JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Katika kuenzi miaka 24 ya kifo cha baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Juma Chikoka ameandaa bonanza la michezo mbalimbali kwa vijana wilayani hapo.
DC Chikoka anasema kuwa lengo la bonanza hilo ni kuendeleza kutoa elimu na mwamko kwa vijana kukumbuka na kuenzi yote mazuri aliyoyafanya Muasisi wa Taifa letu Hayati Julius Nyerere.
Bonanza lilianza na jogging na baadaye kuwa mechi za mpira wa miguu kwa Wanawake na Wanaume.
DC amesisitiza kuendeleza umoja, mshikamano na uzalendo kama njia ya kumuenzi Baba wa Taifa.
DC Chikoka anasema kuwa lengo la bonanza hilo ni kuendeleza kutoa elimu na mwamko kwa vijana kukumbuka na kuenzi yote mazuri aliyoyafanya Muasisi wa Taifa letu Hayati Julius Nyerere.
DC amesisitiza kuendeleza umoja, mshikamano na uzalendo kama njia ya kumuenzi Baba wa Taifa.