneno
 
Jana nilikua nasikiliza taarifa ya habari ambayo ilikua inasomwa na mtangazaji fulani wa kituo cha radio cha pride fm Mtwara wakati anasoma habari fulani akakosea baadhi ya neno ila cha kushangaza huyo mtangazaji akaanza kucheka...kwa kwel nilishangazwa sana na kitendo hiki, yaan napata taabu kuamini kama huyu mtangazaji kwel ana jua taratibu za kazi yake.......
 
waandishi wengi tulionao si wa kutumia taaluma ya uandishi wa habari na utangazaji kuifanya kazi hiyo bali hutumia mazoea na wakati mwingine umaarufu, sijui alikuwa muigiza filamu za kibongo au mwanamuziki basi anageuka kuwa mtangazaji akishaambiwa ana sauti nzuri basi mtangazaji. na mbaya zaidi huwa hawaishii kutangaza vipindi vifananavyo na wao bali huenda mbali hadi kutangaza taarifa za habari. hili ni tatizo. ifike mahali wamiliki wa vyombo vya habari wajue nani anatakiwa kufanya nini kwa wakati upi. taarifa za kiutafiti zitangazwe au kuandikwa na waandishi waliosomea taarifa za namna hiyo.
 
Fani ya Habari imevamiwa, sijui watangazaji wanaokotwa wapi, ladha ya taarifa za habari iliyokuwepo enzi hizo (namkumbuka mtangazaji mmoja wa RTD alikuwa anaitwa Christine Chakunegela) haipo tena.

Sasa hivi ni Radio stations chache na Magazeti machache tu ndivyo vyenye habari zenye mvuto, vinginevyo lugha mchosho habari mchosho
zaidi hapo ni ukanjanja tu....
 
Eti "nyimbo mpya ya msanii Linah" badala ya kusema "wimbo mpya wa msanii Linah".
 
Fani imevamiwa hivyo msishangae make kila anayepata div. 5 hukimbilia Utangazaji na uandishi wa Habari...
 
Mmoja kwenye radio fulani alipata shida sana kutamka jina lifuatalo la mtu maarufu. Francois Hollande alitamka: Frankois Hola and.....
 
Jana nilikua nasikiliza taarifa ya habari ambayo ilikua inasomwa na mtangazaji fulani wa kituo cha radio cha pride fm Mtwara wakati anasoma habari fulani akakosea baadhi ya neno ila cha kushangaza huyo mtangazaji akaanza kucheka...kwa kwel nilishangazwa sana na kitendo hiki, yaan napata taabu kuamini kama huyu mtangazaji kwel ana jua taratibu za kazi yake.......

1. nilikuwa

2. anajua

3. Baadhi inatumika katika wingi .....ilipaswa kuwa baadhi ya maneno

4. Hicho

5. Tabu

Nahisi hakuna tofauti kubwa kati yao na wengi wetu humu.
 
Kuna jamaa anaitwa ........(jina la mwanzo silijui) Mwihava wa redio clouds,sidhani kama anaujuzi katika sehemu ya kazi yake, hususan katika kufanya mahojiano..mara kadhaa nimepata kumsikia. Moja ya mifano ilikua katika tukio la viungo vya binadamu lililoikumba IMTU, alipata kumhoji Daktari mmoja wa Muhimbili, baada ya Daktari kukanusha Muhimbili kuhusika na viungo hivyo, Bw. Mwihava aliuliza swali moja tu, alimuuliza hivi..."Daktari vile viungo vya binanaadamu vimetoka Muhimbili nini?!
Binafsi nilijiuliza hivi kweli hili swali limekaa sawa!? ....Muhimbili nini?!? Tena uliza yake ni ile tone ya Kibrazameni brazameni katika serious issue (ingekuwa mambo ya bongoflava nisingeshangaa)..na mara nyingi huongea kwa tone ya namna hiyo sijui ndo inavyopaswa kuwa.!!
 
1. nilikuwa

2. anajua

3. Baadhi inatumika katika wingi .....ilipaswa kuwa baadhi ya maneno

4. Hicho

5. Tabu

Nahisi hakuna tofauti kubwa kati yao na wengi wetu humu.

Lakini hoja ni ya msingi, mbali na uwepo wa watu wasioandika kiswahili kwa namna itakiwavyo ndani ya jamvi.
 
Mimi kweli nakerwa na hilo,ijapokuwa lafudhi ya mtu kuibadilisha,ni taabu sana.Sasa kuna kinachonikasirisha,mtangazaji anaposema asichokijua.Jana,kuna dada mmoja,anatangaza kwamba idd el fitri ni lazima uchinje.Mh,kama hujui si unyamaze!
 
halafu kuna tatizo linaloongezeka kila siku la matumizi mabaya ya 'h' kwa maneno yanayoanza nayo na au 'vowels', mfano badala ya kuandika "ajali hiyo ilitokea siku ya sikukuu ya Idi" mwandishi anaandika "hajali iyo hilitokea siku ya sikukuu ya Hidi".
 
Sio kila mtangazaji ni mwandishi na sio kila mwandishi ni mtangazaji ila mwandishi anaweza kuwa mtangazaji
 
Jooji maratooo wa aiitiivii...
Nyimbo hii iwe maarum kwa salim mbonde wa rtd...

Kero sana.
 
Kuna wengine sijui hawaelewi jinsi ya kutofautisha matumizi ya herufi R na L...We msikilize Shafii Dauda wa Clouds jamaa sijui huwa hajui kutofautisha matumizi ya hizo herufi mbili..Mpira yeye anakupa mpila...
 
Back
Top Bottom