bibikuku
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 832
- 495
Vita ya uenyekiti UWT inaendelea. Baada ya Mama Kilango kudaiwa kuendesha kikao cha siri na wenyeviti wa UWT mikoa na wilaya na kuwakatia pesa, sasa Mama Kilango ajitokeza na kujibu mapigo........
Kilango awashukia wanaompiga vijembe UWT | Send to a friend |
Friday, 16 March 2012 20:35 |
0diggsdigg Daniel Mjema, Moshi MBUNGE wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela, amerejea nchini kutoka Newyork Marekani na kujibu mapigo kwa kile alichodai ni njama za kumchafua kuelekea uchaguzi wa Mwenyekiti wa Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT,) unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu. Akizungumza na Mwananchi jana, Kilango alisema yeye ni mwanasiasa makini na anayejua anachokifanya na kwamba, hawezi kulumbana na baadhi ya wanaCCM ambao ni jadi yao kutukana wenzao kipindi cha uchaguzi. Ingawa Kilango hakumtaja jina kiongozi yeyote au mwanachama wa UWT anayemchafua, lakini alisema baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakimtolea maneno ya kashfa. Mimi ni mwanasiasa ninayejua nafanya nini mwaka huu ni wa uchaguzi ndani ya chama, kwa hiyo yatasemwa mengi na mimi mwaka huu nitakaa kimya kama nilivyokaa kimya tumboni mwa mama yangu, alisema Kilango. Kilango alisema kama atajiingiza katika malumbano hayo aliyoyaita hayana tija, atawafanya wanachama wa CCM washindwe kutofautisha kati ya mwanasiasa makini na asiye makini, jambo ambalo ni hatari kwa kiongozi. Mwanasiasa huyo machachari ambaye anatajwa kuwa miongoni mwa wanaowania nafasi hiyo ya juu ndani ya UWT, alisisitiza kuwa kila kiongozi atapimwa kwa matendo yake na kauli zake kwa jamii anayoongoza. Katika la Mwananchi la jana, kulikuwapo na habari kutoka mkoani Dodoma ikimkariri mwenyekiti mmoja wa UWT akimpiga vijembe Kilango kuwa, alisafiri kutoka Uingereza hadi nchini ili kuwahi mkoani humo. Tangu jina la Kilango litajwe kuwa miongoni mwa kinyanganyiro hicho kumekuwapo na kauli za kumpiga vijembe na kuelezea kuwa, hafai kuwania nafasi hiyo. Sofia Simba ambaye ni Mwenyekiti wa UWT ameshatangaza rasmi kutetea kiti chake, ingawa licha ya Kilango kuonekana kuungwa mkono na wanachama wengi wa UWT, bado hajaweka wazi msimamo wake kama yumo kwenye kinyanganyiro hicho ama la. |