Visa gani pombe ilikufanyia hutasahau?

Kuna siku nilikuwa napanda daladala naenda nyumbani, mwaka wa nne chuo kikuu. ile kufika kwenye daladala nikakuta kuna wanaume wawili wanapigana, kuangalia ni conductor na abiria. kumwangalia abiria ni mjomba wangu alikuwa na miaka kama 55 hivi, pande la mtu. kumbe mjomba alikuwa amekunywa pombe, zilimzidi na alijisaidia haja kubwa (ninasema hili kwa uchungu kwasababu nilipata aibu mno), suruali kwa nyuma ililowa kabisa naona mapombe yalitoka kama yalivyo, sasa alipokaa kwenye daladala abiria wakaanza kumkimbia, konda kumshusha wakaoshe gari kwa nguvu ndio ngumi zile nilizikuta, yeye anaona anaaibishwa, watu wamekusanyika wanamwangalia. niwe mkweli, nilijifanya simjui (nadhani ni utoto kwasababu nilikuwa mwanafunzi wa chuo bado na sikuwa na pesa ya kumchukulia taxi na kwasababu hakuniona na nilisimama distance, niliondoka eneo lile).

ajabu yake, hakuachaga pombe hadi anakufa pamoja na aibu kubwa namna hii. dereva kaondoa daladala kaenda kuiosha anapiga kelele ati daladala yangu yote inanuka choo. this is a true story.
Duuuh yani mtu anajinyea kabisa tena kwenye daladala hizi stori hua ni kweli lakini!! Napata tabu sana kuamini!!
Yani wanakua wanakunywaje mpaka kujinyea!!!
 
Nikwambie kitu mkuu? Kwanza ujue mwili wenyewe unahitaji blood alcohol kwa kiwango flani ili metabolism and digestion zifanye kazi vizuri. Wenzetu wanaoelewa hata maofisini utakuta wameweka chupa za wiskey na glass na hunywa kabla hawajaingia kwenye mikutano au kabla ya presentations maofisini, kwenye mijadara mbalimbali kwasababu kwa kiwango kidogo huchangamsha mwili na akili.

Sisi tunakamia; kuna pombe za kunywa muda mrefu kama uko idle, kuna pombe ya kunywa kama una muda mchache pia kuna pombe zinatengenezwa na matumizi yake yanategemea na mazingira (hali ya hewa whether ni joto, baridi au moderate)

Unakuta pombe unayopaswa kunywa kipindi cha baridi we unaifakamia kwenye mazingira ya joto, unategemea nini? Lazima itakuperekesha au kukuzimisha tu.
Mkuu hbeu nisaidie hapa Valuer iko kwneye kundi ghani?
 
Mkuu hbeu nisaidie hapa Valuer iko kwneye kundi ghani?
Ni aina ya Brandy mkuu
images.jpeg
 
Hapana, mwaka jana ilifanyika analysis ya pombe kali zote sokoni (Serikali ilihusika). Majibu yaliyotoka kwa hizi pombe zilizojizolea umaarufu kwa sababu ya bei, yanatisha sana. Baadhi zina methano ambayo hatutegemei kabisa iwepo. Pombe mojawapo ilikutwa na methanol content mpaka unaogopa.
Hadi leo nashangaa Serikali imepotezea kuchukua hatua dhidi ya janga kubwa kwa wananchi wake. Pombe hizi za 2,000/= nyingi ni hatari sana kwa afya, madhara yake tutayaona muda si mrefu, ni bomu hatari kwelikweli.
Duuh, sinwyi tena pombe. Ngoja ninywe juisi tuu.
 
Duuh, sinwyi tena pombe. Ngoja ninywe juisi tuu.
Pombe zenye viwango hazina shida kabisa ukizinywa kwa nidhamu. Hizi zinazochipukia kama uyoga huku zikiuzwa bei chee, ni hatari sana kwa figo, maini na hata afya ya ubongo. Hawa washenzi wanaongeza methanol kwa makusudi kabisa kupunguza gharama za uzalishaji ili kupata faida kubwa.
 
Back
Top Bottom