Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
VIONGOZI wa dini ya kiislamu wakiwemo mashehe na maimamu wamepinga kampeni ya Taifa dhidi ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango nchini. Hayo yalijulikana jana katika semina iliyowashirikisha viongozi hao wa dini iliyowataka watambue juu ya matumizi ya njia hizo Mkoani Kilimanjaro.
Kampeni hiyo ya Taifa ambayo ipo kwenye michakato ya kuwakutanisha viongozi wa dini mbalimbali nchini ili wapewe elimu ya njia hizo na wao wakawafikishie wananchi na kuwapa hamasa juu ya matumizi ya njia hizo.
Viongozi hao walipinga vikali juu ya kampeni hiyo na kusema kuwa hawatahamasisha jamii kwa kuwa njia hizo zinakwenda kinyume na maandiko ya dini hiyo.
Wakizungumza kwa masikitiko baadhi ya mashehe na viongozi wengine wa dini hiyo ya kiislamu wakiwemo na walimu wanawake wamesema kuwa kutokana na maandiko ya dini ya kiislamu kampeni hiyo ambayo wamepatiwa elimu wao hawataitekeleza kwa kuwa ni kinyume na maandiko ya dini.
Wamesema kuwa njia hizo kwanza ni kama ni kumkufuru mwenyezi mungu kwa kuwa yeye hakusema binadamu wazuie uzazi na kusema aliwataka wanadamu waje kuujaza ulimwengu na sio kuzuia kizazi.
Wamesema kuwa kampeni hiyo wanaipinga vikali na hawatawaambia waumini wao watumie njia hizo wao watawaelimsha waumini wao kulingana na maandiko yanavyosema.
Afisa Mipango zoezi la Mpango wa Uzazi wa Mpango Taifa, Bw. Safiel amesema kuwa, wanawakutanisha viongozi wa dini hao na wameonekana kama kutofahamu lengo la Taifa, na dhumuni la kuwakutanisha ni kutaka watambue njia hizo na waelimishe jamii juu ya njia hizo zinazoonekana wananchi walio wengi hawazitambui.
Na kusema kuwa sio kwamba wanawazuia wananchi wasizae bali kwa kudhibiti wimbi la watoto ambao hawapati huduma stahili kutoka kwa wazazi wao na vilevile kuelimisha jamii kuzaa kulingana na uwezo walio nao.
Chanzo: Nifahamishe
Kampeni hiyo ya Taifa ambayo ipo kwenye michakato ya kuwakutanisha viongozi wa dini mbalimbali nchini ili wapewe elimu ya njia hizo na wao wakawafikishie wananchi na kuwapa hamasa juu ya matumizi ya njia hizo.
Viongozi hao walipinga vikali juu ya kampeni hiyo na kusema kuwa hawatahamasisha jamii kwa kuwa njia hizo zinakwenda kinyume na maandiko ya dini hiyo.
Wakizungumza kwa masikitiko baadhi ya mashehe na viongozi wengine wa dini hiyo ya kiislamu wakiwemo na walimu wanawake wamesema kuwa kutokana na maandiko ya dini ya kiislamu kampeni hiyo ambayo wamepatiwa elimu wao hawataitekeleza kwa kuwa ni kinyume na maandiko ya dini.
Wamesema kuwa njia hizo kwanza ni kama ni kumkufuru mwenyezi mungu kwa kuwa yeye hakusema binadamu wazuie uzazi na kusema aliwataka wanadamu waje kuujaza ulimwengu na sio kuzuia kizazi.
Wamesema kuwa kampeni hiyo wanaipinga vikali na hawatawaambia waumini wao watumie njia hizo wao watawaelimsha waumini wao kulingana na maandiko yanavyosema.
Afisa Mipango zoezi la Mpango wa Uzazi wa Mpango Taifa, Bw. Safiel amesema kuwa, wanawakutanisha viongozi wa dini hao na wameonekana kama kutofahamu lengo la Taifa, na dhumuni la kuwakutanisha ni kutaka watambue njia hizo na waelimishe jamii juu ya njia hizo zinazoonekana wananchi walio wengi hawazitambui.
Na kusema kuwa sio kwamba wanawazuia wananchi wasizae bali kwa kudhibiti wimbi la watoto ambao hawapati huduma stahili kutoka kwa wazazi wao na vilevile kuelimisha jamii kuzaa kulingana na uwezo walio nao.
Chanzo: Nifahamishe