Vladimir Putin :- Sihofii nchi za magharibi kuniwekea vikwazo

Sababu kubwa ni madeni ya bank za marekani
Kuwa msambazaji wa gesi nchi za ulaya
 
Rais wa Urusi,Vladimir Putin anefikia hatua ya kusema hato lipa madeni kwa Bank za Marekani

Russia future on hold, baada ya hili vuguvugu hatakopesheka. nani amkopeshe!

Putin amekuwa kama miafrika, hajafikiria mbali kabisa
 
Kumbe ni muoga eeeeee
Acha apewe economics and diplomatics sanctions
Na hayo madeni atayalipa tu
Mbili marekan na nchi za magharibu hawawezi pata taabu yeye na wananchi wake ndo wataonja joto
 
Urusi inauza sana gesi inayohitajika sana ulaya magharibi kila siku na mbaya zaidi kipindi che winter.Putin bado ukomunist na uzalendo unamlevya...analia sana kuwa USSR ilikuwa kimakosa sana na ni pigo kubwa sana. Jamaa hajiamini sana..karusha ,ndege,helcopter, anakimbizana na mabilionea wa kirusi waliopiga bao ktk ubinafsishaji...na kuwaua watu wote wenye mrengo wa kidemocrasia,,, Kwa ujumla akili yake ni kuirudisha USSR na nguvu ya Urusi..sijui km anajua itabidi wapigane na China thisi time kugombea nani ataongoza ukomunisty
 
Rais wa Urusi,Vladimir Putin amezidi kushikilia msimamo wake kuwa hana hofu na taarifa zinazotolewa na nchi za kimagharibi juu ya kumwekea vikwazo kutokana na kushiriki kwake katika hali ya kisiasa nchini Ukraine.
Kama hiyo haitoshi anefikia hatua ya kusema hato lipa madeni kwa Bank za Marekani endapo vikwazo hivyo atawekewa na kusema vikwazo hivyo vitaathiri pande zote mbili yaani Russia pamoja na nchi nyingine za magharibi.
Swali langu ni je,sababu zipi zinazompa Putin kiburi cha kujibiza na hizi Big Powers? au ni sababu anajua nchi za magharibi zinategemea mafuta ambayo yamepita ndani ya nchi ya Russia?

Wewe jamaa unamaanisha Russia sio Super power..
 
Wewe jamaa unamaanisha Russia sio Super power..

Inaweza kuwa super power In some sense but kwa akili ya kawaida ukisikia habari za super power moja kwa moja akili huwa inaenda kwa big capitalist countries kuwa ndio super power
 
Unajua Waafrika Tuna Shida Wengi Wapo Upande Wa Mrusi Moyoni Ila Mdomoni Upande Wa Marekan Na Wenzake Ktk Hili La Cremia.
 
NCHI NYINGI DUNIANI TUNATUMIA VINGI TUSIVYOVIZALISHA NA TUNAZALISHA TUSIVYOTUMIA NA MRUSI AMEJITAIDI KUPUNGUZA KUTUMIA ASIVYOZALISHA KWA KIASI KIKUBWA!SHIDA NI GESI AMBAYO ANAZALISHA ITAKUAJE ILA KWA MUDA HUU ULAYA WANAFIKIRIA MARA MBILI.KIUCHUMI SI MBABE KM G7 ila kiteknolojia anajitosheleza na kiulizi ndo ngome pia nyuklia
 
Mrusi Pia Ana Wafuasi Wengi Asia Na Latin America Japo Afrika Wanapungua Ktk Maeneo Ambayo Ana Emfluence Kubwa Kuna Madhara Kwa Magharibi Kwa Kua Kuna Eidha Soko Kubwa La Bidhaa Au Malighafi Adimu Km Mafuta.pia Tazama Mchina Na Mrusi Hata Idadi Ya Utalii Inayofanyika Ktk Nchi Hizi Ni Kubwa
 
namuunga mkono putin hawa western ni wanafki sana lengo ni kuidhoofisha russia ila watashindwa.
 
huu ndio mwisho ulaya na America wamezidi kuonea vinchi vidogo mara hii wameingia cha kike, watamjua mrussiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii oyeeeeeeeeeeeeee
 
ulaya itatafuta pakutokea mwaka huu kwa ni mijitu fitna na mibinafsi michoyo, then ina roho mbaya sana naomba mungu mrusi aifute katika ramani dunia.
 
Huu mgogoro sio mzuri kwa pande zote zinazohusika.Kuna impact kubwa kiuchumi kuiwekea Russia vikwazo.Russia ni muhimu katika Uzalishaji wa Gas kwa karibu Nchi 13 za Ulaya,Zikiwemo Nchi zenye nguvu kubwa kiuchumi kama Germany na Italy.Mgogoro huu wa kisiasa utaadhiri hali ya Uchumi wa Mataifa mengi ya Ulaya,Marekani na Russia.Warusi wamekwishatangaza wazi kuwa wataacha kutumia US$ Katika biashara zao na mataifa mengine kama China,India,Indonesia na Japan, wakifanya hivyo itakuwa pigo kubwa kiuchumi kwa Nchi ya Marekani.Ni matarajio ya kila mpenda amani kuwa Mgogoro huu utatatuliwa kwa njia za amani.
 
Huu mgogoro sio mzuri kwa pande zote zinazohusika.Kuna impact kubwa kiuchumi kuiwekea Russia vikwazo.Russia ni muhimu katika Uzalishaji wa Gas kwa karibu Nchi 13 za Ulaya,Zikiwemo Nchi zenye nguvu kubwa kiuchumi kama Germany na Italy.Mgogoro huu wa kisiasa utaadhiri hali ya Uchumi wa Mataifa mengi ya Ulaya,Marekani na Russia.Warusi wamekwishatangaza wazi kuwa wataacha kutumia US$ Katika biashara zao na mataifa mengine kama China,India,Indonesia na Japan, wakifanya hivyo itakuwa pigo kubwa kiuchumi kwa Nchi ya Marekani.Ni matarajio ya kila mpenda amani kuwa Mgogoro huu utatatuliwa kwa njia za amani.
Ni wakati muafaka sasa ku share migogoro na watu wazima ili na wao waonje utamu wake!
 
huu ndio mwisho ulaya na America wamezidi kuonea vinchi vidogo mara hii wameingia cha kike, watamjua mrussiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii oyeeeeeeeeeeeeee

..........Mmarekani anatamba wazi wazi kuwa anawapa silaha fedha waasi wano pambana a Assad wa Syria !:rolleyez:
 
Unajua Waafrika Tuna Shida Wengi Wapo Upande Wa Mrusi Moyoni Ila Mdomoni Upande Wa Marekan Na Wenzake Ktk Hili La Cremia.

mimi sio moyoni tu hata mdomoni namkubali sana huyu jamaa.kwa mbali naona anafanana na mbabe Joseph Stalin.tusilolijua tu ni kuwa mambo mengi yanayoendesha siasa za nje yanafanyika sirini,kwa ujasusi na matumizi ya jeshi.Putin anajua anachokifanya na warusi wanamuunga mkono.Achaneni na propaganda za vyombo vya habari vya magharibi!
 
mwache awape hao waasi silaha ipo lakini akumbuke mwisho wake unakaribia, anamaadui kila kona kwa hiyo ajitayarishe kusarambatika.ww kuwa na akili za sabuni mrussiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii babaaaaa maliza hii mijitu mibaya tupumue.
 
Back
Top Bottom