nimeitumia for years, sidhani kama mtu ananunua kiwanja kichwakichwa, utafanya all the necessary due diligence ... Usihofu kabisa, kuna watu wamenunua kwa jina hilo ...
Kigamboni si ardhi hawafanyi processing yoyote? Hata kama vina hati mkiuziana utabadilishia wapi wakati wizara ishatoa stop orde kwa maeneo yote hayo?? Na juzi tu watu wametoka kupewa baria za kuitwa kuhakiki mali kwa mara ya mwisho! Pia kwa nini usitoe namba yako ya simu au email inayoeleweka?
Hizi bei za viwanja siku hizi mpaka zinatisha, hivi watu mnapata wapi hela jamani, hichi kimshahara cha serikali nasi tutanunua hivyo viwanja kweli? au ndio tunaambiwa tuwe wabadhirifu kinamna?
Viwanja vya kibada, vya serikali, havihusiki na stop order ya serikali. nakushauri ukipata nafasi utembelee maeneo hayo na utaona jinsi watu wanavyoendelea na ujenzi. Kuhusu hizo bei, inategemea na eneo. Kwa mfano, kama mtu anataka mbali zaidi kutoka ferry, anaweza kupata kwa bei nafuu zaidi.
Fuatilia vizuri utagundua viwanja vya Kibada, Kisota, Mwongozo (miradi ya serikali), ingwa viko ndani ya mradi wa mji mpya, havihusiki na stop order kwa vile vimepangwa vizuri tayari ..., na hati zinatolewa kama kawaida
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.