Vurugu za Dar na Zanzibar: Dalili za uwepo wa Alshabab???

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
May 9, 2007
3,833
2,790
Nimekaa na kutafakari matukio ya hivi karibuni yaliyofumuka hapa Dar na kule Zanzibar kwa kisingizio cha mtoto kukojolea quran tukufu. Makosa kama haya ni nadra sana kujitokeza hapa nchini ukiachilia mbali mihadhara ya kukashifu dini nyingine ambayo imezaliwa mwaka 1992 na inaendelea hadi sasa.
Vurugu hizi zimenifanya kutoamini kama nipo Tanzania, hakika nilidhani niko Syria au Libya. Lakini nilipotoka ofisini nikaona niko barabara ile ile ninayoipita kila siku niliyoizoae. Kipindi chote hiki nimekaa kimya, siyo kwasababu niliamua kufanya hivyo la hasha bali ni kwasababu ubongo wangu ulidumaa kufanya kazi kwa mshangao wa "Is this Tanzania?????" Hadi nilipozinduka nikawa siamini nilichokiona badala yake nikaishia kudhani kuwa huenda WABABE WA VITA BAADA YA KUSAMBARATISHWA KISMAYU WAMEINGIA NCHINI KWA KIVULI CHA KUKOJOLEA QURAN. Hukumu iliyotolewa kwa makanisa si sahihi. Kitabu kilichokosewa si cha binadamu bali Allah. Ilikuwa wahusika waliofanya mchakato na kufanikisha kukojolewa quran hiyo hukumu itolewe na Allah mwenyewe. Inawezekana adhabu mojawapo ingekuwa ni kuona ukweli wake jinsi ilivyo na nguvu akaweza kuslimu na kuwa muislamu, kinyume na alivyotishwa kwa maandamano na uchomaji na uporaji wa mali za Wakristo. Mara nyingi nimekuwa nashuhudia kauli za viongozi wa kiislamu kwamba waliotenda uovu huo si waislamu. Je siyo waislamu kwa sababu ya huo uovu?? Je ikiwa kungekuwa na majibu ya kulingana na majibu hayo nao Wakristo wakasema aliyekojolea quran siyo Mkristo unafahamu ukubwa wa tatizo ungekuwa mkubwa zaidi. Nasema hivi kwa sababu mara nyingi kumekuwa na kauli hizi kwamba waliofanya uovu fulani si waislamu, je kuwa muislamu maana yake huwezi kukosea??? Ifike wakati waislamu wawe wawazi kwamba waliofanya uovu huo ni waislamu lakini wameteleza.....nk. Katika misikiti mbalimbali mahubiri ya kukashfu Ukristo yanaendelea kama kawaida licha ya serikali kuzuia huo uinjilishaji usiowahusu, je wakikamatwa na kutiwa gerezani nao watakuwa si waislamu japo walikamatiwa ndani ya misikiti waki-injlisha ndivyo sivyo???. Kasi hii ya uvunjifu wa amani Tanzaia tujipange:
1. WAKRISTO ENDELEENI KUDUMISHA AMANI NA UTULIVU, MSIKUBALI KUJIBIZANA NA WATOTO WA MAMA MDOGO HAJRA.
2. YESU ALISEMA MTU AKIKUPIGA KOFI SHAVU LA KUSHOTO MGEUZIE NA LA KULIA, AKIKUVUA SHATI MUACHIE NA KOTI.
3. SALA YA BABA YETU ULIYE MBINGUNI INATUTAKA KUWASAMEHE WALE WOTE WALIOTUKOSEA, TUFANYE HIVYO MARA MOJA.
4. KAMWE TUSIANZE KUHUBIRI UISLAMU MAKANISANI AMA MAHALA POPOTE KWANI SISI SI WAQURANIST.
5. TUSIFU YESU KRISTU BWANA YESU ASIFIWE.
 
Wenye busara tu ndo watakuelewa lakini kuna hawa ndugu zangu na mimi utawaskia hapa na matusi yao
Nashukuru sana nikiri wazi kwamba WAPO WAISLAMU NINAOWAFAHAMU WANAJISIKIA AIBU SANA KWA KITENDO HIKI. WENGI WAMEKUWA WAKISEMA MTOTO HUYU ALIKOJOLEA TU YAMEKUWA HAYA JE ANGENYEA JE.

Matusi nitakayoyapata ni moja ya thawabu nitakayostahili ili neno litimie kwamba "HATA USHAURI WANGU WALIUKATAA NA KUUONA HAUNA MAANA"

 
Back
Top Bottom