Visa za Tanzania na maofisa uhamiahaji

Wamekuja kufanya workshop au kucheki wapi panafaa kuwaibiwa hawa mabwege???? Hata mm akipita mtu mweupe kwenye anga zangu namliza tu.
 
Kwanini u-conclude kosa liko liko kwa uhamiaji au afisa wa ifakara tu? Kwani mwombaji hawezi kuwa alitenda kosa la kufanya shughuli isiyoendana na visa yake? Huwezi kuja na conclusion za aina hii bila kusikiliza pande zote.
Rejea kusoma sentensi vyema, nachelea sina muda wa ufafanuzi.
 
Wewe unayongela CTA nenda kweye website yao haya ndo maelEzo ya CTA: Carrying on Temporary Assignment (CTA)
CTA is issued to prospective visitors who intend to visit Tanzania for purposes of making feasibility studies, establishing professional and business contacts, and making arrangements for investments during the start-up period. The validity of this visa is two months. This type of visa is issued at the entry point.
 
Mkuu lakini ndio sheria inavyotaka?
soma kichwa cha thread,hivi hata hivyo kuna sheria inayoruhusu watu kuuza wanyama kutoka kweney mbuga zetu? au mafisadi kuchota hela? ncho ishauzwa hii ohoooowe kaa tu
 
Ndugu wana JF huyo mzungu kutoka Amerika amekuja kwa short vist katika tasisi fulani hapo Ifakara na hafanyi kazi yoyote ile.Anaagalia wenzeke wamefanikiwa vipi katki utafiti wa malaria hapo Ifakara.Ofisa uhamiahaji anakutana naye anaomba passport yake anamwambia wewe umepewe visa ambayo siyo lazima ulipe tena CTA mzungu anasema mimi nimeenda ubalozini nikaaambia nataka kwenda Ifakara kwa hiyo vist akagongewa visa kafiak Ifakara.Afisa uhamiaji anambiwa mimi sikuambiwa kama kuna malipo yoyote hapo Tanzania je kwa nini nilipe tena?Afisa uhamiaji anampleka polisi lakini baadae anachiwa je huyu mgeni anakosa gani?Kwa nini afisa uhamiaji asifike kwa wenji wake na kuwapa maelezo?Na kisa cha kwenda polisi ni baada ya kuombwa kitu kidogo na kukataa na baadae polisi afisi uhamiajia anasema jaamaa kamkataza kufanya kazi yake kwa makudi no nd maellezo aliyoandika polisi huyo jamaa wa Uhamiaji

Nadhani unahamaki kwa usilolijua na inaelekea hutaki kuelewa. Mgeni wako aliambiwa aliyonayo ni visa ya matembezi (tourist visa) na sio ya kufanya hayo ayafanyayo (temporary assignment). Afisa uhamiaji kumtaka apate kibali stahiki unaona anakosea?!!!!! Huitendei haki Tanzania. Kwa vile ni mmarekani unaona anabughuziwa, akiwa mchina pengine utabadili mawazo. Nikuulize...unauhakika gani kuwa huko ubalozini aliwaeleza kuwa anakuja kufanya hicho alichokutwa akifanya? Usilete mada za kishabiki shabiki. All in all, wameshakueleza hapo juu, balozi zetu ziko chini ya wizara ya mambo ya nje, uhamiaji wapo mambo ya ndani. Ukifanya utafiti mdogo tu... utagundua ni balozi chache sana zilizo na maafisa uhamiaji wakifanya kazi zao huko. Dawati la uhamiaji kwenye balozi nyingi zinafanywa na maafisa toka mambo ya nje! Kwa msingi huu makosa....au mtu kutoelimishwa vilivyo akiwa huko huko hutokea. Wewe unamlaumu tu afisa uhamiaji wa Ifakara bila kujaribu kuchanganua mambo. Yanamwisho hayo...alisema Rashid.
 
Back
Top Bottom