Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Vita vya maneno baina ya Ufaransa na Uingereza vyaongezeka,Sarkozy aonyesha kudharau Uchumi wa Uingereza!
Ugomvi na vita vya maneno kati ya wakoloni wakongwe wa Ulaya yaani Ufaransa na Uingereza vimeongezeka baada ya Rais wa Ufaransa kuufanyia istihzai uchumi wa Uingereza akisema kuwa, nchi hiyo hata viwanda haina.
Jana Rais Nicolas Sarkozy wa Ufaransa alizungumza na waandishi wa habari kupitia televisheni kwa lengo la kutetea mpango wake wa kuongeza kodi nchini Ufaransa na kudai kuwa mpango huo una nia ya kuimarisha uchumi wa nchi hiyo.
Wakati mwandishi mmoja wa alipomuuliza Rais huyo wa Ufaransa kwamba ni vipi anatetea mpango wake huo wakati kabla ya hapo mpango kama huo umetekelezwa nchini Uingereza na kushindwa, Sarkozy amesema mpango huo umeshindwa nchini Uingereza kwa sababu nchi hiyo haina viwanda.
Mwaka 2009 pia Sarkozy alitabiri kuwa, mpango wa Uingereza wa kuongeza kodi ungelishindwa tu, matamshi ambayo hayakuwafurahisha viongozi wa Uingereza ambao nao baadaye walikwamisha mpango wa Ufaransa na Ujerumani katika eneo la Euro jambo ambalo lilitishia vibaya kulisambaratisha eneo hilo.
Matatizo makubwa ya kiuchumi yanayozikabili nchi za Ulaya hivi sasa yanazidi kuonesha uadui na sura halisi ya viongozi wanaochekeana mbele ya vyombo vya habari barani humo.
Ugomvi na vita vya maneno kati ya wakoloni wakongwe wa Ulaya yaani Ufaransa na Uingereza vimeongezeka baada ya Rais wa Ufaransa kuufanyia istihzai uchumi wa Uingereza akisema kuwa, nchi hiyo hata viwanda haina.
Jana Rais Nicolas Sarkozy wa Ufaransa alizungumza na waandishi wa habari kupitia televisheni kwa lengo la kutetea mpango wake wa kuongeza kodi nchini Ufaransa na kudai kuwa mpango huo una nia ya kuimarisha uchumi wa nchi hiyo.
Wakati mwandishi mmoja wa alipomuuliza Rais huyo wa Ufaransa kwamba ni vipi anatetea mpango wake huo wakati kabla ya hapo mpango kama huo umetekelezwa nchini Uingereza na kushindwa, Sarkozy amesema mpango huo umeshindwa nchini Uingereza kwa sababu nchi hiyo haina viwanda.
Mwaka 2009 pia Sarkozy alitabiri kuwa, mpango wa Uingereza wa kuongeza kodi ungelishindwa tu, matamshi ambayo hayakuwafurahisha viongozi wa Uingereza ambao nao baadaye walikwamisha mpango wa Ufaransa na Ujerumani katika eneo la Euro jambo ambalo lilitishia vibaya kulisambaratisha eneo hilo.
Matatizo makubwa ya kiuchumi yanayozikabili nchi za Ulaya hivi sasa yanazidi kuonesha uadui na sura halisi ya viongozi wanaochekeana mbele ya vyombo vya habari barani humo.