Rebo Tz
Senior Member
- Sep 26, 2016
- 169
- 124
Habari wana Jf habari za mchana mm si mjuaji sana ila kwanza tukumbushane hili kidodo...
KARIBU...
Vijana wengi nchini Tanzania hasa tulio na miaka ya kuanzia inshirini na kuendeea tunakuwa tumekumbwa na fikra hasi ambazo zinatufanya tuwe na hisia ya kupoteza malengo yetu ya baadae.
Ili kuokoa kizazi kinachopotea na fikra potofu inabidi kijana wa leo kufungua macho na kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa kuacha lawama kila uchwao kwa serikali kwa kuwa na mawazo yafuatayo;
TUACHE LAWAMA...,vijana wengi wa kitanzania tumekuwa wengi wa lawama kuliko ufanyaji wa kazi. Jamani tushtuke kwani utakuta unavuta shuka wakati kumekucha, suala la kujiona mtoto na kuishi kwenye ndoto kuwa “You still have time, aaaah Its a big No”, inabidi tuendane na mazingira.
“MIMI NINABAHATI MBAYA”, huu ni usemi kwa vijana wengi hasa wale tulio na fikra hafifu kwani tunakuwa tunahisi kuna dhana ya ushirikina na kusababisha maisha ya vijana wengi kuingia katika tabia hasi kama pombe,uvutaji wa bangi na ukahaba, na kuacha kufanya kazi kwa bidii ili kujiokoa kwenye kaburi la umasikini na ujinga.
TUEPUKE NA MARAFIKI,MAKUNDI YASIYO NA TIJA..,najua kwa kizazi hiki ambacho wengi ukiita kwa doti komu,tunapenda marafiki wa kujionesha kwenye mitandao ya kijamii na kula bata lakini hata kama kijana damu yako inachemka inabidi uanagalie maisha yako ya baadaye kwani siku hazigandi na umri unakwenda...
TUACHE TABIA YA KUIGA MAMBO YA KIJINGAA....,hii ni tabia ambayo kuiacha inahitaji msaada wa kisaikolojia,kwani hapa ndo tunawazika vijana wengi sana,tabia ya kuiga inakupelekea kwenye tamaa ambazo zinaweza kukusababishia magonjwa,kufungwa jela kwa wizi na matukio yasio na maadili kama ujambazi na mengineyo.
.·.Kwa hiyo, vijana tuamke na tuache kuishi kwenye ndoto bali tufungue macho na tusonge mbele...
KARIBU...
Vijana wengi nchini Tanzania hasa tulio na miaka ya kuanzia inshirini na kuendeea tunakuwa tumekumbwa na fikra hasi ambazo zinatufanya tuwe na hisia ya kupoteza malengo yetu ya baadae.
Ili kuokoa kizazi kinachopotea na fikra potofu inabidi kijana wa leo kufungua macho na kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa kuacha lawama kila uchwao kwa serikali kwa kuwa na mawazo yafuatayo;
TUACHE LAWAMA...,vijana wengi wa kitanzania tumekuwa wengi wa lawama kuliko ufanyaji wa kazi. Jamani tushtuke kwani utakuta unavuta shuka wakati kumekucha, suala la kujiona mtoto na kuishi kwenye ndoto kuwa “You still have time, aaaah Its a big No”, inabidi tuendane na mazingira.
“MIMI NINABAHATI MBAYA”, huu ni usemi kwa vijana wengi hasa wale tulio na fikra hafifu kwani tunakuwa tunahisi kuna dhana ya ushirikina na kusababisha maisha ya vijana wengi kuingia katika tabia hasi kama pombe,uvutaji wa bangi na ukahaba, na kuacha kufanya kazi kwa bidii ili kujiokoa kwenye kaburi la umasikini na ujinga.
TUEPUKE NA MARAFIKI,MAKUNDI YASIYO NA TIJA..,najua kwa kizazi hiki ambacho wengi ukiita kwa doti komu,tunapenda marafiki wa kujionesha kwenye mitandao ya kijamii na kula bata lakini hata kama kijana damu yako inachemka inabidi uanagalie maisha yako ya baadaye kwani siku hazigandi na umri unakwenda...
TUACHE TABIA YA KUIGA MAMBO YA KIJINGAA....,hii ni tabia ambayo kuiacha inahitaji msaada wa kisaikolojia,kwani hapa ndo tunawazika vijana wengi sana,tabia ya kuiga inakupelekea kwenye tamaa ambazo zinaweza kukusababishia magonjwa,kufungwa jela kwa wizi na matukio yasio na maadili kama ujambazi na mengineyo.
.·.Kwa hiyo, vijana tuamke na tuache kuishi kwenye ndoto bali tufungue macho na tusonge mbele...