Bado Kidogo 2015
JF-Expert Member
- May 24, 2012
- 207
- 78
Wanabodi habari zenu,
Kuna jambo moja kubwa ambalo linaendelea saizi nchini lakini nimeona nilielezee kwa kadri ya uelewa wangu nalo si lingine bali VITA YA PROPAGANGA.
Vita hii ni kama ilizinduliwa rasmi na Rais wa JMT kupitia mkutano mkuu wa Taifa wa chama hicho uliofanyika October - 2012 pale aliposema " Wajibuni maana uongo unaposemwa au kurudiwarudiwa sana hugeuka kuwa ukweli" Hii ni kama ilikuwa hadhari kwa wanaCCM kuwajibu CDM kwa kila watakachokifanya ili kuondoa unayodhaniwa uongo au sumu inayotapanywa na CDM chama ambacho kimegeuka kuwa tishio kwa CCM!
Mara baada ya kutangazwa kwa sekretarieti mpya ya chama hicho sote tulishuhudia mikutano mbali mbali ya hadhara ikifanywa sehemu mbali mbali ili kuhuisha uhai wa chama ulikuwa unaonekana kufa. Sekretarieti hiyo ikiongozwa na A. Kinana, Nape Nauye, Mwigulu Nchema na wengine kwa sasa bado inahangaika kufa na kupona kuhuisha chama ambacho kimetawala takribani miaka 50 sasa.
Pamoja na kufanya mikutano hiyo lakini bado sekretarieti hiyo imekwenda mbali zaidi kwa kuzua hoja ambazo zitawahamisha wanaCDM kujadili ukombozi wa pili wa nchi hii kupitia M4C na operation nyingine, badala yake kujadili mambo ambayo mengi hayana msingi ikwemo ukabila, udini, kadi mbili na hili la saizi la Masalia.
Ni kweli mambo hayo baadhi hata wao wanajua yameprove "failure" kama vile hoja ya udini, ukabila, ukaskazini lakini walifurahi kwa wanaCDM walivyojichanganya kuhusu kadi mbili na hili la kulipuana mtandaoni kwa hoja nzito kama hapa ndiyo mahakama ya chama!!!!
Nini sasa mustkabali wa yote hayo endapo VITA HII YA PROPAGANDA nayo itashindwa ambacho ndicho kiini cha mada yangu????
Endapo haya yote yatashindwa basi tutegemee;
1.0 Matumizi makubwa sana ya fedha ili kurubuni umma au kuhadaa umma. Hii itajumuisha kununua watu wengi maarufu wasio na msimamo ambao watatumika kukidhalilisha chama kwa kuwawekea mdomoni maneno ambayo yatakuwa ni fedheha kwa chama ili hali watu hao wakijua hawasemi ukweli ila ni kutokana na nguvu ya fedha.
Pamoja na hayo bado MEDIA nyingi zitanunuliwa kuendeleza vita hii hasa TVs, radio na magazeti ambayo zina/yana wigo mpana.
2.0 Muendelezo wa matumizi makubwa zaidi ya haya ya nguvu ya dola hasa polisi japokuwa polisi wenyewe wanajua hali halisi serikali wanayoitumikia bado haiwatendei haki maana kadri sinavyokwenda ndiyo maslahi yao yanavyotupa mbali. Nadhani ukitoa walimu wanaofuata kwa madeni ni vyombo vya ulinzi na usalama.
3.0 Vita hii ya propaganda itawahi kutoa majibu na kutoa mwanya wa nini kifanyike juu ya katiba mpya. Upo uwezekano mkubwaa katiba mpyaa isikamilike kwa wakati na kupelekea uchaguzi kufanyika katika mazingira ya 2010.
4.0 Kuunganisha nguvu ya majeshi hasa TISS, TPDF & Police kukisaidia chama kishinde kwa ahadi ya kulipa fadhila na kuruhusu lolote lakini nchi isiangukie kwa wapinzani.
Hayo ni maoni yangu endapo vita hii propaganda itashindwa.
Nawasilisha.
Kuna jambo moja kubwa ambalo linaendelea saizi nchini lakini nimeona nilielezee kwa kadri ya uelewa wangu nalo si lingine bali VITA YA PROPAGANGA.
Vita hii ni kama ilizinduliwa rasmi na Rais wa JMT kupitia mkutano mkuu wa Taifa wa chama hicho uliofanyika October - 2012 pale aliposema " Wajibuni maana uongo unaposemwa au kurudiwarudiwa sana hugeuka kuwa ukweli" Hii ni kama ilikuwa hadhari kwa wanaCCM kuwajibu CDM kwa kila watakachokifanya ili kuondoa unayodhaniwa uongo au sumu inayotapanywa na CDM chama ambacho kimegeuka kuwa tishio kwa CCM!
Mara baada ya kutangazwa kwa sekretarieti mpya ya chama hicho sote tulishuhudia mikutano mbali mbali ya hadhara ikifanywa sehemu mbali mbali ili kuhuisha uhai wa chama ulikuwa unaonekana kufa. Sekretarieti hiyo ikiongozwa na A. Kinana, Nape Nauye, Mwigulu Nchema na wengine kwa sasa bado inahangaika kufa na kupona kuhuisha chama ambacho kimetawala takribani miaka 50 sasa.
Pamoja na kufanya mikutano hiyo lakini bado sekretarieti hiyo imekwenda mbali zaidi kwa kuzua hoja ambazo zitawahamisha wanaCDM kujadili ukombozi wa pili wa nchi hii kupitia M4C na operation nyingine, badala yake kujadili mambo ambayo mengi hayana msingi ikwemo ukabila, udini, kadi mbili na hili la saizi la Masalia.
Ni kweli mambo hayo baadhi hata wao wanajua yameprove "failure" kama vile hoja ya udini, ukabila, ukaskazini lakini walifurahi kwa wanaCDM walivyojichanganya kuhusu kadi mbili na hili la kulipuana mtandaoni kwa hoja nzito kama hapa ndiyo mahakama ya chama!!!!
Nini sasa mustkabali wa yote hayo endapo VITA HII YA PROPAGANDA nayo itashindwa ambacho ndicho kiini cha mada yangu????
Endapo haya yote yatashindwa basi tutegemee;
1.0 Matumizi makubwa sana ya fedha ili kurubuni umma au kuhadaa umma. Hii itajumuisha kununua watu wengi maarufu wasio na msimamo ambao watatumika kukidhalilisha chama kwa kuwawekea mdomoni maneno ambayo yatakuwa ni fedheha kwa chama ili hali watu hao wakijua hawasemi ukweli ila ni kutokana na nguvu ya fedha.
Pamoja na hayo bado MEDIA nyingi zitanunuliwa kuendeleza vita hii hasa TVs, radio na magazeti ambayo zina/yana wigo mpana.
2.0 Muendelezo wa matumizi makubwa zaidi ya haya ya nguvu ya dola hasa polisi japokuwa polisi wenyewe wanajua hali halisi serikali wanayoitumikia bado haiwatendei haki maana kadri sinavyokwenda ndiyo maslahi yao yanavyotupa mbali. Nadhani ukitoa walimu wanaofuata kwa madeni ni vyombo vya ulinzi na usalama.
3.0 Vita hii ya propaganda itawahi kutoa majibu na kutoa mwanya wa nini kifanyike juu ya katiba mpya. Upo uwezekano mkubwaa katiba mpyaa isikamilike kwa wakati na kupelekea uchaguzi kufanyika katika mazingira ya 2010.
4.0 Kuunganisha nguvu ya majeshi hasa TISS, TPDF & Police kukisaidia chama kishinde kwa ahadi ya kulipa fadhila na kuruhusu lolote lakini nchi isiangukie kwa wapinzani.
Hayo ni maoni yangu endapo vita hii propaganda itashindwa.
Nawasilisha.