Waafrika Tuna Bongo Ndogo?

PakaJimmy

JF-Expert Member
Apr 29, 2009
16,203
8,725
Kuna hili jambo ambalo limekuwa linanisumbua kila mara:

Nimekuwa nikiwaza sana na mwisho nikafikia hitimisho kwamba Mungu aliwapendelea WAZUNGU sana, akawapa AKILI NYINGI wao, na uwezo wa kufikiri MKUBWA NA MPANA, KULIKO SISI WAAFRIKA, ndio maana wamefika huko waliko kimaendeleo na mfumo wa maisha kijumla!

Hata tukilaumu kwamba walitununua kama bidhaa enzi za biashara ya utumwa, bado hoja hiyo haifuti hoja ya msingi kwamba wana AKILI nyingi zaidi, maana walinunua watumwa baada ya kugundua kwamba KAZI zimewazidi, na wanahitaji wafanyakazi zaidi kwenye mashamba na viwanda!

Mbona sisi hatukuwa wa kwanza kuwachukua wao kama watumwa, na kuwaleta huku Africa? Tulikuwa wapi? - basi mimi nasema , ni kwasababu tuna akili kidogo , au akili yetu IMEPELEA, kulinganisha na wao.
Nawasilisha, nikiomba mitizamo yenu.
 
Mzee, wanadamu wote tuna akili. Hakuna cha mzungu kutuzidi akili watu weusi. Ukitaka kujua kwamba waafrika tulikuwa mbali kabla ya kuja kwa wazungu kutuvuruga soma historia. Unanikumbusha mwana-historia mashuhuri Walter Rodney aliyeandika kitabu cha How Europe Underdeveloped Africa. Anaeleza kirefu maendeleo makubwa ya waafrika yakienda sambamba na ya ulaya mpaka kwenye karne ya 16 hivi.
 
Wakubwa matatizo makubwa tuliyonayo Waafrika ukilinganisha na wenzetu ni uvivu wa kujisomea na waliosoma wanavijua walivyosomea tu, kumbukeni kunatofauti ya usomi na kujisomea.
 
Mzee, wanadamu wote tuna akili. Hakuna cha mzungu kutuzidi akili watu weusi. Ukitaka kujua kwamba waafrika tulikuwa mbali kabla ya kuja kwa wazungu kutuvuruga soma historia. Unanikumbusha mwana-historia mashuhuri Walter Rodney aliyeandika kitabu cha How Europe Underdeveloped Africa. Anaeleza kirefu maendeleo makubwa ya waafrika yakienda sambamba na ya ulaya mpaka kwenye karne ya 16 hivi.

Sasa kama sisi tuna akili kama wao kwa nini wao wakaja wakatuacha kwa mbali?
Halafu huyo Rodney mzushi flani tu hivi. Kwanza hakuwepo kwenye hiyo karne ya 16. Yeye ana mtazamo wa ki Afrocentric na ktk kujitutumua ili asionekane hamnazo ndo akaja na hizo simulizi za eti viwango vya maendeleo vya Afrika vilikuwa sawa na vya Ulaya wakati huo. Give me a long break! I'm not buying that cow manure.
 
Nani kakudanganya kuwa Waafrica tuna akili ndogo? Akili tunazo tena za kutosha sana...
 
Akili ni nyingi mno ndio maana tunawaafrika hata ile kwenye kile kituo mnachokisikia kinachoitwa NASA.

Hicho kituo kimeanzishwa na wazungu na hao Waafrika waliopo hapo wanafanya kazi chini ya uangalizi wa wazungu. Kama Waafrika wana ubavu basi waanzishe cha kwao huko Tema au Nheregani kitakachokuwa kinaongozwa na Waafrika weusi.
 
Sasa kama sisi tuna akili kama wao kwa nini wao wakaja wakatuacha kwa mbali?
Halafu huyo Rodney mzushi flani tu hivi. Kwanza hakuwepo kwenye hiyo karne ya 16. Yeye ana mtazamo wa ki Afrocentric na ktk kujitutumua ili asionekane hamnazo ndo akaja na hizo simulizi za eti viwango vya maendeleo vya Afrika vilikuwa sawa na vya Ulaya wakati huo. Give me a long break! I'm not buying that cow manure.


We Nyani Ngabu uko na mimi sawasawa!

Wazungu walipewa nusu ya ziada kutushinda.
Kwanini kwetu sisi hata Maprofesa wetu wanarudi kugombea Ubunge, wakaacha fani zao za Kufundisha, Kufanya Utafiti na Kutoa Ushauri?

Kisha wakiwa wabunge wanaanza "sihasa"..uwongouwongo tu na ukweli kwa mbali!!

Narejea."Tuna AKILI PUNGUFU kuliko wazungu!"
 
Miafrica ndo tulivyo.
Mkuu umekosea kidogo tu.Wafrica tuna akili ila sisi ni wajinga ni sawa na kuku.Kuku ukimwaga mchele pembeni anaanza kula ukimpiga anakimbi, baada ya sekunde anasahau kuwa amepigwa anarudi hapo hapo kula tena, ndo tulivyo kama kuku tena wakienyeji.
 
tukumbuke akili iko huru ya mambo yote, usipoitumia si kwamba hauna akili. NA swala la yule mwandishi Bwana Walter, si kila kitu utakachokitolea simulizi ni lazima uwepo ndio maana hata watu wana imani za dini zinazozungumzia mambo mengi na watu kuamini wakati hawakuwepo
 
tukumbuke akili iko huru ya mambo yote, usipoitumia si kwamba hauna akili. NA swala la yule mwandishi Bwana Walter, si kila kitu utakachokitolea simulizi ni lazima uwepo ndio maana hata watu wana imani za dini zinazozungumzia mambo mengi na watu kuamini wakati hawakuwepo

Sasa wewe unachanganya mambo hapa. Walter anazungumzia vitu ambavyo supposedly vilikuwepo. Maendeleo ni mambo ambayo yanaonekana, yanagusika, yananukia, n.k. Siyo imani hiyo. Mambo ya imani ni mchezo mwingine kabisa.
 
sisi afica mazingira yanatubeba thats why hatutumii akili, pia sababu jamaa wameshawahi, hamna haja ya kushindana, tumeumbwa kuridhika na kusifia vya watu,tufanyeje basi? km wahagundua tairi unataka ugundue nini? incase tungekuwa na challenging enviroment, let say hali mbaya ya hewa, topography etc tungetia akili la sivyo ingekuwa kifo tu.
 
sisi afica mazingira yanatubeba thats why hatutumii akili, pia sababu jamaa wameshawahi, hamna haja ya kushindana, tumeumbwa kuridhika na kusifia vya watu,tufanyeje basi? km wahagundua tairi unataka ugundue nini? incase tungekuwa na challenging enviroment, let say hali mbaya ya hewa, topography etc tungetia akili la sivyo ingekuwa kifo tu.

Hivi joto la Dar au Timbuktu ni hali nzuri ya hewa?
 
Sasa wewe unachanganya mambo hapa. Walter anazungumzia vitu ambavyo supposedly vilikuwepo. Maendeleo ni mambo ambayo yanaonekana, yanagusika, yananukia, n.k. Siyo imani hiyo. Mambo ya imani ni mchezo mwingine kabisa.
Sisi tunachanganya hoja sana, mahubiri mengi yanazungumzia watu walioitwa manabii waliokuwepo, yanazungumzia maeneo yaliyokuwepo na hata sasa yapo ni kama maendeleo aliyoyazungumzia Bwana Walter, inawezekana yalikuwa yameshafikiwa au la ni kiasi cha kuamini maana hakuna aliyekuwepo kama maendeleo hayo au manabii na mitume hao walikuwepo wakati husika. Swala kubwa ni akili, watu wote wana akili ila labda mgeniambia tumetofautiana jinsi ya kutumia akili tulizonazo katika kutambua mambo na hata kuyapambanua. We shouldn't change our opinions and call them reality, we better dig them deep either.
 
Hata kama tuna akili sawa lakini fact is wao wame tumia zao kuliko sisi. Kuwa na ubongo na kuto utumia hauona faida yoyote. That's what separates a "could be" and a "already is". It's time we lived up to our potential badala ya kujiona "sleeping giants" kila siku. We need to wake up from our slumber.
 
Ukitaka kujua kama tunaakili au hatuna subiri 2010. Au kwa ufupi angalia tu jinsi EPA tunavyoiendesha. Watu wanaona maslahi ya mafisadi ni bora kuliko ya taifa. Wazungu hawako hivyo, wenzetu wanaangalia taifa kwanza, sio vyama.
 
We Nyani Ngabu uko na mimi sawasawa!

Wazungu walipewa nusu ya ziada kutushinda.
Kwanini kwetu sisi hata Maprofesa wetu wanarudi kugombea Ubunge, wakaacha fani zao za Kufundisha, Kufanya Utafiti na Kutoa Ushauri?

Kisha wakiwa wabunge wanaanza "sihasa"..uwongouwongo tu na ukweli kwa mbali!!

Narejea."Tuna AKILI PUNGUFU kuliko wazungu!"

Kama tuna akili pungufu mbona tukufanya kazi na wazungu au tulifanya kazi uzunguni tunafanya kazi vizuri na tunatumia vizuri akili zetu?
 
Back
Top Bottom