Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Vigogo wanane kortini kwa ufisadi
Vigogo wanane kortini kwa ufisadi
Waandishi Wetu
VIGOGO wanane wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni wakikabiliwa na mashtaka 45 tofauti.
Mashtaka ya watendaji hao wa Manispaa ya Kinondoni yamegawanyika katika sehemu kuu mbili ikiwemo kutumia madaraka vibaya pamoja na kutoa taarifa za uongo kwa mkurugenzi wa Manispaa hiyo.
Washtakiwa hao ambao walifikishwa mahakamani hapo jana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ni pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Ardhi Manispaa ya Kinondoni, Hamidu Mgaya, Ofisa Mtendaji Kilongawima Mbezi, Wanura Maranda, Mwenyekiti wa mtaa Kilongawima Mbezi, Francis Woiso na Diwani wa kata ya Kunduchi, Patrick Makoyola.
Watuhumiwa hao kwa pamoja walisomewa mashtaka hayo na Mwendesha Mashitaka wa Takukuru, Leonard Swai, ambaye aliieleza mahakama kuwa watuhumiwa hao wamevunja kifungu namba 31 cha kuzuia na kupambana na rushwa kwa kutumia madaraka yao vibaya pamoja na kutoa taarifa za uongo kwa waajiri wao.
Swai alidai mbele ya Hakimu Yohana Yongolo wa mahakama hiyo kuwa, mnamo mwezi Juni na Julai mwaka 2008, watendaji wa hao walitoa taarifa za uongo kwa mkurugenzi wao zikionyesha kuwa eneo ambalo lililopo katika michoro ya mipango miji namba TR.DRG. 1/12/8001 kuwa linamilikiwa na Athumani Mahimbo ambapo walimsajili kwa namba ya eneo 2466 Block L Mbezi.
Swai alidai kuwa watuhumiwa hao walifanya jambo hilo huku wakijua kuwa ni kosa na kwamba mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni asingelikubali hilo endapo angepewa maelezo sahihi.
Wengine waliofikishwa mahakamani hapo na Takukuru ni Anna Macha ambaye ni Ofisa Mipango Miji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mapambano Baseka (Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Kinondoni), Said Waligwah (Ofisa Mtafiti wa ardhi Manispaa ya Kinondoni) na Hamidu Mgaya (Ofisa ardhi manispaa ya Kinondoni).
Swai alidai kuwa watuhumiwa hao walitumia madaraka yao vibaya na kuvunja kifungu cha sheria namba 12(1) cha mwaka 1999 namba nne katika sheria ya michoro ya mipango miji kwa kummilikisha Kheri Mabira eneo walilolisajili kwa namba 2473 lililoko Block L Mbezi.
Swai alidai eneo hilo ni la wazi ambalo lilitengwa na serikali kwa matumizi ya umma.
Watuhumiwa wote walikana na mashtaka hayo na walipata dhamana baada ya wadhamini kukubaliana na masharti waliosomewa na hakimu.
Hata hivyo, watuhumiwa saba kati ya nane ndiyo walifika mahakamani hapo huku Patrick Makoyola akikosekana, ambapo mahakama iliamuru atafutwe na polisi na kufikishwa mahakamani hapo.
Hata hivyo, Hakimu Yongolo alisema kesi hiyo itasomwa tena Julai 26 mwaka huu.
Chanzo: Mwananchi
My Take:
Vipi hawa PCCB kazi yao kubwa ni kufungua mashitaka dhidi ya kutoa taarifa za uongo. Kwa nini huwa hakuna mashitaka ya kupokea rushwa au wizi,i nk?