Vigogo wanane wa manispaa ya K'ndoni kortini kwa ufisadi

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234

Vigogo wanane kortini kwa ufisadi


Vigogo wanane kortini kwa ufisadi

Waandishi Wetu

VIGOGO wanane wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni wakikabiliwa na mashtaka 45 tofauti.

Mashtaka ya watendaji hao wa Manispaa ya Kinondoni yamegawanyika katika sehemu kuu mbili ikiwemo kutumia madaraka vibaya pamoja na kutoa taarifa za uongo kwa mkurugenzi wa Manispaa hiyo.

Washtakiwa hao ambao walifikishwa mahakamani hapo jana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ni pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Ardhi Manispaa ya Kinondoni, Hamidu Mgaya, Ofisa Mtendaji Kilongawima Mbezi, Wanura Maranda, Mwenyekiti wa mtaa Kilongawima Mbezi, Francis Woiso na Diwani wa kata ya Kunduchi, Patrick Makoyola.

Watuhumiwa hao kwa pamoja walisomewa mashtaka hayo na Mwendesha Mashitaka wa Takukuru, Leonard Swai, ambaye aliieleza mahakama kuwa watuhumiwa hao wamevunja kifungu namba 31 cha kuzuia na kupambana na rushwa kwa kutumia madaraka yao vibaya pamoja na kutoa taarifa za uongo kwa waajiri wao.

Swai alidai mbele ya Hakimu Yohana Yongolo wa mahakama hiyo kuwa, mnamo mwezi Juni na Julai mwaka 2008, watendaji wa hao walitoa taarifa za uongo kwa mkurugenzi wao zikionyesha kuwa eneo ambalo lililopo katika michoro ya mipango miji namba TR.DRG. 1/12/8001 kuwa linamilikiwa na Athumani Mahimbo ambapo walimsajili kwa namba ya eneo 2466 Block L Mbezi.

Swai alidai kuwa watuhumiwa hao walifanya jambo hilo huku wakijua kuwa ni kosa na kwamba mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni asingelikubali hilo endapo angepewa maelezo sahihi.

Wengine waliofikishwa mahakamani hapo na Takukuru ni Anna Macha ambaye ni Ofisa Mipango Miji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mapambano Baseka (Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Kinondoni), Said Waligwah (Ofisa Mtafiti wa ardhi Manispaa ya Kinondoni) na Hamidu Mgaya (Ofisa ardhi manispaa ya Kinondoni).

Swai alidai kuwa watuhumiwa hao walitumia madaraka yao vibaya na kuvunja kifungu cha sheria namba 12(1) cha mwaka 1999 namba nne katika sheria ya michoro ya mipango miji kwa kummilikisha Kheri Mabira eneo walilolisajili kwa namba 2473 lililoko Block L Mbezi.
Swai alidai eneo hilo ni la wazi ambalo lilitengwa na serikali kwa matumizi ya umma.

Watuhumiwa wote walikana na mashtaka hayo na walipata dhamana baada ya wadhamini kukubaliana na masharti waliosomewa na hakimu.

Hata hivyo, watuhumiwa saba kati ya nane ndiyo walifika mahakamani hapo huku Patrick Makoyola akikosekana, ambapo mahakama iliamuru atafutwe na polisi na kufikishwa mahakamani hapo.

Hata hivyo, Hakimu Yongolo alisema kesi hiyo itasomwa tena Julai 26 mwaka huu.

Chanzo: Mwananchi



My Take:

Vipi hawa PCCB kazi yao kubwa ni kufungua mashitaka dhidi ya kutoa taarifa za uongo. Kwa nini huwa hakuna mashitaka ya kupokea rushwa au wizi,i nk?
 
mbona kinondoni iko ivi.jana machozi yamenitoka baada ya kuona wamachinga walioko ndani ya stendi ya mwenge anakaguliwa na baunsa atoe risiti kwa ajili ya kuuza mahindi ya kuchoma ndani ya stendi.hii ni bila risiti ukikataa inakuwa shida kwako.jamani viongozi wenye dhamana na nchii hii hili jambo linakatisha tamaa jamani
 
hakuna kitu TAKURUKU wanajisafisha kama kweli vidume wamtoe chenge uraiani BAE na JK richmond
 

Vigogo wanane kortini kwa ufisadi


Vigogo wanane kortini kwa ufisadi

Waandishi Wetu

VIGOGO wanane wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni wakikabiliwa na mashtaka 45 tofauti.

Mashtaka ya watendaji hao wa Manispaa ya Kinondoni yamegawanyika katika sehemu kuu mbili ikiwemo kutumia madaraka vibaya pamoja na kutoa taarifa za uongo kwa mkurugenzi wa Manispaa hiyo.

Washtakiwa hao ambao walifikishwa mahakamani hapo jana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ni pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Ardhi Manispaa ya Kinondoni, Hamidu Mgaya, Ofisa Mtendaji Kilongawima Mbezi, Wanura Maranda, Mwenyekiti wa mtaa Kilongawima Mbezi, Francis Woiso na Diwani wa kata ya Kunduchi, Patrick Makoyola.

Watuhumiwa hao kwa pamoja walisomewa mashtaka hayo na Mwendesha Mashitaka wa Takukuru, Leonard Swai, ambaye aliieleza mahakama kuwa watuhumiwa hao wamevunja kifungu namba 31 cha kuzuia na kupambana na rushwa kwa kutumia madaraka yao vibaya pamoja na kutoa taarifa za uongo kwa waajiri wao.

Swai alidai mbele ya Hakimu Yohana Yongolo wa mahakama hiyo kuwa, mnamo mwezi Juni na Julai mwaka 2008, watendaji wa hao walitoa taarifa za uongo kwa mkurugenzi wao zikionyesha kuwa eneo ambalo lililopo katika michoro ya mipango miji namba TR.DRG. 1/12/8001 kuwa linamilikiwa na Athumani Mahimbo ambapo walimsajili kwa namba ya eneo 2466 Block L Mbezi.

Swai alidai kuwa watuhumiwa hao walifanya jambo hilo huku wakijua kuwa ni kosa na kwamba mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni asingelikubali hilo endapo angepewa maelezo sahihi.

Wengine waliofikishwa mahakamani hapo na Takukuru ni Anna Macha ambaye ni Ofisa Mipango Miji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mapambano Baseka (Ofisa Ardhi wa Manispaa ya Kinondoni), Said Waligwah (Ofisa Mtafiti wa ardhi Manispaa ya Kinondoni) na Hamidu Mgaya (Ofisa ardhi manispaa ya Kinondoni).

Swai alidai kuwa watuhumiwa hao walitumia madaraka yao vibaya na kuvunja kifungu cha sheria namba 12(1) cha mwaka 1999 namba nne katika sheria ya michoro ya mipango miji kwa kummilikisha Kheri Mabira eneo walilolisajili kwa namba 2473 lililoko Block L Mbezi.
Swai alidai eneo hilo ni la wazi ambalo lilitengwa na serikali kwa matumizi ya umma.

Watuhumiwa wote walikana na mashtaka hayo na walipata dhamana baada ya wadhamini kukubaliana na masharti waliosomewa na hakimu.

Hata hivyo, watuhumiwa saba kati ya nane ndiyo walifika mahakamani hapo huku Patrick Makoyola akikosekana, ambapo mahakama iliamuru atafutwe na polisi na kufikishwa mahakamani hapo.

Hata hivyo, Hakimu Yongolo alisema kesi hiyo itasomwa tena Julai 26 mwaka huu.

Chanzo: Mwananchi



My Take:

Vipi hawa PCCB kazi yao kubwa ni kufungua mashitaka dhidi ya kutoa taarifa za uongo. Kwa nini huwa hakuna mashitaka ya kupokea rushwa au wizi,i nk?
..Wameshtakiwa kwa kosa la Matumizi mabaya ya madaraka,kusema uwongo na kujipatia manufaa kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na kupambana na Rushwa No.11,2007. Yote hayo ni makosa ya Jinai mzee
 
huyo mwandishi anaandika taarifa bila kufanya utafiti wa kina, waandishi bana. hamidu mgaya sio mkuu wa kitengo cha ardhi na wala sio afisa ardhi. Mgaya alikua mkuu wa kitengo cha upimaji na ramani na yeye ni mpima wa ardhi, pia mapambano baseka ni afisa mipango miji na wala sio afisa ardhi. Waandishi msiwe wavivu kufanya utafiti wa habari kwani mnaupotosha umma
 
hao nao ni vigogo? vigogo wapo wanaendelea kuitafuna nchi huku wako kwenye viyoyozi hizo ni kafara ili takukuru ionekana inafanya kazi.
 
Back
Top Bottom