Viongozi wa nchi watumwa, wananchi wenye nchi watumwa, nani wa kuukomesha utumwa?

Lidafo

JF-Expert Member
Sep 26, 2019
551
747
Dhana ya utumwa imekuwa ikibadilika kulingana na vipindi tofauti vya muda. Enzi za mababu zetu utumwa ulikuwa ni wakufungwa minyonyoro na kufanyishwa kazi ngumu bila ujira. Taifa likaja kupata uhuru ikawalazimu wakoloni kuacha makoloni yao ambapo kiukweli hawakupenda ndio maana wakaendeleza dhana ya utumwa yaani tukawa huru kuendesha mambo yetu wenyewe ila kwa kupangiwa jinsi ya kuyaendesha na mataifa ya nje au na baadhi ya watu ndani ya nchi wanaohisi wana nguvu kuliko serikali hiki ndicho kile kinachoitwa utumwa huru.

Tupo katika utumwa wa fikra, Embu fikiria Hivi ni kweli hatuwezi kuunda sera zetu za elimu bili kuiga mataifa ya nje? Ni kweli hatuwezi kuendesha mambo yetu ya Kiuchumi bila mataifa ya nje (Rejea ishu ya sasa ya bandari na DP World) Hivi ni kweli hatuwezi kuwa na mifumo yetu ya ulinzi na usalama? Ujinga huu ndio uliozaa mambo ya bunge kukosa nguvu dhidi ya serikali, Mahakama kukosa nguvu dhidi ya serikali na serikali kukosa nguvu dhidi ya mabeberu.

Hapa tunaweza sema viongozi ni watumwa, lakini kwa upande mwengine wananchi wamekuwa wakiingilia kati baadhi ya mambo muhimu na kuishauri serikali ila serikali Imekuwa ikipiga teke na kunyamazia maoni ya wananchi, tafsiri yake ni kuwa wananchi nao ni watumwa.

Nani sasa wakukomesha utumwa huu?
 
Utumwa wa fikra ni mbaya na hatari kuliko utumwa wa minyororo, mwafrika ana utumwa wa fikra ambao chanzo chake ni yeye mwenyewe na Wala sio mtu kutoka nje.
 
Rais wetu mjomba Ake ni muomani..kwahiyo anajiona Mwarabu. Tanganyika tuwe makini, bandari - dubai, misitu - saudia arabia, mbuga zetu ( loriondo) - saudia Arab wamejenga hotel na wamasai Wamefukuzwa, Kia (uwanja wa niece)- Omani.

Mtanganyika kuwa makini
 
Utumwa wa fikra ni mbaya na hatari kuliko utumwa wa minyororo, mwafrika ana utumwa wa fikra ambao chanzo chake ni yeye mwenyewe na Wala sio mtu kutoka nje.
Unafikiri kipi kifanyike ili mwafrika aweze kujitoa katika utumwa wa fikra?
 
Rais wetu mjomba Ake ni muomani..kwahiyo anajiona Mwarabu. Tanganyika tuwe makini, bandari - dubai, misitu - saudia arabia, mbuga zetu ( loriondo) - saudia Arab wamejenga hotel na wamasai Wamefukuzwa, Kia (uwanja wa niece)- Omani.

Mtanganyika kuwa makini
Wale ni waarabu tupu
 
Tukumbuke wananchi nao ni watumwa kwa viongozi hili limekaaje?

Hili ni tatizo la wananchi wenyewe, wamewapa nguvu viongozi kiasi kwamba wamekuwa waoga viongozi ndio wamekuwa miungu.

Nchi zingine kiongozi hawez fanya upumbavu. Anajua wananchi watamuondoa chap, huku wananchi ni waoga
 
Hili ni tatizo la wananchi wenyewe, wamewapa nguvu viongozi kiasi kwamba wamekuwa waoga viongozi ndio wamekuwa miungu.

Nchi zingine kiongozi hawez fanya upumbavu. Anajua wananchi watamuondoa chap, huku wananchi ni waoga
Hivyo kitakachopelekea wananchi kujitoa katika uwoga huo ni wananchi wenyewe kuamua kuacha uwoga na kushinikiza viongozi wawajibike
 
Dhana ya utumwa imekuwa ikibadilika kulingana na vipindi tofauti vya muda. Enzi za mababu zetu utumwa ulikuwa ni wakufungwa minyonyoro na kufanyishwa kazi ngumu bila ujira. Taifa likaja kupata uhuru ikawalazimu wakoloni kuacha makoloni yao ambapo kiukweli hawakupenda ndio maana wakaendeleza dhana ya utumwa yaani tukawa huru kuendesha mambo yetu wenyewe ila kwa kupangiwa jinsi ya kuyaendesha na mataifa ya nje au na baadhi ya watu ndani ya nchi wanaohisi wana nguvu kuliko serikali hiki ndicho kile kinachoitwa utumwa huru.

Tupo katika utumwa wa fikra, Embu fikiria Hivi ni kweli hatuwezi kuunda sera zetu za elimu bili kuiga mataifa ya nje? Ni kweli hatuwezi kuendesha mambo yetu ya Kiuchumi bila mataifa ya nje (Rejea ishu ya sasa ya bandari na DP World) Hivi ni kweli hatuwezi kuwa na mifumo yetu ya ulinzi na usalama? Ujinga huu ndio uliozaa mambo ya bunge kukosa nguvu dhidi ya serikali, Mahakama kukosa nguvu dhidi ya serikali na serikali kukosa nguvu dhidi ya mabeberu.

Hapa tunaweza sema viongozi ni watumwa, lakini kwa upande mwengine wananchi wamekuwa wakiingilia kati baadhi ya mambo muhimu na kuishauri serikali ila serikali Imekuwa ikipiga teke na kunyamazia maoni ya wananchi, tafsiri yake ni kuwa wananchi nao ni watumwa.

Nani sasa wakukomesha utumwa huu?
20230702_083536.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ni mfumo mbovu wa CCM
Sitaki kukubaliana wala kupingana na wewe, Watanzania inatupasa tujitathmini sana kwanza tusiamini sana kama Chama cha siasa ndiyo mkombozi wa matatizo yetu, bado tupo kwenye utumwa wa kuamini Samaki mmoja akioza basi wote wameoza. vyama vyote vya Siasa havina tofauti maana viongozi wake ni wanaadam wenye miili na fikra zinazolingana. sitaki kuamini kwamba CCM ni mbaya moja kwa moja ila kuna watu ndani ya CCM ambao wanaitia doa ionekane ni mbaya, hivyohivyo kwa Chadema, ATC Nk. Wanasiasa hawa usione wanalumbana na kutoleana maneno mabaya mengine hata tukadhani ni kutishiana maisha, hawa wanatuzubaisha tu, wakiwa chemba wote wanaongea lugha moja matokeo yake Wananchi ndiyo tunayumbishwa tunakosa msimamo wakati wao maisha yanaendelea kuwanyookea (Tukumbuke kwamba Vyama na wanasiasa, sisi Wananchi ndiyo Mtaji wao na ndiyo tumewaweka hapo walipo).
Kwahiyo katika hivi vyama tariban vyote vinakuwa na sera na mitizamo mizuri sana lakini ndani ya hivyo vyama ndiyo kuna vivuruge! Unaweza kuta ndani ya CCM watu wanaoifanya ionekane ni ya ovyo hawazidi 20 lakini humo humo kuna wazalendo waliopitiliza! hivyo ushauri wangu ni Wananchi kujitafakari. kutafuta njia ya kudeal na hawa wachumia tumbo kuliko kutoa hizo lawama na kuonesha moja kwa moja kukata tamaa kwa kulalamikia chama moja kwa moja wakati hivi vyama ni sisi Wananchi ndiyo tumeviweka.
 
Back
Top Bottom