Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 975
- 47
Mtafiti wa TEKNOHAMA na mwandishi, Ole Jørgen Anfindsen (pichani) anasema kuwa Waafrika wana akili ndogo (IQ = intelligence quotient) kuliko watu wengine duniani. Amesema wazi leo kwenye kipindi cha TV 2 alltid nyheter saa 18:55 19:19 CET, kuwa kwa kuwa watu wa mataifa mengine akili zao ni finyu, basi ni vigumu watu kutoka mataifa hayo, kuzoea mila, desturi na utamaduni wa Norway, hususan wa nchi za magharibi. Akiendelea, alisema kuwa watu wenye IQ ndogo inakuwa vigumu kuenda sambamba na teknolojia inavyoenda kasi.
Alikuwa akielezea utafiti alioufanya na kuandika kwenye kitabu chake kiitwacho Selvmordsparadigmet. Pamoja na kuelezea uzezeta wa Waafrika, pia ameishambulia siasa na sheria za zinazohusu wageni kuwa ni laini mno kiasi cha kutia aibu. Anapendekeza sheria za wageni kuzibwa matundu na kukazwa zaidi ili wageni wasiingie Norway kiholela.