T14 Armata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2017
- 10,751
- 35,317
Kuna watu wanauza trust na aesthetics kwenye hiyo biashara, wengi wao wauza simu. Huwezi uza iPhones kwenye duka lenye sakafu na mabenchi wateja hawatoamini kama hata warranty watapata.
Huu uzi sio sheria. Ni ushauri tu. Kama huu ushauri hauendani na biashara yako inavyotaka basi ni vyema na sahihi kutoufuataKuna watu wanauza trust na aesthetics kwenye hiyo biashara, wengi wao wauza simu. Huwezi uza iPhones kwenye duka lenye sakafu na mabenchi wateja hawatoamini kama hata warranty watapata.
Umepanick, hakuna nilipodai uzi ni sheria. Labda useme umejiandikia mwenyewe kwamba watu wasichangie. Si lazima kila mtu awe na mtazamo wako, mtazamo wangu na wako ni tofauti.Huu uzi sio sheria. Ni ushauri tu. Kama huu ushauri hauendani na biashara yako inavyotaka basi ni vyema na sahihi kutoufuata
Punguza uogaUmepanick, hakuna nilipodai uzi ni sheria. Labda useme umejiandikia mwenyewe kwamba watu wasichangie. Si lazima kila mtu awe na mtazamo wako, mtazamo wangu na wako ni tofauti.
Inategemea na biashara, kuna maduka mengi ya vijana yanauza kwa mali kauli. Anaweka nguvu kwenye marketing na aesthetics maana mtaji haufanyi lolote kwenye inventory. Na wanauza sana tu sometimes kupita wenye maduka. Biashara halijawahi kuwa suala la kukaririshwa. Ever-changing business environment
Decoration au branding ni sehemu ya mtaji mkuu kuna biashara lazima ufanye rebranding kuendena na biashara yako mada yako haija taja biashara ya aina gani isio hitaji decoration kali.....acha ku generalise mkuu.Mojawapo ya kosa kubwa sana la kiufundi kwa vijana wengi wadogo wanaoanza biashara ni kuwekeza pesa nyingi kwenye vitu ambavyo havirudishi pesa kwa haraka au pengine havirudishi kabisa. Vijana wanafungua maduka ila wengie hawafikishi mwaka mmoja wamefunga baada ya kushindwa biashara.
Vijana wanafanya makosa mbalimbali ya kiufundi ila kosa lililoshika kasi zaidi ni kutumia pesa nyingi sana kufanya decorations ya duka badala ya kununua mzigo wa kutosha. Imekuwa kawaida kuona bajeti ya decorations milioni 5 halafu mzigo wa dukani milioni 3. Ukiliona duka kwa nje ni zuri balaa hadi ndani ila mzigo ni mdogo usioendana na hadhi ya duka. Wengine hufanga kosa zaidi kwa kuteketeza pesa kufanya sherehe ya uzinduzi wa duka (launching party).
Ninawashauri vijana wakiwa wanafungua duka wafanye decorations za kiasi kidogo sana ila baadae wakijaliwa watafanya decorations kali kwa kutumia sehemu ya faida iliyopatikana kwenye biashara. Vijana acheni kushangilia ushindi wakati hata mechi bado. Hakikisheni mnanunua stock ya kutosha. Huo ndo usalama wa biashara.
Mkuu tofautisha decorating and advertising hivi ni vitu viwili tofauti, kutangaza huduma usio nao kunauua huduma hata zingine ata ulizo nazo.Umeweka mabango ya tigopesa, airtel money, mpesa, Crdb, nmb nk tena mabango makubwa. Halafu mtu anakuja kuhitaji huduma ya crdb unamwambia bado hatuna mashine. Hii ipo sana, decorating an office ni gharama kubwa sana, japo kuna ofisi bila decorations haiuzi.
Ni ushauri tu sio lazima kuufuataDecoration au branding ni sehemu ya mtaji mkuu kuna biashara lazima ufanye rebranding kuendena na biashara yako mada yako haija taja biashara ya aina gani isio hitaji decoration kali.....acha ku generalise mkuu.
Mfano mzuri sana huu.. juzi nilikua natafuta saloon ya kunyoa.. kila saloon nikiiona naona hii ni zile saloon za kishua kunyoa 10,000. Sababu ya decoration na madoido waliyoweka.. siingii saloon hizo.. nkatafuta mpaka nkaona saloon zile za kawaida ndo nkaingia..Hizo decoration wakati fulani zinaweza kuwakimbiza wateja wakihisi kwa uwezo wao hawawezi kununua bidhaa zilizomo kwa kudhani bei itakuwa ghali sana, kuna bucha fulani lilifunguliwa limefanyiwa decorations za kufa mtu mpk unahisi humu kweli nikitaka nyama robo wanapima kweli!! Au bei yake ndiyo hii sawa na bucha za kawaida
Basi inabidi ulipite tu uende bucha za kawaida hizi mpk walipobandika bei ndiyo mtu anafahamu kumbe bei sawa tu ni mbwembwe tu decorations hata wanyonge wanaweza kuingia
Mkuu bango linatengenezwa kwa gharama, mtu hana hela ya kuchezea eti aweke Tigopesa na M-Pesa tu miezi mitatu baadae akiweka na CRDB achane bango aweke bango jipya.Umeweka mabango ya tigopesa, airtel money, mpesa, Crdb, nmb nk tena mabango makubwa. Halafu mtu anakuja kuhitaji huduma ya crdb unamwambia bado hatuna mashine. Hii ipo sana, decorating an office ni gharama kubwa sana, japo kuna ofisi bila decorations haiuzi.
Unawasema wauza nyanya na mifuko ya plastiki si ndio? Sasa decorations kwenye banda la nyanya ya nini. Tafuta Wachaga wauza electronics, accessories & gadgets uone kama hawajafanya decorationsBiashara wajifunze kwa wachaga aloo mchaga aweke decoration ya ml1 weeh