Jodoki Kalimilo
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 12,013
- 10,170
Kazi ipo katika kuleta mabadiliko maana leo katika kuangalia taarifa ya habari star tv nimeshuhudia viongozi wa kisiasa wakisusia kikao kisa mkuu wa wilaya amewatangazia kuwa hakuna posho. Kilichonisikitisha wengi waliokataa ni kutoka vyama vya mageuzi hapa ndipo nilipoona kwamba tuna safari ndefu kat kuondoa hizi posho zisizo na tija hasa ukizingatia kilichotakiwa ni uwepo wa wajumbe pia mawazo yao yalikuwa ni ya muhimu zaidi kuliko hizo posho kwani wajumbe wote walikuwa ni kutoka Tabora mjini na kikao kilikuwa ni sehemu ya kazi yao kama wanasiasa. CHADEMA kweli wapo serious na hii issue za posho maana wao waliendelea na kikao pamoja na kwamba kilikuwa hakina posho nadhani huu ni mwanzo mzuri wa kupinga seating allowance kwani tutakuwa na mahudhurio mengi ya watu waliofuata posho lakini mchango / mawazo ya maendeleo inakuwa hakuna.