Kwa hali ilivyo nchini mwetu namna viongozi wetu wanavyoiendesha nchi, Kwa mikataba ya vificho yenye kuliingiza taifa kwenye hasara mfano ikiwa kuibinafsisha bandari yetu ambayo ni nguzo kuu ya uchumu wetu,na mikataba mingine mingi yenye agenda za Siri tusiyoijua.
Iwapendeze viongozi wetu wa dini zote kuteua siku maalum kwa ajili ya kuliombea taifa,kengele makanisani zipigwe mara 3 kuashiria msiba na maombolezo kwa haya yanayoendelea nchini.
Nimejaribu kufuatilia pia bungeni namna pia msukuma na wenzake bungeni wanavyolipigia debe suala la kuibinafsisha bandari na ziara yake ya Dubai akiwa na kamati ya Mbarawa ambao ni hao hao wanaitumbukiza nchi shimoni.
Na inaashiria kabisa wameandaliwa kwa kazi hiyo kupiga debe kwa kisingizio cha kutuwakilisha wananchi kupitia bunge.
Itoshe kuishia hapa Maana napata maumivu makubwa kushuhudia mambo haya ya hovyo yanayotendwa na watu tuliowaamini na kuwapa dhamana ya kuiongoza nchi.
Ninaomba tumlilie Mungu peke yake ndiye wa kutujibu dhidi ya watesi wetu hawa, tulionao kwenye nchi hii yetu nzuri tuliyopewa na Mungu wetu.
Iwapendeze viongozi wetu wa dini zote kuteua siku maalum kwa ajili ya kuliombea taifa,kengele makanisani zipigwe mara 3 kuashiria msiba na maombolezo kwa haya yanayoendelea nchini.
Nimejaribu kufuatilia pia bungeni namna pia msukuma na wenzake bungeni wanavyolipigia debe suala la kuibinafsisha bandari na ziara yake ya Dubai akiwa na kamati ya Mbarawa ambao ni hao hao wanaitumbukiza nchi shimoni.
Na inaashiria kabisa wameandaliwa kwa kazi hiyo kupiga debe kwa kisingizio cha kutuwakilisha wananchi kupitia bunge.
Itoshe kuishia hapa Maana napata maumivu makubwa kushuhudia mambo haya ya hovyo yanayotendwa na watu tuliowaamini na kuwapa dhamana ya kuiongoza nchi.
Ninaomba tumlilie Mungu peke yake ndiye wa kutujibu dhidi ya watesi wetu hawa, tulionao kwenye nchi hii yetu nzuri tuliyopewa na Mungu wetu.